WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, August 29, 2016

RAIS DK MAGUFULI AHUDHURIA MISA YA JUBILEI YA DHAHABU (MIAKA 50) YA NDOA YA RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA NA ANNA MKAPA


Rais Mstaafu Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa
wakionyesha cheti chao cha Jubilei ya dhahabu ya
miaka 50 ya ndoa yao
Dar es Salaam
Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin William Mkapa Agosti 27, 2016 ameadhimisha Jubilei ya Dhahabu ya Miaka 50 ya ndoa yake na Mama Anna Mkapa katika Kanisa la Mtakatifu Petro, lililopo Oysterbay Jijini Dar es Salaam.

Misa ya Jubilei hiyo imefanyika nyakati za mchana katika ukumbi wa Kardinali Rugambwa, kando ya kanisa la Mtakatifu Petro-Oysterbay ikitanguliwa na Misa ya shukrani iliyofanyika katika Kanisa hilo asubuhi.

Jubilei hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Rais Dk. John Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli, Makamu wa Rais  Samia Suluhu Hassan, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dk. Jakaya Kikwete, Rais Mstaafu wa Awamu ya Sita wa Zanzibar Dk. Amani Abeid Karume, Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere, Mawaziri Wakuu Wastaafu Cleopa Msuya, Dk. Salim Ahmed Salim, Jaji Joseph Warioba na Edward Lowassa.

Misa Takatifu ya Shukrani imeongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Arusha Mhashamu Askofu Josephat Lebulu na kuhudhuriwa na Maaskofu na Maaskofu Wakuu saba akiwemo Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.

Akizungumza mwishoni Misa Takatifu, Rais Magufuli amempongeza Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa kwa kutimiza miaka 50 ya ndoa na ameeleza kuwa ndoa hiyo iliyowaunganisha wanandoa wanaotoka katika madhehebu tofauti ya Kikristo imetoa fundisho kubwa kuwa binadamu wanapaswa kuwa wamoja hata kama wana tofauti mbalimbali zikiwemo za kimadhehebu ya dini, siasa na kanda.

Rais Magufuli amesema miaka 50 ya ndoa ya Mkapa ambaye ni Muumini wa Kanisa Katoliki na Mkewe Mama Anna Mkapa ambaye ni Muumini wa Kanisa la Kilutheri inawafundisha watanzania wote hususani wanasiasa kuishi kwa upendo na kuilinda amani waliyonayo na ametoa wito kwa viongozi dini kuendeleza juhudi zao za kuliombea taifa na kuwaunganisha wananchi licha ya tofauti walizo nazo.

Kwa upande wake Rais Mstaafu, Mkapa pamoja na kuwashukuru Viongozi wote, ndugu, jamaa na marafiki waliohudhuria Misa ya Shukrani na Jubilei hiyo ya miaka 50 ya ndoa yake amemshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuijaalia ndoa yake umri mrefu.

Rais Mstaafu Mkapa pia ametoa mwito kwa watanzania kupenda na kushirikiana huku akibainisha mafunzo aliyoyapata kutoka kwa viongozi wa dini kuwa "Kila mmoja ni zawadi kwa mwenzake"

Nae Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amempongeza Rais Mstaafu Mkapa na Mkewe Mama Anna Mkapa kwa kuadhimisha miaka 50 ya ndoa na amewasihi watanzania kuiga mfano mwema uliooneshwa na wana ndoa hao ambao wamedumu katika imani bila kuyumba.

Kardinali Pengo amesema ndoa ya Rais Mstaafu Mkapa anaifundisha jamii kuwa tunaweza kuishi kwa imani zetu bila kubadili dini

 Rais Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Petro  Fr. Stephano Kaombwe wakati akiwasili kuhudhuria  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa ya Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
Rais Dk. John Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa, wakati akiwasili kuhudhuria  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa ya Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016. Lowassa alikuwa mshindani wake mkubwa katika kinyang'anyiro cha Urais katika uchaguzi mkuu uliopita mwaka 2015, ambapo Lowassa aligombea kupitia Chadema.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisalimiana na Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa, wakati akiwasili kuhudhuria  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa ya Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 "Maharusi"  Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa wakiingia kanisani  tayari kwa  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa yao katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa  wakiwa tayari kwa  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa yao katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016  
 Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Petro  Fr. Stephano Kaombwe akiongoza Ibada ya ukumbusho wa ahadi za ndoa wakati wa Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa ya Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Petro  Fr. Stephano Kaombwe akiongoza Ibada ya ukumbusho wa ahadi za ndoa wakati wa Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa ya Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa akimvisha pete Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa akivishwa pete na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
 Rais Dkt John Pombe Magufuli akimtakia amani Mama Anna Mkapa
Mama Janeth Magufuli na Mama Maria Nyerere wakiwatakia amani Mzee Mkapa na Mama Anna Mkapa
 Rais Dkt John Pombe Magufuli akimtakia amani Mhe. Edward Lowassa
 Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa wakipokea hati malumu ya ndoa kutoka Vatican kwa Baba Mtakatifu Papa Francis kutoka kwa Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo
 Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa wakipongezwa na Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo. PICHA ZAIDI>>BOFYA HAPA

Tuesday, June 21, 2016

RAISI DR. MAGUFULI NA JICHO JIPYA LA WATENDAJI KATIKA SERIKALI;



Serikali ya awamu ya tano kwa mara ya kwanza imeamua kuwatumia sana wataalamu ambao wana sifa za kielimu katika utendaji wa wake katika idara nyingi serikalini; mwelekeo ambao umekuwa wazi inajitahidi sana kuondoka na kasumba ya kuwapa watu vyeo kwa huluka ya kisiasa kwa kulindana na kurudisha fadhila. Ilikuwa jambo la kawaida hata wasomi wetu kwa sababu ya hulka ya kisiasa hata pale walipokuwa wakipata nafasi za uongozi walikuwa wanazisahau kabisa taalumu zao na kufanya kazi kwa mazoea ya siasa.

kuwa mwana siasa kwa ujumla wake sio  taaluma, ni haki ya kila mtanzania (msomi au sio) lakini lazima tofauti moja iwe bayana kuwa msomi anapongia katika siasa anaangaliwa katika jicho tofauti kwa mategemeo na matarajio kuwa anatafanya kazi kwa weledi mkubwa na kuongeza tija kwa taifa; Kitu ambacho kwa kipindi kirefu kilikuwa sio kweli. Ilikuwa ni aibu na hasara ambayo Tanzania imekuwa ikipata kwa wasomi wake kujiingiza katika siasa ambazo mchango wake kwa maendeleo ya taifa ulikuwa ni mdogo kuliko angejikita katika kufanya utafiti unaohusiana na fani yake.
Kwa wasomi wetu kuingia katika siasa ilikuwa ni mwanzo wa kuzika taaluma zao; hata pale ambapo walitakiwa kutoa ushauri ambao ungekuwa na manufaa makunwa kwa taifa, hata kama ushauri huo ungekuwa mchungu kwa serikali mara nyingi walikuwa wakitoa ushauri wenye masilahi kwa mtu au chama. Hivyo kuwa hasara kwa Taifa. Kwa wakati huo ilikuwa vyema kwa  Siasa kuwaachie wanasiasa.

Mara nyingi tumechambua kuwa siasa ni mchezo mchafu; lakini ukweli ni kuwa siasa kama mfumo hauna tatizo lolote, wenye tatizo ni wachezaji wanasiasa ambao moja ya sifa yo kubwa ni uwezo wa kuongea na kubadilisha maneno ili sio kuwasaidia wananchi ili kujinufaisha kupitia chama Fulani na uundwaji wa serikali yao; hivyo hata wasomi wetu kama raia wa Tanzania hakuna tatizo kama hao wasomi wanajiingiza kwenye siasa. Shida ni pale wanapokuwa wanasiasa waongo na wasioaminika.

Inatakiwa tufike mahali kama ilivyo kwenye nchi za mataifa yaliyoendelea kuwa utagundua wanasiasa ni wanasiasa na wataalamu huwa hawajichanganyi kwani muda wote wako wakiumiza vichwa kufikiria jinsi ya kugundua kitu fulani. Linapokuja tatizo katika jamii huwa wana wanajitahidi kutimiza wajibu wao kwa kutumia utaalamu wao katika kuleta suluhu ya tatizo.

Tunamshukuru Dr. Magufuli kwa kuanza kutaka kupata matokeo chanya kutoka kwa wasomi wetu katika awamu hii wamepewa mafasi kubwa ili weweze sasa kufanya kazi kwa utaalamu na sifa ambazo wanazo kwa faida ya Taifa na kuwaondolea wananchi wa kawaida ugumu wa maisha ambo uko mbele yao; ni kweli ilikuwa jambo la  aibu sana kuona hadi hii leo Serikali imeshindwa kutumia wasomi wake na rasilimali zilizopo kuleta ufanisi katika kuleta maendeleo kwa wananchi wake matokeo yake ni usanii wa kisiasa ndio uliowekwa mbele. Lakini kubwa zaidi ni kuona hata pale inapopatikana fursa ya ukombozi kujikwamua katika ujinga na umaskini wa kujitakia,hutokea Wasomi wetu kutusambaratisha wenyewe kwa wenyewe.

Wasomi wetu awamu hii ni kipindi chenu cha kuumiza na kushauri na kubuni mipango ya kuwafanya Watanzania katika kuleta mageuzi makubwa ya uchumi na maisha ya watu wake; Dr. Magufuli  anategemea sana ushauri na misimamo madhubuti ya wasomi ili kuisadia serikali katika kujenga Tanzania Mpya. Katika siku za nyuma ilikuwa sahihi kusema kuwa  wananchi wa nchi hii walikuwa na  shahada ambazo zilikuwa hazitumiki zilikuwa zimefungiwa kwani nafasi zao zilichukuliwa na wanasiasa ambao walikuwa hawana sifa za utendaji kwa Taalumu bali kwa siasa; Tumeona mifano ya Maprofesa wengi wasio na idadi, wengi amboa walikuwa wamekijikita kwenye siasa hivyo taaluma yao ilikuwa haina nafasi ili walazimu kucheza ngoma ya siasa na sio ngoma ya utaalamu wao katika kutoa ushauri au kutekeleza adhima ambayo ilikuwa mbele yao.

Katika mazingira yetu, tunapozungumzia Siasa, watendaji wote walilazimika kuwa chini ya mwamvuli wa maagizo ya chama na serikali yake na si vinginevyo hivyo walitakiwa kukizi zaidi zaidi matakwa na mahitaji ya watawala kuliko matakwa na mahitaji ya jamii. Ni jambo la kawaida kwa vyama vya siasa kutumia muda mchache sana kujishughulisha na matatizo/changamoto zinazokabili jamii na badala yake kujikita katika masuala yanayohusiana na uongozi na kutwaa madaraka. Lakini Mheshimiwa Dr. Magufuli anataka wasomi wetu ndio sana wawe chachu ya utawala Bora; wawe ni chimbuko la ufanisi na utatuzi wa Migogoro; wawe ndio daraja bora la maendeleo kwa taifa kwa kutumia uwezo wao wa  kuchanganua, kutambua, na kuelewa jambo. Na na ndio maana wasomi  katika jamii yoyote ile wana uwezo mkubwa wa kuona masuala mbali mbali zaidi ya mwanasiasa wa kawaida kwa  maslahi mapana ya kitaifa.

Tofauti na miaka ya nyuma, Tanzania ya leo imejaliwa kuwa na wasomi wengi sana waliotokana na vyuo vyetu vikuu. Vyuo vikuu ni taasisi zenye umuhimu wa kipekee wa kupangilia na kuendeleza kitu amhacho jamii inaweza kuakisi. Lakini kwa vile wasomi wana nafasi na uwezo wa kushughulika na masuala mbalimbali ya kijamii hawa ndio wenye jukumu kubwa la kuisaidia jamii yetu iondokane na umaskini ambao kwa mshangao mkubwa na bila aibu

kama kioo cha jamii – kwa maana ya kwamba inaipa jamii taswira yake. Wasomi wa nyanja mbali mbali wana uwezo na wajibu wa kutuelezea watanzania tunaonekana vipi kama jamii. Wasomi wana uwezo na wajibu pia kutupa tahadhari juu ya hatari iliyopo mbele yetu; na vile vile kutusaidia kutupatia maana ya vitu ambavyo wanasiasa wetu aidha wanavipotosha, hawavielewi au wanafanyia mzaa kwa faida zao binafsi. Na kwa mara nyingine nina imani kuwa katika awamu hii ile dhana iliyojengeka na jamii yetu ya kuamini wanasiasa na kuliko wasomi ina weza sasa ikapata tafsiri tofauti. 

Lakini ni wajibu wa wasomi wetu kuidhihirishia jamii kuwa wao ndio watatuzi wa kero zetu na sio wansiasa ambao walio wengi hawana taaluma inayotakiwa katika kupambana na kero tofauti tofauti.

Tukumbuke wakati wa Mwalimu alivyoweza kuwatumia wasomi wetu kwani miaka ya 1960s – 1970s, kila wakati taifa lilipokuwa linakabiliwa na changamoto mbalimbali, Mwalimu alikuwa na utamaduni wa kwenda Chuo Kikuu (Mlimani) kukutana na kujadiliana na wanafunzi. Ndio maana tofauti na leo, ilikuwa ni mara chache sana kwa serikali ya Mwalimu kukwaruzana na wasomi. Ni muhimu kwa wasomi kuendeleza juhudi za aina hii.Lengo kubwa Raisi Dr. Magufuli ni kujenge upya dhana ya utendaji kazi yenye nidhamu, uwajibikaji na weledi kwa Taifa na kuondoa utendaji kazi wa mazoea. Sasa ni wakti umefika kwa wasomi wetu ambao mmepewa dhamana ya kuongoza vitengo mbali mbali kulingana na taaluma zetu kufanya kazi katika msingi huo wa utendaji ambao utakuwa na tija kwa taifa letuna faida ya wananchi wetu na mageuzi ya kweli ya uchumi wa Taifa letu;
Mungu Ibariki Tanzania: 

Mungu Mbariki Raisi wetu na dhamira yake nzuri ambayo ameanza kuionyesha kwa Taifa.

Amina

Tuesday, April 5, 2016

SERIKALI ZENYE RUSHWA NA UFISADI – KIINI CHAKE NI NINI?



Wafilipi 2: 4


Leo tujitafakari  na tujiulize kuwa je kuna serikali yeyote ya kidunia ambayo inaweza kuwa madarakani bila kuwa na kutumikia rushwa na ufisadi? Tukumbuke kuwa mwisho wa siku watumishi wa serikali bado ni raia wa nchi husika na zao la taifa husika; Je kwa mantiki hii viongozi ambao wanaunda serikali wanaweza kuepukana na vitendo vya rushwa na ufisadi? Je unakubaliana nami kuwa serikali za kidunia zimejaa rushwa na ufisadi ambao ni ubatili mtupu? Je tunaweza kuwa na serikali ambayo haina tabia hizi katika dunia hii? Bibilia inatukumbusha kuwa  serikali ambayo haitakuwa na harufu ya rushwa lazima itoke nje ya serilaki za kibinadamu;

Tafakari ya leo inatukumbusha kuwa serikali za kidunia ambazo hatimaye zinatawaliwa kwa rushwa na ufisadi, zinasaidiwa kuingia madarakani na raia ambao wanakuwa na malengo tofauti kwa masilahi yao binafsi; wengine wakijua wazi kuwa endapo serikali hiyo itaingia madarakani basi haja zao za kukwepa ushuru, au kuendesha biashara yao bila kufuata masilahi mapana ya nchi yatafanikiwa; hivyo na serikali itatengeneza mianya ya wao kuendelea kujinufaisha na kuwaacha wananchi wanyonge masikini katika umasikini wao kwani nguvu nyingi zitaelekezwa kwao. Tumeona sehemu kubwa za tawala hizi watu ambao ni waaminifu ndio wanaoumia zaidi.

Tafakari ya leo inatukumbusha kuwa ili tuweze kuangamiza rushwa na ufisadi lazima nguvu za kutokomeza zianzie kwa viongozi wa juu ambao wamepewa mamlaka juu ya nchi na Mwenyezi Mungu. Serikali yeyote ile ambayo itakuwa tayari kupambana na rushwa na ufisadi ujue kuwa itapoteza umaarufu wake; katika hili bibilia tukisoma Mhuburi 7:20 bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani, ambaye afanya mema, asifanye dhambi.

Tafakari yetu bado inatuongoza kuwa  tukiondoa wanadamu ambao sio wakamilifu; Yesu Kristo ambaye Mungu alimchagua kutawala ufalme wake, hakuweza kushawishika katika yale ambayo yalikuwa sio sahihi kutenda;  Yesu alionyesha hili pale alipokataa rushwa  kubwa ambazo alipewa na shetani juu ya kukabidhiwa utawala wote wa kinunia na fahari zake kwa kuambiwa kumsujudia shetani Mathayo 4: 8-10  kisha ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha miliki zote za ulimwengu na fahari yake; akamwambia haya yote nitakupa , ukianguka kunisujudia; Ndipo Yesu akamwambia Nenda zako shetani, kwa maana uimeandikwa msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake. Katika shida na mateso yote bado Yesu aliendelea kudumisha msimamo wake ulio sahihi wa kumtumikia Mungu bila kushawishiwa na mtu mwingine yeyote kwa ukombozi wetu sisi.

Ni ukweli mtupu kuwa nchi nyingi zinafanya uchaguzi ambao nadharia inaruhusu watu kuwachagua viongozi ambao wataingia ofisini/madarakani kwa ajili ya kuendesha nchi; lakini ukiangalia chaguzi nyingi na taratibu za chaguzi hizo hizo ambazo tunaona kampeni zake  nanatawaliwa kwa rushwa kwa kiasi kikubwa sana, hivyo wale wenye uwezo ndio wanaowaingiza watawala madarakani; hapa nafikiri utakubaliana na mimi vyama vya siasa ndivyo vinavyoongoza kwa matendo makubwa sana ya rushwa katika kuhakisha kuwa viongozi tukona vyama vyao ndio wanakuwa washindi ili waweze kuongoza serikali, hivyo watafanya kila hila ili waweze kushinda.

Tafakari yetu ya leo inawaasa viongozi wetu kuwa ili kuweza kuepukana na tabia zote za rushwa na kifisadi; lazima watekeleze amri kuu ya upendo ambayo ni amri ya dhahabu; kile ambacho wewe unataka ufanyiwe mfanyie mwenzako hivyo hivyo; Mathayo 7:12 Basi yo yote myatakayo mtendewe na watu; nanyi watendeeni vivyo hivyo; maana hiyo ndiyo torati na manabii. Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii Mpende jirani yako kama nafsi yako. Hili kwa viongozi wetu wengi ambao ndio tegemeo la kuondoa umasikini wa watu wao wameshindwa kutekeleza hili; wao wanapenda kutendewa vizuri na kundi dogo la watu waliowaingiza madarakani na kunufaishana wao kwa wao; wameshindwa kabisa kutekeleza hii Golden Rule.

Kwa msingi huu rushwa na ufisadi unaimarishwa zaidi na choyo ya mali na ubinafsi wa kujililbikizia mali; hapa tunaona kuwa viongozi wako tayari kupokea rushwa mfano kutoka kwa makandarasi, nao makandarasi wanapata nafasi ya mwanya wa rushwa katika kutumia vifaa ambavyo havina ubora unaotakiwa ili waweze kujilipa na kupata faida kubwa; kwa msingi huu rushwa na ufisadi utaweza tu kwisha kama tutaondoka na dhana ya ubinafsi na choyo ya kujitajirisha; kama Waefeso 4:23 inavyotufundisha na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu: tunatakiwa kuvua uongo na tunatakiwa kusema kweli daima ili tuweze kuvaa utu mpya ulioumbwa katika mungu ili kutekeleza wajibu wetu ipasavyo na kuwa na hofu ya Mungu. Na ujumbe huu kutoka katika waraka wa Paulo kwa Wafilipi 2:4  ni muhimu sana ambapo anatufundishwa kuwa Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe bali kila mtu aangalie mambo yaw engine.

Tatizo la tawala za kiduani hata kama wakati mwinginwe wanaweza patiwa elimu nzuri ya kupambana na rushwa na ufisadi bado viongozi wetu wanapenda kushiriki katika vitendo vya rushwa. Kwa msingi huu ni vigumu kwa serikali zetu kupambana na rushwa; tukumbuke mafundisho ya bibilia kuwa watu wenye uchu wa mali, na waongo hawataingia mbinguni; mara nyingi viongozi wala rushwa wana hizi tabia mbili ya Uchoyo wa mali na uongo wanapowadanganya watu wake ili kuhalalisha uovu wao na kikundi kidogo kilicho waingiza madarakani kwa masilahi yao;

Hii ndio tafakari yetu ya leo Amina

Emmanuel Turuka
Corrupt Government


.


Wednesday, March 9, 2016

MIEZI MINNE YA DR. JOHN POMBE MAGUFULI NA TANZANIA MPYA:-

 

JE FALSAFA YA MHESHIMIWA MAGUFULI YA HAPA NI KAZI TU NI SAWA NA  SEMI HIZI?

Kumpa mtu samaki utakuwa umemlisha katika siku ya leo; ukiweza  Kumfundisha mtu  namna ya kuvua samaki  utakuwa umeweza kumsaidia kumlisha katika maisha yake yote.

Ukiweza kumfundisha mtu namna ya kutengeneza na kusafirisha na kuweza kuuza samaki katika masoko ya nje; utakuwa umefanikiwa kuchochea maendeleo ya kiuchumi

Raisi Magufuli toka aliposhika nafasi ya kuliongoza Taifa la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ameendelea kuwa gumzo la utendaji uliotukuka hasa akipigania maendeleo ya wananchi Masikini. Amekuwa na maono ya  uzalendo wake kwa kujitoa kwa kusimamia vizuri rasilimalia za taifa letu. Ameweza kuonyesha umahili katika kusimamia nidhamu ya utendaji katika Wizara na idara zote za serikali, huku akibana matumizi ili kuelekeza nguvu zaidi katika miradi ya maendeleo ambayo inawagusa wananchi moja kwa moja.

Raisi magufuli katika kipindi hiki kifupi amweza kujijengea sifa ya kuwa "unforgettable" miongoni mwa viongozi wa juu wa Tanzania na amekuwa kipenzi cha wanyonge ambao wanamwona kama mkombozi wao katika shida na umasikini wao. Mfano maauzi yake ya haraka ya kuwanusuru wagonjwa waliokuwa wanalala chini katika hospitali zetu; vitendo kama hivyo wananchi wananwmona Dr. Magufuli kama Kiongozi mwenye  maono ya   maendeleo ya nchi yake:

Katika kipindi hiki kifupi ameweza kusimamia ukusanyaji wa mapato ya serikali ambayo yameongezeka sana na kusaidia katika kupunguza utengemezi hasa katika bajeti ya maendeleo ambayo tulikuwa tunategemea sana ufadhili na kukwamisha shughuli za msingi za maendeleo ya Taifa letu. Amekuwa kiongozi ambaye ameonyesha uwezo wa Kujenga na kuboresha uchumi, wetu katika siku zijazo mbele; Ameweza pia kukuza mifumo ya kiutawala na sera zinazolenga zaidi katika kusimamia maisha na ukuaji wa uchumi wa nchi ili tuweze kuondokana na tatizo kubwa la umasikini wa Taifa letu.

Nimejaribu kueleza hayo yote ili kuonyesha kuwa bila kuwa na uongozi wenye maono usiotafuta faida yake wenyewe, usiokuwa tayari kuwawajibisha watendaji wabovu na wanaokiuka maadili na uvunja sheria  hatuwezi kutoka hapa tulipo, tutaendelea kufurahia kauli mbiu ambazo hazina maana wala msingi mkubwa kwa maendeleo ya Taifa.

Kwa sasa Taifa linamwitaji kiongozi mwadilifu, mkweli ambaye anaweza kupambana na matatizo ya rushwa na ufisadi bila kuyaonea aibu. Ili kulivusha Taifa la Tanzania katika mabadiliko ya maendeleo ambayo kama taifa tunayahitaji kwa sasa; tunahitaji Kiongozi ambaye anauchungu sana na nchi yake hasa katika kuwasaidia wananchi ambao ni wanyonge ambao wanahitaji mkate wao wa kila siku na watoto wao waweze kwenda shule; Tumeliona hili kwa Raisi wetu Dr. Magufuli amekuwa msimamizi wa khali ya juu wa utekelezaji wa mpango wa mabadiliko ambayo kama taifa tunayahitaji kwa sasa; katika kampeni alituhahidi kuwa  hana mchezo hata kidogo katika hili  na hatakuwa na msamaha kwa wale wote ambao hawatafikia malengo ambayo serikali yake imeainisha kutekeleza.

Ameshatoa onyo kwa viongozi na wafanyakazi kuwa hayuko tayari kuona kuwa rasilimali ya taifa zinachezewa na wajanja wachache, ikibainika serikali yake itawafukuza kazi bila huruma;  Kwa Dr, Magufuli  ufanisi utakuwa unapimwa kwa uwajibikaji na uadilifu na sio propaganda za kisiasa.

Mheshimiwa Magufuli amepania kurudisha kwenye kamusi maneno uwajibikaji na uwajibishaji kwa watendaji wa serikali katika taasisi zake na idara zake,  na ameamua kuondoa kabisa kwenye kamusi maneno kama utashi wa kisiasa urafiki na undugu na michakato katika kutekeleza wajibu katika majukumu yako ya kikazi.

Mheshimiwa Magufuli anaamini kuwa  hakuna maendeleo ya kweli kama tutaendelea kuendekeza utashi wa kisiasa; ni dhahiri kuwa tuwe tayari kuhesabu kuwa hakuna maendeleo ya haraka yatapatika katika nchi yetu bado tukiwa tunatawala na michezo michafu ya siasa; tukumbuke kuwa majukumu  ya kiserikali yanatakiwa kuzingatia zaidi, misingi yake ya utendaji, na utaalamu, nidhamu na ukweli na sio kuendekeza  urafiki na undugu. 

Mheshimiwa Magufuli amethubutu na amejitangazia wazi kuwa yeye ni sadaka ya watanzania katika kupambana na ufisadi na yuko tayari kujitoa Muhanga ili tu watanznaia wanyonge waweze kunufaika na rasilimali za taifa lao.

Mheshimiwa Magufuli utendaji wake unaongozwa na kauli mbiu ya sitawaangusha: Hapa Ni Kazi Tu; katika imani kuwa ameona umasikini na tabu ya Taifa letu hivyo kama watanznia walivyojenga imani kwake hivyo naye ameweka juhudi zote katika kusimamia kwa dhati kabisa rasilimali za Taifa ili kurudisha matumaini makubwa kwa serikali yake anayoiongoza kwa wananchi kwa maendeleo yao.

Binafsi kama mtanzania na mfuatiliaaji wa utendaji wa kazi  Dr. John Pombe   Magufuri,   pamoja  na  mapungufu yake kama binadamu amekuwa miongoni mwa viongozi wachache ;   kama  kiongozi wa juu kabisa hataki kuona watendaji ambao wako chini yake wanatenda kazi kwa mazoea; daima ameonyesha kuthubutu katika kutekeleza sheria na kuwashugulikia watendaji wabovu  huku akiwa tayari kufuata sheria na kujielimisha ili aweze kuzielewa zaidi sheria  za nchi na wizara husika;  

kwa keli ni ni msimamiaji mzuri  wa sheria katika utendaji hata  kama  wakati  mwingine  maamuzi yake yanakuwa kero kwa kwa watendaji wenzake wanaomzunguka lakini bado yanafaida kubwa kwa jamii ya Kitanzania. Kimsingi    kama  nilivyoainisha  hapo  juu  inawezekana  magufuli  akawa  na  madhaifu  yake  lakini  huwezi  kuondoa ukweli kuwa katika kipindi hiki kifupi cha uongozi wake amekuwa kiongozi mzuri wa Juu aliyeweza kufanya  vizuri katika kazi ya kusimamia hata kuchukua hatua kali kwa wakati dhidi ya wale wote ambao wamekuwa na hawafuati maadili ya kazi na vinara wote wa Rushwa na Ufisadi. Hilo  hata     wananchi   wa  kawaida  wameliona hilo nao wamempa tano.

Ni ukweli  ni wazi  kuwa  Magufuli ni kiongozi mchapakazi  na msimamizi mzuri  “Mnyonge mnyongeni  lakini  haki yake mpeni, wengi tunamtambua Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya, tunakuomba uendelee kufanya hivyo hivyo na  Serikali yake ya awamu ya tano iendelee kujiepusha kufanya kazi na watendaji wabovu:  

Watanzania wamemchagua mheshimiwa Magufuli kwa sababu utendaji wake kazi mzuri na kuwa kiongozi ambaye ameonyesha kiwango cha juu cha maadili; na ameonyesha katika kampeni zake kuwa yuko tayari kuwavusha wananchi  kuelekea katika bandari ya salama na yenye amani na maisha bora.

Magufuli ameonyesha upendo wa juu kabisa sio tu kwa watanzania wote bila kujali itikadi zao au dini zao au makabila yao. Ni kiongozi ambaye anaonyesha  upendo kwa wananchi wote; kwake uongozi ni kwa ajili ya wote na sio watu wachahce tu.

Tukumbuke kuwa kuwa uongozi ni dhana nzito ya kuaminiwa ambayo unakabiziwa na watu; lakini na kwa  kuwa uongozi wa kweli ni matokeo ya kuwa na maadili mazuri. Tukumbuke kuwa kuweza kutekeleza majukumu yako vizuri, Lazima kuwe na uhuisano wa karibu kati ya uongozi na mwongozo.
 
Mheshimiwa Magufuli tunaweza sema kuwa  amejitambua mwenyewe kuwa kazi moja ambayo anakabiliwa nayo ni kuwaletea mabadiliko wananchi wa Tanzania hivyo amejiaamini YeYe mwenywe kuwa anaweza kufanya hivyo hivyo anayo mizizi ya huruma na uvumilivu ndani  na ni mtu ambaye haogopi kushindwa

Kiongozi bora atahangaika kuhakikisha kuwa maisha ya wananchi wake yanasonga mbele na kuwa na misha bora. Ukiwa mnyonyaji wewe ni kiongozi mbovu; viongozi ni viashiria vya mabadiliko katika jamii, na kuendeleza mafanikio tukumbuke kuwa sio vigumu kumtawala mtu ila jukumu ni kumwendeleza mtu.

Viongozi wanaishi kwa kuelewa mazingira na tabia za watu; kiongozi lazima awe tayari kuyapokea mabadiliko kila kitu kinaendelea kubadilika; kiongozi lazima ajue kuwa haitakiwi kuogopa awe tayari kujifunza na kamwe ahitimu shule ya mabadiliko, kiongozi lazima awe tayari kuishi na mabadiliko ya tamaduni. kiongozi mzuri anajua mapungufu ya watu wake, mapungufu yetu yanakamilishwa na wengine ambao wanautaalamu zaidi.

uvumilivu ni nguzo muhimu kwa viongozi wazuri ( role model). kiongozi mzuri lazima ajue kuwa kushindwa ni sehemu ya uongozi bora kwani inakupa nguvu ya kuanza upya, unawapenda watu wako kama huwapendi basi usiwe kiongozi hata kama watu hawakupendi bali kama kiongozi bado unatakiwa kuwajali.

kiongozi lazima ujifunze kutokuona wivu wa mafanikio ya watu wengine sio kukosoa kila kitu hata kama mwenzako amefanya vitu vizuri tabia ya kupongezana ni nzuri sana kwa kiongozi mwenzake. viongozi ni wabunifu ambao wanatakiwa kuleta mabadiliko na kuleta utamaduni wa kazi na kudumisha utamaduni wa mafanikio ni wajibu wa kiongozi mzuri, kwa hiyo viongozi wanatakiwa kuwa viashiria wa mabadiliko ya kweli kwa taifa.

 
kiongozi wanatakiwa kuwa na mawazo mazuri ya kimaendeleo na kujua namna ya kuyatumia kwa ajili ya maendeleo ya watu wao na kwa faida ya watu wao, mgonagano wa mawazo ni sehemu tu ya uongozai mzuri. kiongozi hatakiwi kuhangaika wakati kunatokea matatizo ndani ya uongozi kila kitu kipo kwenye mpito. kiongozi lazima uelewe kuwa yale uliyojifunza shuleni wakati mwingine hayafnayi kazi wakati wote na tayari kufahamu kuwa kufanyia utafiti mabadiliko ya tamaduni za uongozi wako.

VIVA MAGUFULI TUNAKUJUA WEWE NI:

Ni Jembe:
Ni Tingatinga
Ni Mtumishi wa watanzania wote
Unayajua mapungufu yako.
Unaongoza kwa usemi wa sisi sisi.
Ni Mnyenyekevu na mtumishi wa watu wote.
Ni mwadilifu
Mtu wa watu hasa wanyonge
Ni Mwogopa Mungu

VIVA MHESHIMIWA  JOHN POMBE MAGUFULI RAISI WA AWAMU YA TANO MWENYEZI MUNGU AKUPE NGUVU YA KULIVUSHA SALAMA TAIFA LA TANZANIA KATIKA MIAKA HII MITANO KATIKA MAENDELEO AMBAYO  SISI WATANZANIA TUMEYASUBIRI KWA MIAKA MINGI SANA;

UKADIRIFU INAKUTAKIA UONGOZI BORA MIEZI HII MINNE YA UONGOZI WAKO KAMA RAISI WA AWAMU YA TANO


Thursday, February 18, 2016

NEW: MATOKEO YA KIDATO CHA NNE -2015

NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA

CSEE 2015 EXAMINATION RESULTS ENQUIRIES


CLICK ANY LETTER BELOW TO FILTER CENTRES BY ALPHABET
A
B
C
D
E
F
G
H
I
J
K
L
M
N
O
P
Q
R
S
T
U
V
W
X
Y
Z