WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Friday, November 30, 2012

Palestina Yazidi Kukubalika




 Na Mwandishi Maalum
 Palestina jana ( alhamisi) imeibuka kidedea baada ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, kuweka historia kwa kupiga kura Azimio lililoipandisha hadhi ya kutambuliwa kama Nchi Muangalizi asiye Mwanachama wa Umoja wa Mataifa. Azimio hilo lilipitishwa kwa kura 138 za ndiyo , kura tisa za hapana na 41 za kutofungamana na upande wowote. Kati ya nchi zilizopiga kura ya hapana na ambazo zilitegemewa ni Marekani, Israel na Canada huku Ujerumani na Uingereza zikipiga kura ya kutofungamana na upande wowote Ukumbi Mkuu wa Mikutano wa Baraza hilo ulifurika wajumbe wa katika tukio hilo la kihistoria lililokuwa na sura ya mchuano mkali wa mpira wa miguu ambapo kila upande ulikuwa ukijitahidi kushangilia kwa nguvu kila msemaji wa upade fulani aliposimama kujenga hoja ya kutaka Azimio liungwe mkono au akijenga hoja ya kupinga Azimio hilo. 

Azimio hilo limeungwa mkono na mataifa mengi kutoka pande zote yaani mataifa yale makubwa kama vile Ufaransa, China, na Urusi nchi ambazo ni wajumbe wa kudumu wa Baraza Kuu la Usalama. Zikiwamo pia nchi nyingi za Jumuiya ya Ulaya, Afrika,Asia na Visiwa vya Karibian Tukio hilo pia lilishuhudiwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, ambaye alisema, kura ya kupitisha azimio hilo ilikuwa ikisisitiza umuhimu wa kutoa msukumo mpya wa kuanza mazungumzo na akazisihi pande hizo mbili kuonyesha dhamira ya kurejea kwenye meza ya mazungumzo. Licha ya ukweli kwamba bado Palestina ina safari ndefu ya kuweza kukubaliwa kuwa mwanachama kamili wa Umoja wa Mataifa, lakini kwa kukubaliwa kwake kuwa na hadhi ya kuwa nchi muangalizi asiye mwanachama, kunaifungulia milango ya kujiunga na taasisi nyingine za kimataifa, ikiwamo Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai( ICC) kama ikitaka kufanya hivyo. 

Akizungumza kabla ya kupiga kura, Rais wa Mamlaka ya Palestina, Mahmoud Abbas, aliwataka wajumbe wa Baraza hilo kuchukua hatua muhimu ya kurekebisha dhuluma ambayo wametendewa wananchi wa palestina kwa muda mrefu. Kwamba alikuwa anaitaka jumuiya ya kimataifa kuliunga mkono azimio hilo na hivyo kupeleka ujumbe wa matumaini kwa wananchi wa Palestina ambao amewaelezea kama walioteseka kwa muda mrefu na waliokuwa wakielekea kukata tamaa. Katika hotuba yake iliyokuwa ikikatishwa mara kwa mara kwa makofi na miluzi kutoka kwa wajumbe wa mkutano huo. Kiongozi huyo wa Palestina, akabainisha kwamba walikuwa wameamua kuchukua hatua hiyo baada ya kuona mazungumzo ya kutafuta amani kati yake na Israeli ni kama vile yalikuwa yamekufa. 

Hata hivyo akasisitiza kwamba wamefikia hatua hiyo ya kupita Baraza Kuu kuomba kupandishwa hadhi na kutambuliwa kuwa nchi muangalizi asiye mwanachama hasa baada ya ombi lao kupitia Baraza Kuu la Usalama kutofanyiwa kazi. Lakini pia wamechukua hatua hiyo kama kielelezo cha kuthamini amani na haki yao ya msingi kama raia wengine ya kuwa na uhuru wa si tu kuwa na taifa lao linalotambuliwa bali pia haki na fursa ya kujiamulia mambo yao wenyewe. “ Hatukuja hapa kutaka kufuta uhalali wa taifa fulani yaani Israeli, lakini tuko hapa kutafuta uhalali wa taifa jingine yaani Palestina,kwamba lazima sasa iijipatie uhuru wake” akasema Mahmoud Abbas Na kuongeza “ Tunawaomba leo hii mtupatie cheti chetu cha kuzaliwa”. Akasama Abbas na kuongeza kwamba uamuzi huo hauna maana kwamba wanaachana na mchakato wa kurejea kwenye meza ya mazugumzo. Wala haukuwa na nia ya kutaka Azimio la kuipandisha hadhi Palestina limepigiwa kura katika tarehe ( Novemba 29) ambayo Baraza hilo lilikuwa likiadhimisha miaka 65 tangu lililopitisha azimio namba 181 lililoigawa Palestina kuwa mataifa mawili lile la Kiyahudi na la Kiarabu. 

Aidha Tarehe hiyo pia huadhimishwa siku ya kimataifa ya mshikamano na wananchi wa Palestina. Siku ambayo ilipitishwa mwaka 1977 Kwa upande wake Balozi wa Israeli katika Umoja wa Mataifa, Ron Prosor yenyewe imesema nchi yake haikubaliani na azimio hilo na kwamba Palestine ilikuwa inafanya kosa kubwa na itakuja kujuta hapo baaaye. Aidha Israel inasema haliitambui Azimio hilo kwa sababu lilikuwa limeegemea upande mmoja na lilikuwa haliitambua taifa la Kiyahudi. Mjumbe huyo wa Israeli akiongea kwa kejeli alieleza baya kwamba, azimio hilo haliwezi kwa namna yoyote ile kuleta amani bali lilikuwa linarejesha nyuma mchakato wote wa kuleta amani, na kwamba yenyewe ilikuwa inamini katika majadiliano badala ya njia za mkato mkato kama iliyofanya Palestina hiyo jana. 

Nayo Marekani kupitia Balozi wake Susan Rice imeeleza bayana kwamba haikubaliani na azimio hilo ambalo kwao ilikuwa ni kama kupoteza muda. Hata pamoja na kukandia na kuzikejeli nchi zilizopiga kura ya kuunga mkono azimio hiyo, Marekani inasema itaendelea na juhudi zake za kuhakikisha kwamba mazungumzo ya kutafuta suluhu ya kudumu kati ya pande hizo mbili yanaendelea. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilikuwa ni kati ya nchi zilizopiga kura ya kuunga mkono azimio hilo, na Balozi Tuvako Manongi alielezea ni kwa nini Tanzania iliamua kupiga kura ya ndiyo. 

Baadhi ya sababu alizotoa ni kwamba Tanzania ilishaitambua Palestina kama nchi huru tangu mwaka 1961 na imekuwa na uhusiano wa kidiplomasia na nchi hiyo kwa miaka mingi. Aidha akasema kwa kupishwa kwa azimio hilo jumuia ya kimataifa ilikuwa inalitambua taifa huru la wapalestina kama vile ilivyoitambua Israel na kwa Tanzania mataifa yote mawili yana uhalali wake. Akaongeza pia kwamba Tanzania inaamini Palestina ilikuwa na kila sababu ya siyo tu kutambuliwa lakini pia kuwa na uhuru wa kujiamulia mambo yake. Akasisitiza kuwa Tanzania inaamini katika makubaliano na majadiliano yanayolenga kufika suluhu ya kuwa na mataifa mawili yakiishi sambamba na kwa amani kulingana na makubaliano ya mwaka 1947;

source:mjengwa blog

Maalim Seif aongoza mamia kumzika mke wa Hamad Dar



Baadhi ya waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza la marehemu Kissa Gwalugano Mohamed,ambaye ni mke wa Mbunge wa Wawi,Zanzibar Bw.Hamad Rashid Mohamed,kwenda msikitini na mazishi kufanyika jana jioni katika makaburi ya Kisutu,Dar es salaam.


Na Goodluck Hongo

MAKAMU wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, jana aliongoza mamio ya waombelezaji katika mazishi 
ya Kissa Gwalugano Mohamed ambaye ni mke wa Mbunge wa 
Wazi, Zanzibar Bw. Hamad Rashid Mohamed.

Viongozi wengine waliohudhuria mazishi hayo ni Pamoja na Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Bw. Wiliam Lukuvi, Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Bw. Ludovick Utouh.


Wengine ni Spika wa Bunge, Bi. Anne Makinda, Mwenyekiti wa CUF Taifa, Profesa Ibrahimu Lipumba, Mwenyekiti wa CHADEMA, Bw. Freeman Mbowe na Mwenyekiti wa UDP, Bw. John Cheyo, viongozi mbalimbali wa Serikali, vyama vya siasa pamoja na wabunge.

Katika msiba huo, viongozi wa kisiasa waliweka pembeni tofauti zao na kumfariji Bw. Mohamed ambaye chama hicho kiliwahi kumfukuza uanachama.

Mazishi hayo yalifanyika Dar es Salaam jana katika makaburi ya Kisutu, saa kumi jioni.

Akizungumza kwa niaba ya familia, Profesa William Matuja aliwashukuru viongozi wote walioshiriki mazishi hayo kwani wamefarijika sana ingawa wamepata pigo kwa kifo hicho.

Marehemu alizaliwa Oktoba 20,1955 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya, alisoma katika Shule ya Msingi Azimio, baadaye Sekondari ya Zanaki jijini Dar es Salaam.

Alisema baadaye alijiunga na masomo ya kompyuta na kuajira THB (iliyokuwa Benki ya Nyumba nchini), lakini alichana kazi na kuamua kujiajiri mwenyewe hadi mauti ilipomkuta.

Alifunga ndoa na Bw. Mohamed mwaka 1984 na walibahatika kupata watoto kati ya hao mmoja wa kiume. Marehemu alikuwa akilalamika kusumbuliwa na mgongo na baada ya kupimwa 
iligundulika kuwa na ugonjwa wa mifupa.

Marehemu alilazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Novemba 27 mwaka huu, baada ya kuzidiwa na kupelekwa katika chumba cha wagonjwa mahututi na kufariki saa tatu usiku.

Majira


1 comment:

  1. Jamani kuna ugonjwa wa mifupa ndiyo nini?? Arthritis?? OMG pole Uncle kwa msiba huu mkubwa jamani, she is too young to die. Yale yale ya seriously viongozi wetu mnahitaji kureview the health system in Tanzania. Just this week nimesoma habari za kusikitisha kuhusu vifo vya vijana ambao na uhakika vimesababishwa na UZEMBE WA MADAKTARI FOR NOT GIVING PROPER DIAGNOSIS OR PROPER TREATMENT.




    Viongozi washiriki mazishi ya mke wa mbunge wa jimbo la wawi , Hamad Rashid

     Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akimfariji Mbunge wa Jimbo la Wawi (CUF) Mhe. Hamad Rashid Mohd nyumbani kwa Mbunge huyo Mikocheni jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha mke wake bibi Kisa Mohd.
     Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akimfariji Mbunge wa Jimbo la Wawi (CUF) Mhe. Hamad Rashid Mohd nyumbani kwa Mbunge huyo Mikocheni jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha mke wake bibi Kisa Mohd.
     Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akimfariji Mbunge wa Jimbo la Wawi (CUF) Mhe. Hamad Rashid Mohd nyumbani kwa Mbunge huyo Mikocheni jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha mke wake bibi Kisa Mohd. Kushoto ni Mwenyekiti wa CUF Prof. Ibrahim Lipumba.
     Sheikh Abdallah Issa (kushoto), akiongoza dua ya kumuombea marehemu bibi Kisa Mohd nyumbani kwake Mikocheni Dar es Salaam.
     Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akisalimiana na viongozi mbali mbali wa vyama vya siasa na serikali katika Makaburi ya Kisutu aliposhiriki mazishi ya bibi Kisa Mohd, mke wa Mbunge wa Wawi (CUF) Mhe. Hamad Rashid Mohd.
     Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akiweka mchanga katika kaburi la marehemu bibi Kisa Mohd, mke wa Mbunge wa Wawi (CUF) Mhe. Hamad Rashid Mohd aliyezikwa katika makaburi ya Kisutu Jijini Dar es Salaam. (Picha na Salmin Said, OMKR)
    Na Hasssan Hamad OMKR

    Viongozi mbali mbali wa vyama vya siasa na serikali wameshiriki katika mazishi ya bibi Kisa Mohd ambaye ni mke wa Mbunge wa Jimbo la Wawi (CUF) Mhe. Hamad Rashid Mohd.
     Mazishi hayo yaliyofanyika nyumbani kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam na kuzikwa katika makaburi ya kisutu, yaliongozwa na Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad.

    Viongozi wengine waliohudhuria ni pamoja na Mwenyekiti wa CUF Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa UDP John Cheyo, Mwenyekiti wa ADC bw. Said Miraji na Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda.
    Mwili wa marehemu huyo ulisaliwa katika msikiti Maamur ulioko maeneo ya Upanga na baadaye kupelekwa katika makaburi ya Kisutu kwa ajili ya mazishi.

    Marehemu bibi Kisa Mohd alifariki Jumanne iliyopita baada ya kusumbuliwa na matatizo ya Presha kwa muda mrefu, na kuzikwa Alkhamis tarehe 29/11/2012.

    Akizungumza katika mazishi hayo, msemaji wa familia hiyo amewashukuru viongozi na wananchi waliojitokeza kushirikiana nao katika msiba huo, na kwamba familia imepoteza mtu muhimu ambaye pengo lake haliwezi kuzibika kwa kipindi kifupi.

    Imewekwa na MAPARA

Bakwata yamkana Sheikh Ponda mahakamani



BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), limemkana Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda na wenzake, baada ya kudai mahakamani kuwa eneo walilovamia wakidai ni mali ya Waislamu linamilikiwa kihalali na kampuni ya Agritanza.
Katibu Mkuu wa Bakwata, Sheikh Suleiman Lolila alisema hayo jana wakati akitoa ushahidi katika kesi ya jinai inayomkabili Ponda na wenzake 49 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakidaiwa pamoja na mambo mengine kuvamia na kupora ardhi na wizi wa vifaa vya ujenzi.
Akitoa ushahidi wake jana huku akiongozwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Tumaini Kweka, Lolila ambaye ni shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka alidai kuwa eneo hilo awali lilikuwa likimilikiwa kihalali na Bakwata.
Hata hivyo, alidai kuwa baadaye Bakwata walibadilishana na Kampuni ya Agritanza Limited baada ya kuona eneo lililobaki halifai kujengwa chuo kikuu kutokana na ufinyu wake.
Alidai kuwa awali eneo hilo lilikuwa kubwa lakini miaka ya 2000 lilianza kumegwa na kuzigawia baadhi ya taasisi na wafanyabiashara na kwamba tume iliundwa na kubaini kwamba hayo yalifanyika kinyume na utaratibu.
“Baada ya kumegwa eneo lililobakia ni finyu ambalo halitoshi kujengwa chuo kikuu. Mimi nilikuwapo wakati Baraza la Wadhamini wa Bakwata wakijadili jinsi ya kupata eneo kubwa na kuijadili Kampuni ya Agritanza iliyokuwa na eneo la ekari 40 Kisarawe ili tubadilishane,” alidai.
Shahidi huyo aliongeza kuwa Agritanza ilikubali kubadilishana maeneo na kwamba wao walichukua ekari nne zilizopo Markaz (Chang’ombe) na Bakwata ikachukua ekari 40 zilizopo Kisarawe.
“Hayo yalifanyika baada ya kupata baraka kutoka katika Baraza la Maulamaa lililokaa na kuamua hivyo Januari 22, 2011,” alisema shahidi huyo na kuongeza:
“Baada ya kufanyika mabadilishano, Agritanza walianza kushughulikia usajili wa kiwanja namba 311/3/4 na walipata. Hivyo kwa sasa ni wamiliki halali, tulishamalizana nao.”
Shahidi huyo aliendelea kudai kuwa eneo hilo Serikali ililitoa kwa Wamisri kwa ajili ya kujenga chuo chini ya usimamizi wa Bakwata.
Alidai kuwa kwa mujibu wa mkataba huo uliosainiwa mwaka 2003, endapo Wamisri wataondoka Tanzania watarejesha eneo hilo katika umiliki wa Bakwata.
Shahidi huyo pia alitoa kielelezo cha makubaliano ya Baraza la Wadhamini wa Bakwata na Agritanza, kuhusu kubadilishana uwanja.
Hata hivyo, Wakili wa utetezi, Juma Nassoro alipinga kwa madai kwamba kisheria walitakiwa kutoa notisi kabla ya kuwasilisha kielelezo hicho mahakamani.
Akijibu hoja hizo, Wakili Kweka alidai kuwa barua halisi wanayo na kwamba ipo katika kumbukumbu za Bakwata, huku akisisitiza kuwa shahidi anastahili kutoa kielelezo hicho kwa sababu saini yake ipo.
Hakimu Mkazi, Victoria Nongwa anayesikiliza kesi hiyo, alikikataa kielelezo hicho akisema Serikali ilitakiwa kutoa notisi kabla ya kuwasilisha kielelezo hicho.
Hakimu Nongwa alisema kwa kuwa barua halisi ipo wanatakiwa kuiwasilisha mahakamani, lakini akasema endapo barua halisi haipo, basi taarifa ya jana itatambulika kuwa notisi na wataruhusiwa kuiwasilisha.
Baada ya kumaliza kutoa ushahidi wake, Hakimu Nongwa aliahirisha kesi hiyo hadi Desemba 13 itakapoendelea kusikilizwa kwa mashahidi wengine wa upande wa mashtaka.
Sheikh Ponda na wenzake walipandishwa kizimbani mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Novemba 18, mwaka huu na kusomewa mashtaka manne likiwamo la wizi wa mali ya Sh59.6 milioni.
Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, washtakiwa wote 50 wanakabiliwa na makosa manne kwa pamoja, lakini Sheikh Ponda na Sheikh Mukadamu Swalehe wakasomewa shtaka jingine zaidi.
Mashtaka manne yanayowakabili washtakiwa wote ni wizi, kula njama, kuingia kwa nguvu kwenye eneo lisilo mali yao kwa nia ya kutenda kosa na kujimilikisha ardhi kwa nguvu na kusababisha uvunjifu wa amani.
Shtaka la tano ambalo linawakabili Sheikh Ponda ambaye ni mshtakiwa wa kwanza katika kesi hiyo na Sheikh Swalehe ambaye ni mshtakiwa wa tano, ni la uchochezi.
Washtakiwa wengine katika kesi hiyo wako nje kwa dhamana isipokuwa Ponda na Swalehe tu ambao dhamana zao zimezuiliwa na DPP.
Wakati washtakiwa hao wakipandishwa kizimbani katika Mahakama hiyo kwa tarehe tofauti, Wakili Kweka alidai kuwa DPP ametoa hati ya kuzuia dhamana yao chini ya Kifungu cha 148 (4) cha Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Jinai (CPA).
Hata hivyo, Wakili anayewatetea washtakiwa hao 50, Nassoro aliipinga hati hiyo kwa madai kuwa sababu zilizotolewa na DPP za kupinga dhamana za usalama na masilahi ya Jamhuri ni za kiujumla na kwamba Mahakama haiendeshwi kwa namna hiyo.
Akijibu hoja hizo, Wakili Kweka alidai kuwa kwa Kifungu cha 148 (4), alichokitumia DPP, Mahakama inafungwa mikono na kwamba kwa mujibu wa kifungu hicho, DPP halazimishwi kutoa sababu yoyote.
Mwananchi

“YANI MTU KAFA KWASABABU DAKTARI HAKUWEPO WAT A SHAME”



 Msomaji wangu alitoa maoni haya ambayo kwa kweli yalinigusa sana kufuatia kifo cha msanii John Maganga ambaye alikuwa anafanya vizuri katika kuelimisha umma wa Tanzania.


YANI MTU KAFA KWASABABU DAKTARI HAKUWEPO,WAT A SHAME JAMANI SISI WATANZANIA WAT A SHAME.

 

“Stephano aliingizwa chumba cha upasuaji, wakati sisi kwa maana ya mimi na baba yake tukiwa tumekaa, dokta alitoka na kutuambia mashine za kupumulia zina matatizo kwa hiyo tunafanya transfer ya kwenda Muhimbili kwa matibabu zaidi, hivyo zilifanyika taratibu na Stephano aliingizwa kwenye gari la wagojwa na kupelekwa hospitali ya  Muhimbili.

 
Baada ya kufika Muhimbili, Stephano aliingizwa chumba cha dharura (emergence room), na baada ya dakika kama 10 hivi, alitoka Doctor ambaye tunafaamiana naye na kusema kuwa, kwa tatizo alilonalo John, hatakiwi kufanyiwa upasuaji kama walivyofikiria madaktari wa Mwananyamala ambapo walidhani kuna utumbo umekatika.

 

Daktari huyo wa Muhimbili aliendelea kutuambia sehemu ambayo inaonekana kuleta matatizo ni sehemu ya kongosho ambapo vipimo vinaonesha ina matatizo, ime fell kwa hiyo ina mwaga maji kwenye tumbo ndiyo maana anapata maumivu kwenye tumbo na tumbo kujaa.

Baada ya maelezo hayo Dokta tunayejuana naye alitueleza kwamba mtaalamu wa tatizo hili hayupo na kwamba anategemewa kuja kesho yake asubuhi na kutuasa tuende nyumbani na kwamba watammwekea mashine ya kupumua na sisi turudi kesho.”

 

Kwa kweli kma  msomaji ambaye ameeleza hisia zake hapo jua, ukisoma maelezo haya kweli yanachefua na kuona kuwa hospitali yetu bingwa ambayo tunaitegemea haina emergency protocol , kwa kweli ni aibu ambayo kama taifa lazima tuitafutie mfumbuzi mara moja;

Je huyo daktari bingwa haruhusiwi kiitwa ili aje kuokoa maisha ya mtanzania mwenzetu?

Je daktari huyo bingwa kwa wakati wa tukio alikuwa Nje ya Mkoa wa Dar es salaam au alikuwa Nje ya Nchi?

Je madakatari wetu bingwa hawaruhusiwi kuitwa kazini kama kuna issue ya dharua?

Au wanaitwa katika shughuli za dharua kwa viongozi wa juu tu na familia zao tu?

Je matababu yetu ya dharua yanakwenda kwa madaraja ili dakatari mhusika aweze kurudi kazini na kuokoa maisha ya mgonjwa?

Maelezo haya kweli yamesikikisha na kuhudhunisha sana na tunajiuliza sisi watu wa hali ya chini tukimbilie wapi sasa wakati wa dharura kama madaktari wetu ambao wanafanya kazi zao kwa viapo ya kuokoa maisha ya watu, hawawezi kurudi kazini kutoa huduma mpaka siku inayofuata;

Serikali yetu inamelionaje jambo hili, inakubaliana nautaratibu huu wa utendaji ambao hauonyeshi kujali maisha ya raia wake kupitia madakatari wetu bingwa na sekta nzima ya afya:

 

MWENYEZI MUNGU AILAZE ROHO YAKO MAHALI PEMA PEPONI SISI TULIKUPENDA LAKINI MWENYEZI MUNGU AMEKUPENDA ZAIDI NDUGU YETU JOHN MAGANGA.

Thursday, November 29, 2012

Bado kuna utata mkubwa kuhusu demokrasia ya kweli Barani Afrika



Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe


 
Mpinzani wa Mugabe, Morgan Tsvangirai


 
Kiongozi wa Kambi rasmi ya Upinzani Tanzania,
Freeman Mbowe

BISHOP J. HILUKA
Dar es Salaam
RIPOTI iliyotolewa na shirika moja linaloheshimiwa sana nchini Afrika Kusini inayoonesha kuwepo orodha ya wapiga kura hewa milioni 2.6, kwa dhamira ya kuendeleza udanganyifu, katika daftari la kudumu la wapiga kura nchini Zimbabwe, inatuthibitishia kuwa demokrasia ya kweli barani Afrika bado ni kitendawili.

Orodha hiyo inaashiria kuwepo zaidi ya watu elfu 41 walio na umri wa zaidi ya miaka 100 - hii ikiwa ni mara nne zaidi ya idadi ya watu hao nchini Uingereza, ambayo ina idadi kubwa zaidi ya watu na muda mrefu wa kuishi ikilinganishwa na Zimbabwe.

Hii imekuja wakati Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, akiitisha uchaguzi ufanyike mwaka huu, huku mpinzani wake na Waziri Mkuu katika serikali ya mseto, Morgan Tsvangirai, akisema kuwa uchaguzi huo unapaswa kuandaliwa mwaka 2012 baada ya katiba mpya kuidhinishwa ili kuhakikisha kuwa kuna uhuru na haki.

Wastani wa umri wa kuishi miongoni mwa raia wa Zimbabwe umeteremka hadi miaka 49, lakini kumeripotiwa kuwa na wapiga kura 41,100 wanaodaiwa kuwa na zaidi ya umri wa miaka 100.

Serikali za Kiafrika zimekuwa na tabia ya 'kuchakachua' ili ziendelee kutawala, na kuna uwezekano kuwa nchi nyingi za Afrika pamoja na kujidai kuwa na chaguzi huru huwa zinatawaliwa kwa mabavu na si kwa ridhaa ya wananchi, kutokana na uchakachuaji kama huu wa kura.

Naamini kwamba kwa mustakabali wa nchi yoyote, vyama vyote vya siasa vina haki sawa mbele ya katiba ambayo pia inawapa wananchi haki na uwezo wa kuchagua chama chochote kati ya hivyo vilivyopo na kukiweka madarakani.

Ni kutokana na ukweli huo, sheria na kanuni za uchaguzi zinahitaji kuwepo na mazingira sawa kwa vyama vyote vinavyoshiriki uchaguzi. Mazingira hayo ni muhimu ili kutoa fursa ya mshindi kupatikana katika misingi ya kidemokrasia ambayo hustawi katika uchaguzi ulio huru na wa haki.

Kwa msingi huo, Serikali nyingi za Kiafrika zinapaswa kujenga utamaduni wa majadiliano ya kina, kukuza na kudumisha demokrasia pamoja na kuwashirikisha watu katika mchakato mzima wa kujiletea maendeleo yao, jambo ambalo litasaidia kwa hakika kujenga na kuimarisha misingi ya haki, amani, upendo na mshikamano kati ya watu.

Lakini hii demokrasia, hasa kwa nchi za Afrika ni neno ambalo kwa miaka mingi sasa limekuwa likipita masikioni mwa watu wengi hali ya kuwa wengi wao hata hawajui maana na uzito halisi wa neno hilo. Kwa lugha rahisi, neno hili linatafsiriwa kama aina ya uongozi wa watu kwa ajili ya watu. Uongozi huo hupatikana kwa kufanyika uchaguzi ambao unatakiwa uwe huru na wa haki.

Uchaguzi huru na wa haki unamaanisha kwamba wananchi wagombee nafasi za uongozi wanazotaka ikiwa wana sifa zinazostahili, wawe na uhuru wa kuongea na wananchi wenzao kuhusu sera na mipango yao pindi watakapopewa dhamana ya kuwaongoza ikiwa ni pamoja na kuukosoa uongozi uliotangulia bila uwoga wa aina yoyote kwa kueleza ukweli waziwazi kuhusu 'madudu' yaliyofanywa na uongozi huo na jinsi gani wao wataweza kufanya marekebisho na kuboresha hali ya maisha ya wananchi wenzao pamoja na nchi kwa ujumla.

Pia wawe huru kuwachagua viongozi wanaowataka bila woga wala vitisho, wala kununuliwa hati zao za kupigia kura kwa kilo mbili za sukari na upande wa khanga kutokana na hali zao kimaisha kuwa duni kiasi kwamba hawawezi hata kukumbuka ni lini ilikuwa mara ya mwisho kwao kunywa chai yenye sukari!

Katika hili nchi za Afrika zinatakiwa kuacha unafiki wa kujifanya zinafuata demokrasia na utawala bora wakati sio kweli. Sasa wakati umefika kwa viongozi wa Afrika kuyafanya kwa vitendo wanayohubiri na kuondokana na mfumo wa utawala jeuri na wa kibabe, kwa ajili ya mafao na maendeleo ya watu wa Afrika, Bara ambalo kwa miaka mingi linaendelea kukumbana na kinzani, migogoro na hali ngumu ya maisha.

Wakati umefika kwa nchi za Kiafrika kujenga na kuimarisha misingi ya haki jamii, ugawaji bora zaidi wa rasilimali ya nchi, utengenezaji wa fursa za ajira kwa kuboresha mazingira ya wananchi wanaoishi vijijini ili waweze kutumia ardhi waliyonayo kwa ajili ya maboresho ya hali ya maisha yao. Serikali hizi zina changamoto ya kuondokana na ubinafsi, uroho wa mali na madaraka, mambo ambayo yamelitumbukiza Bara la Afrika katika kinzani, migogoro na vita ya wenyewe kwa wenyewe.

Uongozi ni dhamana nzito ambayo inatakiwa iwe kwa ajili ya watu na nchi husika kwa ujumla na si kwa ajili ya maslahi binafsi ya wachache kama wafanyavyo wengi katika nchi za Afrika, ambao wengi wao wanaingia madarakani kiujanjaunjanja au kinyume na misingi ya demokrasia.
Pia kuwepo matumizi ya nguvu na vitisho katika nchi ni dalili ya ung'ang'anizi wa madaraka na hivyo kuondoa maana halisi ya demokrasia! Ung'ang'anizi huu mara nyingi unaashiria kwamba viongozi wetu hawana sifa ya kupewa dhamana hiyo.

Vitisho na hasa matumizi ya nguvu kwa wapinzani wa serikali ni dalili ya kufilisika kwa ushawishi, kwani huambatana na kimbilio la vitisho kama njia ya kujihami! Serikali kutumia vitisho kwa watu binafsi si haki, kwani mtu unayemzidi uwezo huwezi kumtishia kwa sababu hakutishii au hakusumbui.

Bara la Afrika halina budi kusoma alama za nyakati, kwa kutambua mabadiliko ya uongozi, nafasi na dhamana ya vijana katika kuleta mabadiliko, bila kusahau athari za matumizi ya vyombo vya mawasiliano ya jamii, yanayoiwezesha dunia kuwa kama ulimwengukijiji.
Imewekwa na Mkereketwa

Mmiliki gari lililomuua Sharo Milionea alonga



MMILIKI wa gari ambalo lilikuwa likiendeshwa na msanii maarufu nchini, Hussein Ramadhan ‘Sharo Milionea’ na kupata nalo ajali iliyosababisha kifo chake huko Muheza, Tanga, Mohammed Ismaili maarufu kwa jina la Mudi Suma, ameibuka na kueleza uhusiano wake na marehemu, huku akisema amekubali hasara.
Akizungumza kwa simu kutoka Muheza jana Suma alisema hana mpango wa kudai fidia au kupeleka malalamiko yoyote kwa ndugu wa marehemu kwa kuwa; “Kilichotokea ni kazi ya Mungu.” “Siwezi kudai hata kidogo hivyo ni vitu vya kupita tu. Marehemu alikuwa ni zaidi ya ndugu yangu, gari ni kitu kidogo sana katika uhusiano tuliokuwa nao,” alisema Suma na kuongeza kwamba hata Marehemu Sharo Milionea naye alikuwa amemwachia mali zake kadhaa ikiwamo gari.
“Siyo gari tu alilokuwa ameniachia. Kuna mikataba yake ya kazi, Bajaji yake na funguo za chumbani kwake. Nasubiri kukabidhi vitu hivyo baada ya kukaa na ndugu zake. Vitu viko kwenye mikono salama,” alisema.
Kuhusu gari lake lililopata ajali, Suma alisema lilikuwa na bima ndogo, lakini anapanga kwenda TRA atakaporejea Dar es Salaam kufuatilia baadhi ya mambo.
“Kabla ya kuondoka bima ile kubwa ilikuwa imekwisha kwa hiyo nikaamua kuikatia bima ndogo. Nitakapofika kesho (leo) Dar es Salaam, nategemea kwenda ofisi za bima kuzungumza nao,” alisema Suma.
Alipoulizwa kama kuna mtu mwingine atakayeathirika kutokana na gari hilo kuharibika katika ajali mbali na yeye, alijibu: “Hakuna tofauti na mimi mwenyewe na familia yangu.”
Kabla ya ajali
Suma alieleza kuwa kabla ya kuanza safiri yake, Sharo Milionea alifika nyumbani kwake mchana na kumweleza kuwa afya yake haikuwa nzuri.
“Kabla ya kuondoka aliniambia kuwa hajielewi elewi na kifua kilikuwa kinambana. Nikamshauri asiondoke peke yake, atafute mtu wa kuondoka naye ambaye atamsaidia kuendesha gari njiani,” alisema Suma na kuongeza:
“Tulianza kuwapigia simu jamaa zetu wanne wa kusafiri naye lakini kila tuliyemwambia hakuwa tayari. Ilikuwa ni changamoto mpaka ilipofika saa 10:45 hivi jioni, akaamua kuondoka peke yake. Wakati anatoa gari getini kwangu, nikamwambia, basi jaribu kuwa mwangalifu sana, maana alikuwa kweli anasumbuliwa na kifua. Tukakubaliana kwamba atakaporudi aende hospitali kucheki afya yake.”
Kuhusu uhusiano wake na marehemu, Suma alisema: “Mimi ni mfanyabiashara na yeye alikuwa msanii, lakini ilitokea tukawa marafiki sana mpaka ikafikia wakati nikaona kuwa ni ndugu yangu. Nilimwamini nikamtambua kama sehemu ya familia.”
Alisema marehemu alikuwa akitumia gari hilo kila alipolihitaji na safari ya kwenda nalo Tanga kwa wazazi wake ilikuwa ni ya tatu.“Siyo mara ya kwanza kuitumia gari lile, nilikuwa nimemwamini sana. Safari ya kwanza alichukua na kusafiri nalo mwenyewe, halafu safari ya pili ikafuata na hii ilikuwa safari ya tatu,” alisema Suma.
Eneo la ajali wakimbia makazi
Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Songa Kibaoni mahala ambako Sharo Milionea alipatia ajali, wamezikimbia nyumba zao baada ya Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu kutoa siku moja kwa waliopora mali za marehemu huyo kuzisalimisha mara moja.

Mgalu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Muheza alisema jana kwamba usiku wa kuamkia jana, baadhi ya nyumba kijijini hapo zilikuwa tupu baada ya wakazi wake kuzikimbia.
“Baadhi ya nyumba katika Kijiji cha Songa Kibaoni usiku wa kuamkia leo (jana) zilikuwa tupu, wenyewe wamezikimbia baada ya kusikia amri yangu ya kutaka waliopora vitu vya marehemu Sharo Milionea wavisalimishe,” alisema Mgalu.Alisema kukimbia kwao ni ishara kwamba walihusika katika uporaji wa fedha na vitu vya marehemu mara baada ya ajali.
“Tumewaachia ngazi ya ukoo waendeshe mchakato wa kupiga kura za kuwafichua wahusika wa tukio la uporaji wa msanii huyo halafu majina yao watuletee sisi ili tutumie utaalamu wetu kuwanasa waliohusika,” alisema Mgalu.
Mkuu huyo wa Wilaya alisema mbali ya mchakato huo, amri yake ya kufanya msako wa nyumba kwa nyumba iko palepale.
Alisema anataka kuonyesha mfano wa makali ya Serikali kwa waliohusika na uporaji huo ili kuwa fundisho kwa wengine wanaoishi kandokando ya barabara wenye tabia ya kupora mali za wanaopata ajali.
Mwananchi

ZANZIBAR HEROES KIBOKO YA AKINA NIYONZIMA - WAWAPIGA MBILI MTUNGI

Mfungaji wa goli la kwanza la timu ya Zanzibar Heroes akiambaa na mpira huku mabeki wa timu ya Rwanda wakijaribu kumzuia wakati wa mchezo wa mashindano ya Cecafa Challenge uliochezwa katika Uwanja wa Nelson Mandela uliopo Nambole nchini Uganda

Wachezaji wa Zanzibar Heroes wakishangilia goli wakati wa mchezo dhdi ya timu ya Rwanda uliochezwa katika Uwanja wa Nelson Mandela uliopo Nambole nchini Uganda katika mashindano ya Cecafa Challenge

source: shaffih Dauda.blog

Jaji Chande Aikwepa Kesi Ya Lema




 JAJI Mkuu wa Tanzania, Mohamed Othman Chande amejitoa kusikiliza rufaa ya kesi ya aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, badala yake nafasi yake imechukuliwa na Jaji Bernard Luanda.
Kujitoa kwa jaji mkuu kumekuja ikiwa zimebaki siku tano kusikilizwa upya kwa rufaa hiyo Desemba 4, mwaka huu, baada ya awali Mahakama ya Rufani, kuona rufaa hiyo ilikuwa na dosari.
Mahakama hiyo ilikubali hoja ya wajiburufaa kuwa rufaa hiyo ilikuwa na dosari kutokana na tofauti ya vifungu vya sheria vilivyotumika katika hukumu iliyomvua ubunge Lema na vilivyotumika katika hati ya kukaza hukumu, iliyowasilishwa mahakamani sambamba na rufaa hiyo.
Hata hivyo, kilichomwokoa Lema ni kifungu cha 111 cha Kanuni za Mahakama, ambapo mahakama hiyo ilisema kuwa chini ya kanuni hiyo, dosari hizo zinaweza kurekebishwa.
Jaji Chande ndiye aliyekuwa kiongozi wa jopo la majaji watatu katika kesi hiyo akiwamo Salum Massati na Natalia Kimaro.
Jaji Mkuu aliingia kwenye kesi hiyo akichukua nafasi ya Jaji Mbarouk Salim Mbarouk aliyekuwa amepangwa awali, ambaye sababu za kuondolewa hazikuwekwa wazi.
Wakili wa  Lema, Method Kimomogoro alithibitisha kuwa amepata taarifa kuwa jaji mkuu hatasikiliza rufaa hiyo na badala yake Jaji Luanda ndiye atachukua nafasi yake.
“Ni kweli jaji mkuu hatakuwapo kusikiliza rufaa ya Lema nimewasiliana na Msajili Dar es Salaam ameniambia hatokuwepo kwenye hilo jopo,” alisema Kimomogoro na kuongeza:
Hata hivyo, Wakili Kimomogoro alisema “Huu ni utaratibu wa kawaida wa mahakama kwa kuwa huenda jaji mkuu akawa amesafiri au ana shughuli nyingine.”
Wakili wa wajiburufaa, Alute Mughwai alisema hajapata taarifa kama Jaji Mkuu ameondolewa kwenye jopo hilo kwa kuwa huo si utaratibu wa mahakama kutoa taarifa hizo.
“Mahakama huwa haitoi taarifa, zinawekwa (taarifa) kwenye ubao wa mahakama siku ambayo rufaa inasikilizwa,” alisema.
Aliendelea, “Jaji yeyote atakayepangwa sisi hatuna tatizo kwa kuwa wote ni majaji, wewe uko huko Dar na mimi niko huku bara (Arusha), hivyo unaweza ukazipata taarifa zaidi huko kwa kuwa ndiyo uko jikoni Dar.”