WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, April 29, 2015

YANGA BINGWA 2015,YAINYUKA POLISI MORO 4-1



Simon Msuva (kushoto) akishangilia na Amis Tambwe baada ya Tabwe kuipatia timu yake bao la katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Yanga imeshida 4-1. (Picha na Francis Dande)
Mashabiki wa Yanga wakishangilia bao lililofungwa na Amis Tambwe.
Mshambuliaji Wa Yanga, Simon Msuva akimtoka beki wa Polisi Moro, Hassan Mganga katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Shabiki wa Yanga akifurahia bao la pili la timu yake.
Wachezaji wa Yanga wakishangilia baada ya kumalizika kwa mchezona Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 4-1.
Amis Tambwe akipokea mpira baada ya kufunga"Hat Trick"
Kocha wa Yanga, Hans Pluijm akishangilia baada ya timu yake kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara.
Mashabiki wakishangilia.(Muro)

source:mjengwa blog

Thursday, April 9, 2015

YANGA YAITANDIKA SOKA COASTAL UNION 8-0, TAMBWE APIGA ‘HAT TRICK’


Kiungo wa Yanga, Salum Telela, akimiliki mpira mbele ya
wachezaji wa Coastal Union ya Tanga katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Barauliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo. Yanga imeshinda 8-0.(Picha na Francis Dande).
Simon Msuva akishangilia bao aliloifungia timu yake.
Wachezaji wa Yanga wakishangilia.
Haruna Niyonzima akiruka kihunzi cha, Hamoud Abdulhalim.
Amis Tambwe akiwatoka wachezaji wa Coastal Union.
Mwamuzi wa mchezo kati ya Yanga na Coastal Union ya Tanga,
Simon Mbelwa, akimpa ‘tano’ mshambuliaji wa Yanga, Amis Tambwe, baada ya kuifungia
timu yake ‘hat trick’ na kukabidhiwa mpira katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka
Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jana. (Picha na
Francis Dande). 
Amis Tambwe akipongezwa na kocha wake.
Amis Tambwe akipongezwa na mashabiki wa Yanga.
Amis Tambwe akichuana na mchezaji wa Coastal Union, Mohamed Ally.
 
source:matukio na vijana

HITMA YA MAREHEMU MZEE KARUME YASOMWA LEO ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Vuai Ali Vuai maara alipowasili katika viwanja vya Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja kubhudhuria katika Hitma ya Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume Iliyofanyika leo asubuhi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein(katikati) akiwaongoza Viongozi mbali mbali pamoja na Wananchi katika Kisomo cha hitma ya aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja Iliyofanyika leo asubuhi.
Baadhi ya Viongozo wakisoma hitma akiwemo aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume(kushoto) Balozi Ali Karume katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja Iliyofanyika leo asubuhi.
Waislamu na wananchi mbali mbali wakiwa katika kisomo cha hitma ya aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja Iliyofanyika leo asubuhi.
Akinamama wa Mitaa mbali mbali ya Mji wa Unguja wakiwa katika kisomo cha Hitma ya aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja Iliyofanyika leo asubuhi.
Mke wa Rais Zanzibar Mama Mwanamwema Shein(katikati) akiwa na Mama Shadya Karume Mke wa Rais Mstaafu wa Zanzibar(wa tatu kulia) Mama Fatma Karume (wa pili kulia) Mke wa Makamo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano Mama Zakia Bilali (kushoto) Bi Khadija Aboud (wa pili kushoto)Mjumbe wa Kamati Kuu wa CCM,katika hitma ya kumuombea dua Rais wa kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume,iliyosomwa leo katika ukumbi wa Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein akiweka shada la mauwa katika kaburi la Marehemu Rais wa kwanza wa Zanzibar Mzee Abeid Amani Karume,baada ya kisomo cha hitma na dua iliyoombwa na wananchi wa Zanzibar katika Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar leo asubuhi.
Makamo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilali akiweka shada la mauwa katika kaburi la Marehemu Rais wa kwanza wa Zanzibar Mzee Abeid Amani Karume,baada ya kisomo cha hitma na dua iliyoombwa na wananchi wa Zanzibar katika Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar leo asubuhi.
Muasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Hamid Ameir akiweka shada la mauwa katika kaburi la Marehemu Rais wa kwanza wa Zanzibar Mzee Abeid Amani Karume, baada ya kisomo cha hitma na dua iliyoombwa na wananchi wa Zanzibar katika Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar leo asubuhi.
Balozi Ali Karume (Mtototo) kwa niaba ya familia akiweka shada la mauwa katika kaburi la Marehemu Rais wa kwanza wa Zanzibar Mzee Abeid Amani Karume,baada ya kisomo cha hitma na dua iliyoombwa na wananchi wa Zanzibar katika Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar leo asubuhi.
Wake wa Viongozi wakiitikia dua iliyoombwa katika kaburi la Marehemu MzeeAbeid Amani Karume baada ya hitma iliyosomwa leo katika ukumbi wa Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja na kuhudhuriwa na waislamu mbali mbali Mjni na Vijijini.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein pamoja na Viongizi wengine wakiitikia Dua iliyoombwa na Mufti Mkuu wa zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi (kulia) baada ya kisomo cha hitma iliyosomwa leo katika ukumbi wa Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja.
Baba Askofu wa Anglikan wa Kanisa la Mkunazini Michael Hafidh akiomba dua wakati Viongozi mbali mbali waliofika katika kaburi la aliyekua Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume,baada ya kisomo cha hitma iliyosomwa leo katika ukumbi wa Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja.(Picha na Ikulu, Zanzibar.)
 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein leo ameongoza hitma ya kumuombea dua Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu mzee Abeid Amani Karume, iliyofanyika Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui mjini Zanzibar.
 
Hitma hiyo, ilihudhuriwa na viongozi mbali mbali akiwemo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Mohammed Kharib Bilal, Rais mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Awamu ya Sita, Mhe. Amani Abeid Karume, Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd.
 
Viongozi wengine walihudhuria katika hitma hiyo ni  Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabhi, Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji, Sheikh wa Mkoa wa Dar-es- Salam Sheikh Mussa Salum na viongozi wengineo.
 
Wengine ni viongozi wa serikali zote mbili na viongozi wastaafu, viongozi wa vyama vya siasa, Masheikh kutoka Zanzibar na Tanzania Bara, Wabunge na Wawakilishi, wananchi kutoka sehemu mbali mbali pamoja na Mabalozi wadogo waliopo hapa Zanzibar.
 
Hitma hiyo ya kumuombea dua Marehemu Mzee Abeid Amani Karume pia ni miongoni mwa maadhimisho ya Siku ya Mashujaa ilitanguliwa na Qur-an tukufu, iliyosomwa na Ustadh Sharif Muhidin na kuongozwa na Sheikh Jafar kutoka Masjid Noor Mohammad,iliopo Kwa Mchina Mwanzo.
 
Mara baada ya hitma hiyo, Sheikh Mkoa wa Dar-es-Salaam, Sheikh Mussa Salum alitoa mawaidha na kumuelezea marehemu mzee Abeid Amani Karume kuwa ni kiongozi aliyepigania maendeleo ya wananchi wa Zanzibar na kumuombea MwenyeziMungu ampe makaazi mema Peponi.
 
Akieleza kuhuhu umuhimu wa siku hii, Sheikh Mussa alisema kuwa siku ya leo ni muhimu sana kwa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla kwa lengo la kumuombea dua Marehemu Karume pamoja na mashujaa wengine.
 
Aidha, Sheikh Mussa alitumia fursa hiyo kukumbusha juu ya umauti na kusisitiza kuwa ni  jambo ambalo litafika kwa kila kiumbe alichokiumba MwenyeziMungu na kusisitiza kuwa ni vizuri mwanaadamu akakumbuka asili yake na hatma yake.
 
“Kifo ni onyo, kifo ni mawaidha na kifo ni mazingatio...kutokana na hali hiyo kuna kila sababu ya kutenda mema, kuwa na mahaba, kuwa na udugu wa kiimani.. huku tukiendelea kumuombea dua mzee wetu huyu kwani yeye ameonja umauti kama ilivyoeleza Qur-an ikiwa na maana kuwa roho yake bado iko hai” alisema Sheikh Mussa.
 
Pamoja na hayo, Sheikh Mussa katika kutilia mkazo suala zima la udugu wa kiimani alitoa pongezi kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein kwa kuendelea kusimamia Serikali ya Mapindui ya Zanzibar yenye muundo wa Umoja wa Kitaifa ambayo imewafanya Wazanzibari kuimarisha udugu wao na kuwa kitu kimoja kama Uislamu unavyotaka.
 
Alisema kuwa hatua hiyo imezidisha umoja sambamba na kuimarisha amani na utulivu uliopo na kuifanya Zanzibar kuwa tulivu na kusisitiza kuwa huo ndio udugu wa kiimani.
 
Baada ya kisomo hicho cha hitma ambacho hufanyika kila mwaka inapofika tarehe 7, Aprili, viongozi hao na wananchi waliohudhuria katika hitma hiyo walimuombea dua, marehemu mzee Abeid Karume katika kaburi lake lililopo pembezoni mwa afisi hiyo ya CCM Kisiwandui dua iliyoongozwa na viongozi wa dini tofauti akiwemo Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Omar Kabhi, Askofu Michael Hafidh kutoka Kanisa la Anglikana Zanzibar na Bhaguan Suria (Mshamba) aliyesoma kwa niaba ya Wahindu.
 
Viongozi na wanafamilia waliweka mashada ya maua katika kaburi la marehemu mzee Abeid Amani Karume akiwemo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Mohammed Kharib Bilal, Mzee Hamid Ameir aliyeweka shada la maua akiwakilisha wazee walioshiriki Mapinduzi ya Januari 12, 1964.
 
Mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Luteni Jeneral S.A. Ndomba, Balozi Ali Karume aliyewakilisha familia ya Marehemu Sheikh Abeid Amani Karume na Balozi mdogo wa China anayefanya kazi zake hapa Zanzibar Mhe. Xie Yualing aliyewawakilisha Mabalozi wenzake wa hapa nchini.
 
Aidha, Mama Mwanamwema Shein aliungana na akina mama wengine katika hitma hiyo katika Afisi hiyo ya CCM Kisiwandui, akiwemo mjane wa marehemu mzee Abeid Karume, Mama Fatma Karume, Mama Asha Bilali,Mama Zakia Bilal, Mama Asha Balozi na Mama Pili Balozi, Mama Shadya Karume na viongozi wengine wanawake wa kitaifa wakiwemo Mawaziri, Wabunge, Wawakilishini na wananchi kutoka sehemu mbali mbali ya Zanzibar na Tanzania Bara.
 
April 7, 1972 ndiyo siku aliyouawa Rais wa Kwanza wa Zanzibar marehemu Mzee Abeid Amani Karume na wapinga maendeleo nchini ambapo hivi leo imetimia miaka 43 tokea utokee msiba huo.
 
(Picha / Habari: Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar)

Monday, April 6, 2015

UJUMBE WA PASAKA 2015: AMANI YETU ITALINDWAJE TUNAVYOELEKEA KATIKA UCHAGUZI WA TAIFA LETU 2015?




"Sauti ya mtu imesikika jangwani: `Mtayarishieni Bwana njia yake; nyosheni mapito yake.  Kila bonde litafukiwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa; palipopindika patanyooshwa, njia mbaya zitatengenezwa.  Na, watu wote watauona wokovu utokao kwa Mungu."`

 "Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mngeweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?  Basi, onyesheni kwa matendo kwamba mmetubu”.

Umati wa watu ukamwuliza, “Tufanye nini basi? Akawajibu, Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo. Nao watoza ushuru wakaja pia ili wabatizwe, wakamwuliza, Mwalimu, tufanye nini?  Naye akawaambia, Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa.  Nao askari wakamwuliza, "Na sisi tufanye nini?  Naye akawajibu, Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu."

Leo tunavyosherekea siku hii ya Pasaka ujumbe mzito kwa viongozi wa serikali, vyama vya siasa na viongozi wa dini tudumishieni amani yetu; na hii itawezekana kwa kutekeleza kauli ya Yohana Mbatizaji  Toshekeni na masilahi” na kwa viongozi wa dini “Hubirini ukweli na muwe wa kweli; hivi vikitekelezwa vitalijengeeni Taifa letu Amani ya kweli”:

Neno  hili ni zito japo lilizungumzwa kipindi kirefu nyuma lakini tunaendelea kulishuhudia leo tunapowaangalia watendaji wetu katika serikali zetu, ndani ya vyama vya siasa na sasa hata miongoni mwa viongozi wa dini ambao nao wameanza kupenyeza masilahi yao binafsi, na kuanza kuzoofisha amani ya Taifa letu.

Neno hili linatufundisha uadilifu, uwajibikaji kulingana na maadali  na kanuni za kazi ambazo zinatulazimu sisi kama watendaji wa Taifa kuweka mbele matakwa ya Taifa na sio masihahi binafsi;

Najiuliza tena  leo hii hata viongozi wa dini mbona wamekuwa mbele katika kutanguliza masilahi binafsi mbele kuliko mwongozo wa Vitabu vikatifu kwa katika kujenga amani; Je wanafanya hivyo kwa kivuli cha nani? Na  hili linamaana gani kwa taifa letu? 

wananchi wa Taifa hili wanahitajii uhuru wa kiuchumi ambao unatokana na viongozi wetu watangulize mbele masilahi ya Taifa, warizike kidogo wananchokipata; kinyume chake kama hawatarizika na hicho kidogo hawataweza  kuweka mbele masilahi ya taifa na bali watatanguliza mbele vitendo vya  rushwa na ufisadi ambao unarudisha maendeleo ya Taifa nyuma sana na kudhoofisha amani yetu.

Ujumbe wa  Pasaka ya mwaka 2015  itukumbushe sisi  Kama Taifa na kama Raia na watendaji ambao tumekula kiapo cha utii na maadili bora ya uwajibikaji kwa Taifa letu kuwapa wananchi wanyonge zawadi kubwa ya  uhuru  wa kiuchumi,  ili kila mmoja wetu aweze kuyafurahia  zawadi pekee ya rasilimali  ambayo Mungu amelijalia Taifa letu. Hakuna atayepingana nami kuwa  nchi yetu imefurika kwa  asali na maziwa tatizo ni wachache tu ambao wanafaidi kwa kutoridhika na mishahara yao. 

kwa kipindi kirefu tumeona kuwa nchi yetu  Tanzania iliyokuwa ikifurika neema  ya rasilimali sasa imegeuka; kuwa nchi inayofurika machungu; matendo yaleyale ya kifisadi, ya ukandamizaji, ya unyanyasaji ambao  Farao aliwatendea wana wa Israeli huko misri miaka hiyo; lakini kwa kuangalia falsafa hiyo ya matendo ya Farao ndio tunaishuhudia sasa namna watendaji wetu walikokabidhiwa dhamana ndani ya Taifa letu  ambao sio waadilifu wananyo haribu nchi, na kuacha machingu kwa wananchi ambao bado wako kwenye dimbwi la umasikini.

je viongozi wetu wa dini leo hii wanahubiri amani ambayo Yohane Mbatizaji aliifafafanua kulingana na makundi yaliyokusanyika?
Je viongozi wa dini wanahubiri amani au wanaendeleza chuki moingoni mwa wananchi wa Taifa letu?

Kulingana na Yohane matajiri wanaotakiwa kuangalia haki ya maskini, "Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo."(Lk 3,11), kwa watoza ushuru waepuke rushwa na matendo ya kifisadi "Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa."(Lk 3,13) na kwa maaskari wazingatie haki "Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu."(Lk 3,14).

Leo hii ndani ya Taifa vitendo hivi vimeshamiri tena kwa kiasi kikubwa; na pengine kila mmoja ameshiriki kwa namna moja au nyingine katika uovu huu. Hii inaweza kuwa moja kwa moja au kwa kutokuwajibika ipasavyo katika eneo lake la kazi na hivyo kusababisha mianya katika kukua kwa matendo haya maovu. Wito wakati tunasherekea Pasaka 2015 sisi kama Taifa inatupasa tubadilike na kuhakikisha haki na upendo vinashamiri katika jamii yetu.

Kama tutafanikiwa kuishi kwa ujumbe huu wa Yohani Mbatizaji kuwa tutosheke ni mishahara yetu mimi naamini kuwa tukiweka mbele maslahi ya nchi, nchi itasonga mbele. TUKUMBUKE KAULI YA YOHANA MBATIZAJI KWA WALE ASKARI kuhusu dhuluma:
TOSHEKENI NA MISHAHARA YENU, watu wana madaraka makubwa mishahara mikubwa na masurufu manono lakini bado wanaiibia nchi. Kwa nini lakini? Hii choyo ulafi kwa nini?

Nafikiri Tatizo la wanasiasa na Viongozi wa dini wakishafanikiwa kujikwamua kimasilahi wanasahau kuwa wananchi bado ni masikini na wanahitaji masaada ili nao waweze kufarahia zawadi ya maisha ambayo wamezawadiwa na Mwenyezi Mungu.

Amani kwao sio wimbo ulio bora tena kwao, maisha bora ya wananchi wao inabaki katika slogan tu.

Wanatumia muda mwingi kutukanana na kuonyeshana ufahari wao, ambao wamepata kwa kuendelea kuwakamua hawa wanachi masikini.

Je watendaji wetu wako tayari kutoa hesabu za utendaji wao siku watakapotakiwa na Mwenyezi Mungu tukiamini kuwa kazi zote hutoka kwa Mungu?

Nafiki Pasaka hii kujifunze kitu kingine kipya kuwa “Jihadharini na tabia ya kupenda fedha, na “toshekeni na mlivyonavyo” kwa sababu Mungu mwenyewe alisema,

“Kwa vyo vyote sitakupungukia kabisa, wala sitakutelekeza na kukuacha bila msaada. Kamwe, kamwe, sitakuacha hata kwa kiwango kidogo, kukuacha bila msaada, au kukuacha, au kukuangusha, au kulegeza mkono wangu kwako. Hakika sitafanya hivyo! Kwahiyo tunafarijika na kutiwa moyo, na kwa uhakika na ujasiri twathubutu kusema, ‘Bwana ndiye anisaidiaye” (Ebr 13:5, 6)

Kwa kutosheka na mishahara yetu na kwa kuamini kuwa sisi ni wachache ambao tumechaguliwa na Mwenyezi Mungu kuwa saidia wengine ili waweze kupata ridhiki zao; au kufurahia asali na maziwa kwa vipaji vyetu kwa kutimiza wajibu wetu tutakuwa tunatekeleza ujumbe huu wa “Utafuteni kwanza ufalme wa Mungu na haki yake na hivi vitu vingine vyote mtapewa kwa maelefu.

Tukitenda kila kitu kwa haki kamwe hatutakosa chochote unachohitaji kitakuwa ziada. Mwenyezi Mungu atakupa namna ya kupata kila uchokihitaji zaidi.

Imani yangu ni kama ile ya Paulo kama tutatosheka ni mishahara yetu,na kuwajali wanyonge katika Kupata Riziki
zao, “Na Mungu wangu atawajazeni na kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu wake …”. Lakini hili litawezekana kama viongozi wetu wa serikali, vyama vya siasa na wale wa dini watafanya kazi zao kulingana na na viapo vya kazi zao.

"Mungu hatakosa KUWAONGEZEA wale wote wanaoifanya kazi yake sawasawa na mapenzi yake" huu ndio ujumbe wa Pasaka 2015