WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Tuesday, November 20, 2012

TAARIFA YA MSIBA NEW YORK



THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
PERMANENT MISSION TO THE UNITED NATIONS



Tel: (212) .972.3612
Fax: (212) 697.3618.
E-mail: tzny@tanzania-un.org
tzrepny@aol.com

201 East 42nd Street
Suite 425
New York, NY 10017

TANGAZO LA MSIBA

Mhe. Tuvako Manongi, Balozi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, kwa majonzi makubwa, anasikitika
kutangaza kifo cha Jesca Emmanuel (12), Mtoto wa Afisa mwenzetu Bw.
Emmanuel Swere Alfred na Bi Doto, kilichotokea ghafla siku ya Jumapili
18/11/2012 katika Hospitali ya Mt. Sinai, Queens, New York. Taratibu na
mipango ya kuusafirisha Mwili wa Marehemu Mtoto Jesca kwenda kijijini
Bumbombi- Shirati Tanzania kwa mazishi zinaendelea kwa usimamizi wa
Ubalozi na Familia ya Marehemu.

Taarifa zaidi zitatolewa na Ubalozi kuhusu siku, tarehe na mahali
tutakapomuaga mpendwa wetu Jesca Emmanuel.

Raha ya Milele Umpe Eee Bwana na Mwanga wa Milele Umuangazie
apumzike kwa amani. Amina

UBALOZI WA TANZANIA UMOJA WA MATAIFA

NEW YORK
rambirambi unaweza kufika kwa address hii. 
30 River Road Apt 16K, Roosevelt Island, NY 10044. 

Phone # 646-552-8578 au 646-552-7743
source vijimambo

No comments:

Post a Comment