WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, November 24, 2012

Kutoka ikulu Zanzibar:Taswira Mbalimbali za Rais wa Zanzibar Dk Ali Shein Alipotua Nchini Vietnam na Muendelezo wa Ziara Yake Nchini Humo



  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed shein, na Mkewe Mama Mwanamwema Shein,wakipokea mashada ya mauwa kama ni Ishara ya ukaribisho katika Ikulu ya Vietnam,alipofika kwa mazungumzo na Makamo wa Rais wa Vietnam Bibi, Nguyen Thi Doan,akiwa na ujumbe wake katika ziara rasmi ya Kiserikali nchini humo ya wiki moja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed shein, akiwatambulisha Viongozi aliofuatana nao kwa Makamo wa Rais wa Vietnam Bibi,Nguyen Thi Doan,walipowasili Ikulu ya nchi hiyo kwa mazungumzo,ya kuimarisha uhusiano na Ushirikiano baina ya pande zote, akiwa katika ziara rasmi ya wiki moja nchini humo.
  Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwamamwema Shein, akisalimiana na Makamo wa Rais wa Vietnam Bibi, Nguyen Thi Doan,alipowasili Ikulu nchini Vietnam,alipofuatana na Rais wa Zanzibar katika ziara Rasmi ya Kiserikali Nchini Vietnam ya wiki moja
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed shein, akisalimiana na Mawaziri na Viongozi mbali mbali wa Nchini Vietnam ,alipofika ikulu ya nchi hiyo kwa mazungumzo na Makamo wa Rais Vietnam Bibi, Nguyen Thi Doan, akiwa katika ziara rasmi ya Kiserikali nchini humo ya wiki moja
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed shein, akisalimiana na Makamo wa Rais Vietnam Bibi, Nguyen Thi Doan,alipowasili Ikulu nchini Vietnam,akiwa na ujumbe wake katika ziara rasmi ya Kiserikali nchini humo ya wiki moja
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed shein,(katikati) akiwa ujumbe aliofuatana nao katika Mkutano maalum na Uongozi wa Serikali ya Vietnam,ukiongozwa na Makamo wa Rais wa Nchi hiyo Bibi Nguyen Thi Doan,(hawapo pichani) katika ukumbi wa Ikulu ,katika kuimarisha Uhusiano na Ushirikiano baina ya pande mbili hizo,katika ziara rasmi ya Kiserikali.
Viongozi wa Serikali waliofuatana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi wakiwa kwenye mkutano maalum na uongozi wa serikali ya Vietnam.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekitri wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed  Shein, akiteta jambo na  mwenyeji wake Kiongozi Mkuu katika Ofisi ya Rais Ikulu Nchini Vietnam,Bw Giang Son,wakiwa katika ukumbi wa Mapunziko  VIP  katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hanoi Nchini Vietnam,akiwa na ujumbe wake katika ziara rasmi ya Kiserikali
Mama Mwanamwema Shein,(kulia) Waziri wa Kazi Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika Haroun Ali Suleiman,(atikati) na Balozi wa Tanzania Nchini China,pia akiwa anafanya kazi zake nchini Vietnam, Philip Sang'Ka Marmo,wakiwa katika Chumba cha Mapumziko  VIP  katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hanoi Nchini Vietnam,wakiwa ni miongoni mwa Ujumbe wa Rais wa Zanzibar Nchini Vietnam
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Maofisa wa Serikali ya Vietnam, alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hanoi Nchini Vietnam, akiwa katika ziara rasmi ya Kiserikali
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekitri wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed  Shein,(katikati) akifuatana na mwenyeji wake Kiongozi Mkuu katika Ofisi ya Rais Ikulu Nchini Vietnam, Bw Giang Son,(wa pili kushoto) baada ya mapokezi rasmi katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hanoi Nchini Vietnam,akiwa na ujumbe wake katika ziara rasmi ya Kiserikali,(kushoto) Balozi wa Tanzania Nchini China,pia akiwakilisha nchini Vietnam Philip Sang'ka Marmo.

Picha Zote na Ramadhan Othman,Ikulu-Zanzibar

No comments:

Post a Comment