WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, October 6, 2012

Tanzania Itaendelea Kutatua Mgogoro Na Malawi


 


 NA MAGRETH KINABO – MAELEZO
 6/10/2012
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe amesema kuwa Tanzania itaendelea kutafuta msuluhishi wa mgogoro wa mpaka kati ya Malawi na Tanzania  kuhusu ziwa Nyasa  iwapo nchi hiyo haitaweza kuja kwenye meza ya mazungumzo  juu ya suala hilo kwa kuchukua hatua mbalimbali.
Mazungumzo ya mgogoro huo ambayo yangetarajiwa kuanzia Oktoba 7 hadi 10, mwaka huu, kinachotarajiwa kufanyika jijini Dares Salaam.
Aidha  Waziri Membe alitoa pendekezo kwa serikali  ya Malawi kwa kuiomba kuwa ikubali timu mbili zilizokuwa katika mazungumzo hayo zikaendelea kukutana ili kuweza kupendekeza msuluhishi  wa tatizo hilo kwa pamoja.
 Kauli hiyo ilitolewa leo  na Waziri huyo katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mara baada ya ziara kurejea  nchini hapa kutoka Canada  alipokuwa akihudhuria mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa usiku wa kuamkia leo  kuhusu  hatua ya serikali ya  Malawi kuandika barua  mbili kwa serikali ya Tanzania mwishoni mwa mwezi uliopita.
Ambapo alisema wamesitushwa na uamuzi huo ,kabla ya kujibu barua hizo.
“Ikiwa Malawi hawatakuja katika meza ya mazungumzo tutaendelea kutafuta msuluhishi juu ya tatizo hili. Tumeamua kulimaliza suala hili chini ya uongozi wa Rais wa Awamu ya Nne ya Rais Jakaya Kikwete kwa kutumia timu za wataalamu tatu, ambazo ni wakumbukumbu ambao wataishia kuchukuia kumbukumbu za maisha ya ziwa hili kabla na baada ya mwaka 1890 nchini Uingereza, pia kukupitia nyaraka mbalimbali itakazozitumia ”alisema . Waziri Membe.
Waziri Membe  alitaja timu nyingine kuwa ni za wanasheria ambapo Mwanasheria Mkuu wa Serikali atahusishwa ili kuangalia namna ya kutoa tamko katika Mahakama ya Kimataifa ya Utatuzi wa Migogoro(ICJ) kuitambua na timu yake ya washauri yenye ujumbe wa watu 14.
Aliongeza kuwa  tatizo hilo pia linaweza kushughulikiwa na marais wastaafu wa Nchi zilizo katika Jumuia ya Maendeleo ya Uchumi ya  Kusini mwa Afrika (SADC), kupendekeza mtu wa kusuluhisha mgogoro huo kwa kupendekeza majina matatu na kutumia  kitengo cha usuluhushi wa migogoro chini ya Umoja wa nchi za Afrika wanaweza kuja kusuluhisha.
Hata hivyo alisema kuwa Malawi haiwezi kuipeleka Tanzania ICJ kwa kuwa  nchi yetu bado haijatoa tamko la kuikubali ICJ ingawa wao weshaikubali tangu mwaka 1969.
“Malawi haiwezi kutupeleka sisi ICJ mpaka tukae katika meza moja tukubaliane nao kuwa twende ICJ,” alisisitiza huku akisema wakifanya hivyo watarudishwa mpaka wakubaliane na Tanzania. Ila sisi tunaweza kuikubali ICJ hata leo na kwenda kuwashtaki Malawi,” alisisitiza.  
Akifafanua kuhusu barua hizo, alisema  ya kwanza ilikuwa ililalamika  juu ya boti Tanzania kupeleka  boti  katika ziwa hilo na kutaka  iondolewe.
Alisema barua ya pili ni  kutoka nchini humo inahusu  kitendo cha serikali ya Tanzania kuchapisha ramani mpya ambayo inaonesha mpaka wa  ziwa hilo kwa Tanzania kuwa upo katikati na kusema kuwa  kinaonekana kuwa ni cha kichochezi.
Waziri Membe alifafanua malalamiko hayo alisema boti hiyo ni timu ya utalii na  mifugo na uvuvi ambao wanafanya doria kama kawaida na wanasaka wavuvi haramu, hivyo madai hayo si ya kweli boti namna hiyo ipo pia katika ziwa Tanganyika na Viktoria kwa ajili ya kulinda usalama maeneo ya majini.
Aidha alisema lalamiko la pili kuhusu ramani mpya alisema  imechapishwa kwa ajili ya kuonesha mipaka ya mikoa minne na wilaya 19 ili viongozi wa maeneo husika watambue mipaka yao na imeonesha mpaka wa ziwa hilo baina ya Malawi na Tanzania uko katikati kama ilivyo katika mkataba wa Heligoland wa mwaka 1890 ,hivyo usingewezwa kuonesha uko kwenye fukwe kama wanavyodai Malawi.

No comments:

Post a Comment