WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Sunday, March 31, 2013

UCHAGUZI WA RAIS KATIKA JAMUHURI YA WATU WA KENYA 2013; UMEKWISHA NA UHURU KENYATTA NI RAIS MTEULE KUAPISHWA April 9 2013





  • NI KWELI KUWA SIASA NI MCHEZO MCHAFU?

  • KAMA NCHI JIRANI TUMEJIFUNZA NINI?

Siasa ni mfumo ambao unahusisha zaidi uongozi wa watu kwa kufuata kanuni, sheria, sera, uwajibikaji, uwazi na ugawaji wa rasilimali sawa kwa wananchi wake hasa  katika kuwaleta maendeleo  wadau wakuu kwa maneno mengine wanahisa wakuu ambao  ni wananchi.

Kwa msingi wa utashi huu, wananchi wanakichagua kikundi cha watu au chama ambacho wanawaamini na kuwapa uwezo wa kuunda serikali ili iwaongoze kwa niaba yao.  Kwa hivyo hakuna nchi yeyote hapa duniani ambayo haina serikali. Tofauti inayoweza kujitokeza ni namna serikali hiyo inavyoundwa katika misingi ipi? Na inatekeleza vipi kanuni na taratibu zake? Je kuna uwazi katika shughuli zake? Viongozi wanabebe dhamana ya watu katika utendaji wao na wawajibikaje kwa wananchi ambao ndio waliowaweka ofisini; na viongozi wanatakiwa wawajibike na kuwaletea maendeleo wananchi wao.

Siasa kama siasa sio mchezo mchafu; siasa inageuka kuwa mchezo mchafu pale tu serilali au chama cha upinzani  ambavyo vimekabidhiwa dhamana na wananchi  vinaanza kwenda kinyume na utaratibu na kanuni sahihi,  na kuto fuata   maadili ya uongozi (code of conduct) ndipo tafsiri ya siasa inaanza kugeuka na kuwa mchezo mchafu. 

Misingi ya siasa chafu imechochewa sana na mwanasalsafa Machiavelli  ambaye aliandika katika maandishi yeke kuhusu viongozi na madaraka; kitabu chake kinawanufaisha sana viongozi katika kuimarisha  nafasi zao za uongozi, amewafundisha viongozi namna ya kuwa waongo (liar), wakatili, wanafiki,  kuwa na uchu wa mali, na hata ikibidi kuua ili kupata madaraka na kuudumisha adhima yao ya kuendelea kunyonya na kujitajirisha. mwongozo huu wa Machiavelli unatumiwa sana na watawala wa mabavu (dictators), kutoka nchi mbalimbali ambao waliongoza au wanaongoza nchi zao kwa manufaa binafsi na sio kuwaletea maendeleo wananchi bali huwajengea hofu na kuwasababishia wananchi wao maisha magumu. Tumewaona  watawala kama; Idd Amin Dada, Mabuto, na kadhalika. Katika mlengo huu hakuna kuwajibishana, kinachofanyika hapa wananchi wanatiwa tu kufuata na  kusikiliza na kutii tuKila kiti ambacho wananfanya na wanatakiwa kuwa watiifu kama usipotia au kama ukikidhana kimawzo na viongozi hao unaishia pabaya tumeona vifo na maisha magumu ya baadhi ya wananchi, ambao waliishia kuishi ughaibuni.
 

Uchafu wa siasa ni pale tunapoilinganisha siasa kama wapiganaji katika mchezo wa mieleka ule ambao hauna kanuni yeyote ili ushinde, unaweza kumchezee au kumpiga au kumwangusha mpinzani wako kwa namna yeyote ile uwezayo ili mradi tu wewe uwe mshindi; hapa hakuna  kanuni yeyote inayohitajika refarii yuko pale kutangaza mshindi tu kwani hana kanuni yeyote ambayo anafuata; hapo ndipo tafsiri ya mchezo mchafu inapoanza.je nini kazi ya wanasheria wetu? Utetezi au uonevu? Tatizo la mchezo huu ukiuanza huwezi kuuacha. Ushauri kama huuwezi kamwe usiucheze waache wanaouweza waucheze,  watu wenye kiburi na wasiojali utu hata mara moja. Na ukiamua kuucheza kamwe usiuache au usiwasaliti wenzako ukifanya hivyo safari yako yakuendelea kufurahia maisha ya siasa yataishia kaburini.

Je siasa zetu zinalenga wapi tunaoutaratibu ambao tunaweza kumwajibisha hata kiongozi wa juu wa    nchi anapokiuka maadili ya uongozi? mkumbuke Nixon na “Watergate scandal” kwa kosa lolote lile ambalo alifanya akiwa kama kiongozi mkuu wan nchi alikiuka maadili ya uongozi kulingana na taratibu za serikali ya Marekani kilichofuata ni kumpigia kura ya kutomwamini na kumwondoa ofisini kama Raisi; alikwenda kwenye ziara kama Raisi wa Marekani ndani ya "Airforce One" lakini alirudi nyumbani kama raia wa kawaida kwa kutumia ndege ya kawaida ya abiria.

                                                                 
Siasa sio mchezo mchafu kwa watu ambao ni wanyeneyekevu na wenye huruma ya kuwahurumia wanyonge, watu wanaomwogopa Mungu, na daima sio wala rushwa, siasa kama kazi ni sawa na kazi nyingine zinazotakiwa kufuata taaratibu, tukumbuke kuwa iwapo mtu mwenye haki anaongoza nchi kila mtu atafurahia matunda na maziwa yatokanayo na rasilimali ya nchi hiyo, lakini iwapo nchi itaongozwa na mtu mwovu, fisadi wanyonge wataumia sana na wenye nacho wataongezewa. Na hapo tutakendelea na kilio cha kila siku kwanini sisi ni masikini katika nchi hii iliyojaa maziwa na asali na wakati huo huo inawatajirisha watu au inchi nyingine?

Tukumbuke kwa wale ambao wamesoma kitabu cha sharkespear  nini alikifanya Macbeth kwa kusababisha umwagaji wa damu ambao ulikuwa hauna sababu kwa sababu tu ya  siasa  za ubinafsi na hatimaye kutekeleza mwonekano wa siasa kuwa mchezo mchafu ambao mwisho wa siku ulimgeukia mwenyewe na kuuwawa. Tatizo la uchafu wa siasa pengine huanzia kwa serikali kuona kuwa ofisi zao ndio biashara yao hivyo hata ile mishahara ambayo wamewekewa kisheria haiwatoshi na huanza kujiingiza katiak rushwa, mikataba mibovu ambayo inawapa masilahi wao binafsi, na kuwaongezea nguvu ya kipesa na uwezo wa kuongoza kwa masilahi ya watu wachache.

Siasa sio mchezo mchafu kwa watu ambao ni wanyeneyekevu na wenye huruma ya kuwahurumia wanyonge, watu wanaomwogopa Mungu, na daima sio wala rushwa, siasa kama kazi ni sawa na kazi nyingine zinazotakiwa kufuata taaratibu, tukumbuke kuwa iwapo mtu mwenye haki anaongoza nchi kila mtu atafurahia matunda na maziwa yatokanayo na rasilimali ya nchi hiyo, lakini iwapo nchi itaongozwa na mtu mwovu, fisadi wanyonge wataumia sana na wenye nacho wataongezewa. Na hapo tutakendelea na kilio cha kila siku kwanini sisi ni masikini katika nchi hii iliyojaa maziwa na asali na wakati huo huo inawatajirisha watu au inchi nyingine?

Katika nchi zetu ambazo umasikini umekidhiri, tatizo la kukosekana kwa ajira, kupeana kazi na vyeo kwa kufuata undugu na urafiki na sio sifa za elimu, kuwanunua watu kwa kuwapa zawadi wakati wa kampeni na hatimaye wakati wa upigaji wa kura, kwa misingi hiyo sio rahisi baada ya uchaguzi kwa wananchi kuwawajibisha viongozi wao. Siasa taalumu nzuri sana na muhimu kwa jamii ikiwa itawapata viungozi wazuri na waungwana ambao wamewaeka wananchi mbele ya maendeleo yao, lakini siasa ikiwapata viongozi wabovu wala rushwa nchi imekwisha na wanyonge hawana chao ndipo hapo siasa inapokuwa ni mchezo mchafu. Kwa msingi huu ni kuwa siasa sio mchezo mchafu ni mchafu tu ikipata watu wala rushwa  na sio waaminifu, walafi wa madaraka,
 
Ni mchezo mchafu tu kama utaratibu wote wa uchaguzi haukwenda vizuri na matokeo yake baada ya hapo ni chuki binafsi baina ya vyama na hiyo mwisho wa siku itamaanisha kuwa chama tawala na  chama cha upinzani ni maadui na hakuna wa umuhimu wa chama kingine kuwapo, vyama vya siasa katika nchi vinaweza kuiongoza kwa kupokezana ni kama huko Marekani wakati wananchi wanapoona kuwa nchi iko amani yao ina mashaka wanakipigia chama cha Republican lakini wakiona uchumi wao unayumba wanakipigia chama cha Democratic;

Tukumbuke maneno ya Raisi JF Kennedy wa Marekani alivyosema” hakuna mtu ambaye atanishawishi mimi kufanya kitu ambacho nafikiri sio kwa masilahi ya nchi yangu, kama wewe au mtu mwingine anafikiri kuwa ndiye, basi huyo ni Mwendawazimu” Hii ndio tofauti ya kiongozi ambaye kwake siasa ni mchezo mzuri kwa masilahi ya wananchi wake na taifa lake, ambaye ni mkweli mwadilifu na ambaye anaweza kutoa maamuzi mazito kwa faida ya nchi yake;

 LAKINI pale tunapokosa maadili ya uiongozi tunakaribisha sana  urafiki, undugu na kugeuza ofisi zetu ambazo zimewekwa kwa masilahi ya Taifa kuwa sehemu za biashara na kuwakaribisha zaidi wenye fedha kututawala kwa kutoa mwongozo nini kifanyike hapo ndipo tunabadilisha tafsiri sahii ya siasa kuwa mchezo mchafu. Pengine bora hata kiongozi ambaye ni mbabe wa maendeleo ya taifa ambaye anapinga uzembe na hana rafiki wala ndugu ndugu yake ni maendeleo ya nchi yake. Je tunao viongozi wa namna hii hasa barani Afrika. tumkumbuke Mzee wetu, Mandela Nyerere na wengine wa namna kama yao.


Uchaguzi wa Jamuhuri ya watu wa Kenya ambao ulifanyika  March 3 2013 tunamshukuru Mungu umeisha salama ambapo mgombea wa urais wa Muungano wa Jubilee Bwana Uhuru Kenyatta amefanikiwa kuwashinda wagombea wenzake nane akiwiwamo mshindani wake wa karibu na waziri Mkuu ambaye amemaliza kipindi chake bwana Raila Odinga.

Kama wanahabari wengi walivyoandika kuwa umekwenda vizuri pamoja na kasoro ambazo zimejitokeza lakini demokrasia imeheshimiwa na wananchi wameyapokea matokea wakiwa na nia mpya ya kuijenga Kenya mpya. Pengine uchaguzi wa mwaka 2007 ambao ulishia na machafuko na mauaji ya wananchi ambao hawana hatia tayari limekuwa ni somo nzuri na wananchi hawataki kurudi tena huko.

Kama wadau wakuu wa siasa wananchi wameamua kuheshimu matokeo kwa faida ya Taifa.Tuchukue fursa hii pia kuwapongeza Wakenya kwa kufanikisha uchaguzi mkuu kwa amani na utulivu. Ni imani yetu kwamba utulivu huo utadumishwa pasipo kuathiriwa na hila zinazohusisha uhasama wa aina yoyote ile.Baada ya maamuzi ya Mahakama kuu kuhusu Pingamizi ambayo Mheshimiwa Odinga aliweka na Mahakama kutupilia mbali pingamizi hiyo na MAHAKAMA KUU YAAMUA UHURU NDIYE MSHINDI HALALI

“Mahakama ya Juu imefikia uamuzi kwa kauli moja kuhusu masuala manne yaliyoibuliwa kwenye kesi za uchaguzi. Uchaguzi ulifanyika kwa njia huru na ya haki na kwa kufuata Katiba na Sheria,” alisema Jaji Mutunga kabla ya kutangaza kuwa Uhuru Kenyatta na William Ruto walichaguliwa kwa njia huru na ya haki kuwa Rais na Naibu Rais mtawalia.

“Kesi za Raila na AFRiCOG zimetupwa. Kila mtu ajilipie gharama. Uamuzi wa kina utatolewa katika muda wa wiki mbili.”

Hebu tuangalie kauli mbalimbali kufuatia uamuzi wa mahakama:

“Mahakama imetekeleza jukumu lake. Jukumu sasa ni kwa raia, viongozi wao, mashirika ya kijamii na wanahabari kuhakikisha umoja wa Kenya unadumu,” alisema Jaji Mutunga.
WAZIRI MKuu Raila Odinga amekubali kushindwa baada ya Mahakama ya Juu kutupilia mbali kesi yake kupinga kupinga kuchaguliwa kwa Uhuru Kenyatta. Bw Odinga amemtakia Rais Mteule kila la heri.

“Hatua yangu ya kwenda mahakamani ilikuwa ishara ya imani yangu katika Mahakama. Haikuwa ni ya kisasi.  Tulijaribu kadiri ya uwezo wetu. Mawakili wetu wakiongozwa na Oraro walikusanya na kuwasilisha ushahidi mwingi.”

“Tunasikitika kwamba Mahakama ilikataa ushahidi kwa msingi kuwa uliwasilishwa kuchelewa au mahakama haikuwa na muda. Mwishowe, Wakenya walipoteza nafasi ya kujua nini kilitendeka.”

“Mimi na Kalonzo hatuna majuto kwa kuwasilisha kesi kortini. Ni matumaini yangu kwamba serikali ijayo itaheshimu Katiba na kuitekeleza. Namtakia Rais Mteule Uhuru Kenyatta na kundi lake kila la kheri. Pia, maseneta wabunge, wawakilishi wa wanawake na magavana ufanisi. Tusigawanywe na mtukio haya. Natoa wito kwa Wakenya na wafuasi wangu wakumbuke maneno ya Wimbo wa Taifa – “Haki iwe ngao na mlinzi.’”


 Sasa ni wakati wa kuijenga Kenya mpya kwa kuzika yote yaliyopita ambayo yalileta mtikisiko kama vile ukabila uliosababisha maafa kama ilivyokuwa uchaguzi Mkuu mwaka 2007. Hakika Wakenya wameonyesha ukomavu kisiasa na ndiyo maana uchaguzi huu umefanyika kwa amani na utulivu wa hali ya juu. Bravo Kenya, bravo Wakenya.
Kama alivyowahi kusema mheshimia James
Mbatia kuwa Uchaguzi wa Kenya ni mfano wa kuigwa kutokana na namna Wananchi walivyohamasika kushiriki katika zoezi la kupiga kura huku Tume ya Uchaguzi nchini humo ikionekana kujipanga ipasavyo kwa ajili ya zoezi hilo.


Tunawatakia Ndugu zetu wa Jamhuri ya watu wa Kenya kila la kheri katika kendelea kulinda demokrasia na kuhakikisha kuwa vurugu zilizotokea mwaka 2007 hazijirudii tena.  Uongozi wako Uhuru kama Rais wa awamu ya nne ukizingatia maadili ya uongozi bora utawaletea faraja wakenya wote bila kujali tofauti zao za kabila au dini.

God Bless Kenya

Friday, March 29, 2013

UJUMBE WA PASAKA 2013: TOSHEKENI NA MISHAHARA YENU:




"Sauti ya mtu imesikika jangwani: `Mtayarishieni Bwana njia yake; nyosheni mapito yake.  Kila bonde litafukiwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa; palipopindika patanyooshwa, njia mbaya zitatengenezwa.  Na, watu wote watauona wokovu utokao kwa Mungu."`

"Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mngeweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?  Basi, onyesheni kwa matendo kwamba mmetubu”.

Umati wa watu ukamwuliza, “Tufanye nini basi? Akawajibu, Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo. Nao watoza ushuru wakaja pia ili wabatizwe, wakamwuliza, Mwalimu, tufanye nini?  Naye akawaambia, Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa.  Nao askari wakamwuliza, "Na sisi tufanye nini?  Naye akawajibu, Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu."

Leo natamani kulizungumzia neon hili  Toshekeni na mishahara yenu:

Neno  hili ni zito japo lilizungumzwa kipindi kirefu nyuma lakini tunaendelea kulishuhudia leo tunapowaangalia watendaji wetu katika serikali zetu; Neno hili linatufundisha uadilifu, uwajibikaji kulingana na maadali  na kanuni za kazi ambazo zinatulazimu sisi kama watendaji wa Taifa kuweka mbele matakwa ya Taifa na sio masihahi binafsi;

Najiuliza tena  Neon hili linamaana gani kwa taifa letu? 

Kama nchi na wananchi wake tunahitajii uhuru wa kiuchumi ambao unatokana na viongozi wetu waridhike na mishahara yao; kinyume chake kama hawataridhika na mishahara yoa na kuweka mbele masilahi yao vitendo vya  rushwa na ufisadi ambao unarudisha maendeleo ya Taifa nyuma sana vitadhidi kuendelea.

 
Ujumbe wa  Pasaka ya mwaka 2013  utukumbushe sisi  Kama Taifa na kama Raia na watendaji ambao tumekula kiapo cha utii na maadili bora ya uwajibikaji kwa Taifa letu kuwapa wananchi wanyonge zawadi kubwa ya  uhuru  wa kiuchumi ili kila mmoja wetu aweze kuyafurahia  hii zawadi pekee ya rasilimali  ambayo Mungu amelijalia Taifa hakuna atayepingana nami kuwa  nchi yetu imefurika kwa uwingi wa asali na maziwa tatizo ni huluka ya kushindwa kutosheka na tukipatacho kwa watendaji wetu na kusababisha, wachache tu ambao wanafaidi rasilimali hii tuliyojaliwa na Muumba wetu. 

kwa kipindi kirefu tumeona kuwa nchi yetu  Tanzania iliyokuwa ikifurika neema  ya rasilimali sasa imegeuka; kwa wengine imekuwa ni nchi inayofurika machungu; matendo yaleyale ya kifisadi, ya ukandamizaji, ya unyanyasaji ambao  Farao aliwatendea wana wa Israeli huko misri miaka hiyo; lakini kwa kuangalia falsafa hiyo ya matendo ya Farao ndio tunaona Namna watendaji wetu walikokabidhiwa dhamana ndani ya Taifa letu  ambao sio waadilifu wananyatenda sasa yanaenda kinyume na uhuru tuliopewa kama zawadi kuto kwa Mungu ambao kila mmoja anastahili kufurahia na kufaidi asali na maziwa yanayofurika katika nchi hii. Na sio kwa kikundi kidogo cha watu.

Yohane Mbatizaji kwa usitadhi kabisa anayafafanua makundi yaliyokusanyika kwa kuwaeleza uwiano sahihi wa toba. Kulingana na Yohane matajiri wanaotakiwa kuangalia haki ya masikini, "Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo."(Lk 3,11), kwa watoza ushuru waepuke rushwa na matendo ya kifisadi "Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa."(Lk 3,13) na kwa maaskari wazingatie haki "Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo.
Toshekeni na mishahara yenu."(Lk 3,14).

Leo hii ndani ya Taifa vitendo hivi vimeshamiri tena kwa kiasi kikubwa katika jamii yetu, na pengine kila mmoja ameshiriki kwa namna moja au nyingine katika uovu huu, moja kwa moja au kwa kutokuwajibika ipasavyo katika eneo lake la kazi na hivyo kusababisha mianya katika kukua kwa matendo haya maovu. Wito wakati tusherekea Pasaka 2013 sisi kama Taifa inatupasa tubadilike na kuhakikisha haki na upendo vinashamiri katika jamii yetu.

Kama tutafanikiwa kuishi kwa ujumbe huu wa Yohani Mbatizaji kuwa tutosheke na mishahara yetu mimi naamini kuwa tukiweka mbele maslahi ya nchi, taifa letu na wananchi wake hasa wanyonge  tutasonga mbele. TUKUMBUKE KAULI YA YOHANA MBATIZAJI KWA WALE ASKARI kuhusu dhuruma:
TOSHEKENI NA MISHAHARA YENU, watu wana madaraka makubwa mishahara mikubwa na masurufu manono lakini bado wanaiibia nchi.

Hebu tujaribu kuangalia kauli ya Mheshimiwa Lusinde alidai kwamba Malipo yetu ni kidogo sana, hayatoshelezi kabisa lakini wananchi tunaowawakilisha hawatuelewi katika hili, maana wanadhani tuna fedha nyingi, sasa hapa kuna tatizo. Nadhani kuwapo utaratibu wa kuwaelimisha, wajue hata kazi nyingine tunazofanya siyo wajibu wetu ila tunajitolea na nyingine hizi zina gharama kubwa.”

Kama mwandishi mmoja alivyowahi andika kuwa “Tatizo la waheshimiwa hawa wakishapata kura wanageuka viumbe tofauti kabisa na wale waliokuwa wakijifanya wana uchungu kweli na wapiga kura wao. Wanasahau kuwa wengi wa wananchi waliowapigia kura waheshimiwa hao kuingia bungeni ni masikini wa kutupwa na hawana wa kumlalamikia (na hata wakilalamika ni kazi bure maana wawakilishi wao nao wapo ‘bize’ kulalamikia mishahara na posho)”.

Je watendaji wetu wako tayari kutoa hesabu za utendaji wao siku watakapotakiwa na Mwenyei Mungu tukiamini kuwa kazi zote hutoka kwa Mungu “Sisi tunajielewa kuwa ni watendakazi wa saa ya kumi-na-moja katika shamba la Bwana la siku za mwisho, na kwamba ingawa mishahara yetu haijulikani na mapema, lakini hatuna mashaka kwa sababu Bwana wetu ni mkarimu”.

Nafiki Pasaka hii kujifunze kitu kingine kipya kuwa “Jihadharini na tabia ya kupenda fedha, na “toshekeni na mlivyonavyo” kwa sababu Mungu mwenyewe alisema,

 “Kwa vyo vyote sitakupungukia kabisa, wala sitakutelekeza na kukuacha bila msaada. Kamwe, kamwe, sitakuacha hata kwa kiwango kidogo, kukuacha bila msaada, au kukuacha, au kukuangusha, au kulegeza mkono wangu kwako. Hakika sitafanya hivyo! Kwahiyo tunafarijika na kutiwa moyo, na kwa uhakika na ujasiri twathubutu kusema, ‘Bwana ndiye anisaidiaye” (Ebr 13:5, 6)

Kwa kutosheka na mishahara yetu na kwa kuamini kuwa sisi ni wachache ambao tumechaguliwa na Mwenyezi Mungu kuwa saidia wengine ili waweze kupata ridhiki zao; au kufurahia asali na maziwa kwa vipaji vyetu kwa kutimiza ibu wetu tutakuwa tunatekeleza ujumbe huu wa “Utafuteni kwanza ufalme wa Mungu na haki yake na hivi vitu vingine vyote mtapewa k maelefu.

Tukitenda kila kitu kwa haki kamwe hatutakosa chochote tunachohitaji  ambacho kitakuwa ziada. Mwenyezi Mungu atakupa namna ya pekee kukidhi mahitaji ya ziada.


Imani yangu ni kama ile ya Paulo kama tutatosheka na mishahara yetu,na kuwajali wanyonge katika Kupata Riziki
zao basi “Na Mungu wangu atawajazeni na kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu…”.

Tunaona mambo mengi yanaendelea ndani ya Taifa letu ikiwa na matokeo ya ubinafsi na ufisadi; tumeshuhudia 


  • matokeo mabaya ya vijana wetu ambao wamefanya mitihani ya kidato cha nne mwaka 2012; na matokeo haya yameitwa ni janga la Taifa; 

  • tunaendelea kushuhudia huduma za afya ambazo hazikidhi kiwango kwa wananchi wanyonge

  • tunaendelea kushuhudia mauaji ambayo yanaendelea ndani ya jamii yetuna mengine mengi. 

Kwa nini haya yote yanatokea jibu ni moja tu watendaji wetu hawatosheki na mishahra yao na hawan muda wa kulisaidia Taifa wako bize na shughuli binafsi ambazo ziko nje ya maadili na hata hawana muda wa kuangalia mitaala mizuri ya elimu ya vijana wetu huu ni mfano mdogo tu.

"Mungu hatakosa kuwajazi wale wote wanaoifanya kazi yake sawasawa na mapenzi yake" huu ndio ujumbe wa Pasaka 2013

Emmanuel  Turuka
Kalamazoo Michigan
madobole@gmail.com

Neno La Leo: " E Bwana , Tutakula Wapi Pasaka?"

9 57afd

Ndugu zangu,
Na ikafika siku ya mikate isiyotiwa chachu. Siku hiyo Mwana- Kondoo wa Pasaka huchinjwa. Yesu akawatuma Petro na Yohana, akawaagiza; `` E nendeni mkatuandalie chakula cha Pasaka.”

Nao wakamwuliza; ``Tukaandae wapi?''

Yesu akawajibu; ``Mtakapokuwa mnaingia mjini, mtakutana na mwanaume aliyebeba mtungi wa maji. Mfuateni huyo huyo, mpaka kwenye nyumba atakayoingia.”

“Kisha mwambieni mwenye nyumba; Mwalimu anauliza, kiko wapi chumba cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka? Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani. Chumba kilicho na fanicha zote. Fanyeni maandalizi humo.''

Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu kama Yesu alivyokuwa amewaambia. Hivyo, wakaandaa chakula cha Pasaka. Wakati ulipofika, Yesu akaketi mezani pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili. Kisha akawaambia;

``Nimetamani mno kuila Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu. Kwa maana, nawaambieni, hii ni mara yangu ya mwisho kula Pasaka mpaka maana halisi ya Pasaka itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu.''

Hapo Yesu akapokea kikombe cha divai, akashukuru akisema, ``Chukueni mnywe wote. Kwa maana, nawaambieni, tangu sasa sitakunywa tena divai hadi Ufalme wa Mungu utakapokuja.'' Alitamka Yesu.

Ni Neno La Leo.

Nawatakia nyote Pasaka Njema!
Maggid,
Iringa

Thursday, March 28, 2013

Tanzia: Mbunge Salim Hemed Hamis (CUF) amefariki dunia

 
Mbunge wa Chama Cha Wananchi (CUF) Jimbo la Chambani, Salim Hemed Khamis afariki dunia, Mbunge huyo alianguka jana ghafla akiwa katika kikao cha kamati ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa katika ofisi ndogo za bunge jijini Dar es salaam wakati kamati hiyo ikiendelea na kikao chake.

Mbunge wa Chama Cha Wananchi (CUF) Jimbo la Chambani, Salim Hemed Khamis afariki dunia, Mbunge huyo alianguka jana ghafla akiwa katika kikao cha kamati ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa katika ofisi ndogo za bunge jijini Dar es salaam wakati kamati hiyo ikiendelea na kikao chake.

Mbunge huyo ambaye siku za hivi karibuni ametoka nje ya nchi kwa matibabu ya afya yake amefikwa hali hiyo na kubebwa na baadhi ya wabunge kwa kushirikiana na baadhi ya wandishi wa habari kutolewa nje ya chumba cha mkutano na kupelekwa hospital ya taifa ya Mhimbili kwa uchunguzi na matibabu zaidi.

Mwenyekiti wa kamati ya bunge ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Edward Lowasa jana amethibitisha kutokea kwa tukio hilo la kuanguka ghalfa.

Mbunge huyo jana alikutwa na masahibu hayo jana na alikimbizwa hospitalini kwa matibabu ambako alilazwa katika chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi wa karibu (ICU).
Wajumbe wa kamati hiyo wakiongozwa na Mwenyekiti wake, Edward Lowassa, na Makamu Mwenyekiti, Mussa Hassan Zungu na baadhi ya wajumbe walimtoa nje ya ukumbi na kumpepea kwa kutumia magazeti na majarida.

Hata hivyo, hali yake ilizidi kuwa mbaya huku akizungumza kwa tabu kuwa alikunywa dawa za shinikizo la damu (BP) kabla hajala chochote na hivyo kuzidiwa.

Wabunge hao na maofisa wa Bunge, waliendelea kumpepea ili apate ahueni, lakini hali ilizidi kuwa mbaya na kushindwa kuongea kila alipoulizwa jambo.

Walimbeba na baada ya muda waliomba msaada kwa wanahabari waliokuwapo eneo hilo huku wakiwazuia wasipige picha za tukio hilo kwa maelezo kuwa si kila kitu ni habari.

Waandishi watano walisaidiana na wabunge hao kumbeba kwa kupitia mlango wa dharura na alipakizwa kwenye gari la ofisi ya Bunge lenye namba za usajili STK 2178 likiongozwa na pikipiki ya polisi yenye namba za usajili PT 2591.

Gari iliyombeba Mbunge huyo iliondoka kwenye ofisi hizo saa 5:15 asubuhi na habari zilizopatikana baadaye zilieleza kuwa alipelekwa Muhimbili kwa matibabu zaidi.

Baadhi ya wabunge walisema kuwa Khamis akiwa amekaa, ghafla alianza kutapika huku akilalamika kuwa hajisikii vizuri baada ya kunywa dawa za BP na hali yake kubadilika na walisaidiana kumtoa nje ya chumba cha mkutano.

Pamoja na wabunge hao pia, alikuwapo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi.

Waliomsindikiza hospitalini ni Mbunge wa Mpanda Mjini, Said Amour Arfi (Chadema) na Mbunge wa Gando, Khalifa Suleiman Khalifa (CUF).

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kurejea kutoka Muhimbili, Khalifa alisema Khamis alipokewa na alikuwa anaendelea kupatiwa matibabu.

Khalifa alifafanua kuwa Khamis anasumbuliwa na tatizo la shinikizo la damu.

Kwa mujibu wa gazeti la Nipashe la leo limeandika kuwa, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Edward Lowassa, alisema hali yake ilikuwa inaendelea vizuri na kuthibitisha kuwa amelazwa ICU. Lowassa alisema kuwa miezi mitatu iliyopita Khamis alikuwa India kwa matibabu. Ofisa Uhusiano wa Muhimbili, Aminiel Eligaesha, alipoulizwa kwa njia ya simu, alithibitisha kuwa mbunge huyo kupokewa hospitalini hapo na kuongeza kuwa alipatiwa matibabu na anaendelea vizuri. Hata hivyo, alisema taarifa kamili itatolewa na ofisi za Bunge.

Kaimu Katibu wa Bunge, John Joel, alisema hadi jana jioni mbunge huyo alikuwa bado ICU chini ya uangalizi wa madaktari. “Bado yuko ICU. Wanamwangalia. Presure (shinikizo la damu) iko juu, tunampumzisha kidogo,” alisema Joel akijibu swali la NIPASHE kuhusu maendeleo ya afya ya mbunge huyo. Akijibu swali iwapo kuna mpango wowote wa kumpeleka mbunge huyo kupatiwa matibabu zaidi nje ya nchi, alisema: “Tunasubiri ushauri wa madaktari.”

--Chanzo cha taarifa hii: IPP Media

Source: http://www.wavuti.com

  HABARI ZAIDI KUHUSIANA NA MAZISHI YA   MBUNGE WA CUF SALIM HEMED KHAMIS


 Baadhi ya Maofisa wa Ofisi Ndogo ya Bunge,wakimsaidia kwa kumbeba Mbunge wa Chambani,Bwa.Salim Hemed Khamis,mara baada ya kuanguka ghafla hapo jana jijini Dar akiwa katika vikao vya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na kukimbizwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu ya haraka.
--
MAZISHI ya aliyekuwa Mbunge wa CUF, Jimbo la Chambani Pemba kisiwani Zanzibar, Marehemu,  Salim Hemed Khamis,yanataraji kufanyika kesho mchana mjini Pemba.
Taarifa za awali kutoka Chama cha Wananchi CUF, zinasema kuwa Mwili wa Marehemu, Khamis utaagwa kesho asubuhi kuanzia majira ya saa 2:30-4:00  katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam ambapo Viongozi mbalimbali wa kitaifa na Kimataifa pamoja na wananchi na Wanachama wa CUF watapata fursa ya kutoa heshima za mwisho kwa Marehemu.

Taarifa hiyo ya Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julis Mtatiro inasema kuwa Msafara utaondoka Karimjee saa 4:00 kuelekea uwaja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ambapo Msafara wa Ndege 2 utaondoka kwenda Pemba.
Saa saba mchana mazishi yatafanyika huko Pemba na maazishi hayo yataongozwa na Viongozi wa serikali, Wabunge na CUF.

Mtatiro amewaomba wanachama nba wafuasi wa CUF jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kuuga mwili wa Mbunge huyo aliyefikwa na umauti akiwa kazini katika vikao vya Kamati za Bunge, ambapo Marehemu alikuwa Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

SOURCE: HAKI NGOWI

Nyerere: Wasomi wameiharibu Elimu; Wafungua shule kwa pupa; Watoa “elimu kimbizi”



 Picture
Hapa nimefuatisha kwa maneno, asilimia kubwa alichokizungumza hayati Mwalimu Nyerere katika hotuba aliyoitoa mwaka 1985 mjini Dodoma wakati akifunga Mkutano wa Chama Cha Elimu ya Watu Wazima (CHAWATA). Anasema:
Kama Taifa, tunastahili kujikumbusha tena umuhimu wa aina zetu mbalimbali za elimu, na mkazo wetu mbalimbali wa elimu.

Nilipokuwa nikizungumza na Watalalamu wa Elimu safari moja Arusha, karibuni hivi, nilijitahidi sana, kuwaomba wataalamu wetu wa elimu, waipe elimu yetu uhuru na hatua zake mbalimbali, umuhimu unaostahili. Bila hivyo tutapoteza fedha, tutapoteza wakati, tutajivunja moyo kwa sababu tunatoa mkazo katika elimu, ambao haulingani na mahitaji yetu.

Sasa hivi nchini, karibu kwa watu wote pamoja --nina hakika na wataalamu kama ninyi, wataalamu wa Elimu ya Watu Wazima-- kuna “demand” kubwa ajabu, ya elimu ya sekondari. Kubwa ajabu. Nasikia wilaya zingine wana mipango watakuwa na watafungua tatu tatu, elimu ya sekondari, na wanafurahi kabisa wenyewe wanaona wanafanya jambo la ajabu kabisa, la kufungua sekondari tatu, wengine nne, kuna mashindano ya ajabu sana. Mazuri? Mazuri!

Lakini ni mashindano ya pupa bila kufikiri.

Pupa tu. Bila kukaa na kufikiri maana yake nini. Unasema nini? Elimu hii mnayoisema hata maana yake ni nini? Na hatima yake ni nini?

Kila ukifikiri, ukikaa na kufikiria sana, ni “escapism”. Si kukabili kweli. Si kulitizama tatizo letu la Tanzania la elimu na maendeleo ukasema tunaihitaji elimu hii kwa sababu bila hii hatuna maendeleo. Si maana yake. Ni “elimu ya ukimbizi”.

Viongozi wa Serikali, wa Chama na “Professionals” hawa wa elimu, wanatuongoza katika elimu ya ukimbizi. Ya kukimbia matatizo. Si elimu ya kutatua matatizo. Hapana. Ni elimu ya kukimbia matatizo. Ni elimu ya kutukimbiza tutoke vijijini. Hawatupi elimu turudi vijijini tukae vijijini na kubadili mazingira yetu yale ambayo haturidhiki nayo, tuliyabadili kwa sababu ya elimu tuliyopata, hapana. Elimu wanayotupa ni ya kukimbia kutoka vijijini. Na hasa inayotokana kabisa na jambo la kufanya kazi kwa mkono. (Elimu) Ya kwenda ofisini.

Marehemu Karume, alikuwa ananiambia, “Lakini mwalimu, elimu hii mnayowapa vijana hawa yoooooote, ya kwenda maofisini, na tuwape meza, Mwalimu tutafuta miti Tanzania!”

Anasema mwalimu tutafuta miti, tutapata wapi meza nyingi namna hiyo? Alikuwa ana-exaggerate lakini niliwahi kumsikia Mmarekani mmoja anasema, “ exaggeration is the art of teaching.” Lakini alikuwa (Karume) ana-point.

Tunaelimisha watu kwenda maofisini. Tumeharibu kabisa mawazo ya watu wetu juu ya elimu, na viongozi wa mawazo haya ni wasomi. Viongozi wa mawazo haya ya kupotosha katika jambo la elimu ni wasomi. Anakujia mtu, “Mwalimu mwanangu ameshindwa, sasa sijui nitafanya nini.” Huyo mtoto wake anayesema ameshindwa, amemaliza elimu ya miaka saba. Taifa limejitahidi limempa elimu kijana huyu miaka saba. Anasema, mwanangu ameshindwa sasa sijui nitafanya nini. Mchukue. Nasema, “nimchukue nimpeleke wapi” Mimi nimchukue nimwingize katika kubeba wakimbizi, wanatoka Butiama. Nibebe wakimbizi kutoka Butiama, kila nikitoka Butiama nina kundi la wakimbizi. Anasema, “nenda naye Mwalimu, mpe kazi yoyote tu Mwalimu, hata ya kusafisha madirisha ofisini kwako.” Mimi nina madirisha mangapi hayo?

Nilijitahidi siku hiyo kusema na Wataalamu wa Tanzania, jamani, hivi ndivyo, elimu hii tunayoitoa, ya ukimbizi --na si Tanzania peke yake, hizi nchi zinazoitwa “third world” zote kabisa-- zenyewe “internally” kila moja ndani yake, Tanzania yenyewe ina kazi hizi za ofisini, zaidi zinafanywa mijini na vijijini kidogo kidogo, elimu ya maana zaidi kwa Tanzania wanavyoiona ndugu zetu, ni elimu inayomhamisha mtu kutoka kijijini kwenda mjini. Elimu ya “secondary”. Na kweli ni elimu ya kuhamisha tu kwa sababu kijana wetu huyu wa “secondary” akiipata elimu yake ile jinsi mlivyompa, akibaki Butiama ni “liability”. Ni “liability” kwa mama yake, kwa shangazi yake, kila mtu (kwa sababau) “he can't work”. Hakufundishwa kufanya kazi. Amefundishwa kukimbia, kwa hiyo pale kijijini anakuwa ni tatizo kubwa. Mtu amesoma miaka 11 au 12 lakini kijijini ni tatizo kabisa kwa sababu ya aina ya elimu aliyopewa.

Nilijitahidi kuwaeleza ndugu zangu, wataalamu wa elimu hapa Tanzania, elimu tunayoitaka, elimu kubwa kupita zote ni ile ambayo tumeipa jina la kweli kweli (yaani) Elimu ya Msingi. Ndiyo msingi wa elimu  yetu. Sasa msingi hauwi mbovu bwana! Msingi hauwi mbovu. Utaalamu wako na nguvu zako, kwa sababu elimu yako yote itabebwa na ule msingi. Msingi hujengwa imara kabisa. Na lazima elimu ya msingi, ijengwe imara kabisa. Maliza kwanza msingi kabla hujajenga huku juu, ama sivyo litaanguka jumba lako. Sasa wote hao wanaokazana tunataka kuongeza “secondary” ni hawa wanaotaka kujenga mapaa mazito wakati msingi hakuna. Jumba litaanguka! Wamekazana na mapaa tu, paa paa... msingi upo?

Hivi nilipokuwa nyumbani juzi nimesikitika sana, wanakuja walimu nazungumza nao, walimu wa elimu ya msingi, wananiambia, “Mzee, siyo kwamba hatuna shule, (bali) hatuna madaftari, hatuna kalamu za kutosha, nyumba za walimu hazitoshi, madarasa hayatoshi.” Mwalimu mmoja ananiambia safari hii wanafunzi wangu wa darasa la saba katika kufanya mtihani wao, imebidi kila mmoja kutoka nyumbani aje na vigoda viwili --kimoja akalie, kimoja aandikie-- na sisi waongozaji wa elimu tupo, lakini tumekazana tunataka kujenga masekondari mengine matatu,  mengine manne, mengine matano katika mkoa, lakini je, msingi tayari? Mmekamilisha msingi? Muwanyime hawa Watanzania, mamilioni, muwanyime nyie elimu yao “minimum”, mkazane na kuongeza elimu kwa watu wengine ambayo hata hatuihitaji kwa Taifa, isipokuwa ni mzazi anataka kumkimbiza mtoto wake tu, kila mmoja apate nafasi ya kumkimbiza mtoto wake.

Tukamilishe elimu ya msingi. Ndiyo elimu “number one”. Miaka saba elimu nzuri. Na miaka saba si muda mfupi hata kidogo. Kama vifaa vinatosha, walimu wanatosha, mishahara yao mizuri, mazingira yao mazuri, nyumba wanazo, miaka saba ni muda mzuri sana wa elimu. Si nchi nyingi sana zinatoa elimu ya miaka saba. Ni muda mrefu sana.

Pili baada ya hapo, ni elimu ya kuwaendeleza hawa. Bado “attention” kwa Watanzania wote. Ni elimu ya kuwawezesha kufanya kazi, siyo kukimbia kazi. Elimu ya kuwawezesha Watanzania kwa maana elimu ni ya Watanzania. Ni elimu ya Taifa. Elimu ya taifa haiwezi kuwa kwa watu wachache tu, ni kwa walio wengi. Na wote sasa wanasoma. Tungekuwa tunafikiria elimu ni kuwawezesha wananchi wetu kuandika, kusoma na kuhesabu, hii tungeifuta tu. Si ni sisi tusiojua kusoma tukishakufa si basi? Wengine wote watakaobaki watajua kusoma na kuandika na kuhesabu na sisi wengine saa 11 imefika, wengine saa 11 na nusu, kama ingekuwa “problem” ni hiyo, ninyi CHAWATA mngekuwa hamna kazi kwa maana kweli jambo la kujua kusoma, kuandika na kuhesabu linafutwa katika elimu ya msingi. Kila “generation” zinazokuja zinajua kusoma na kuandika lakini, elimu wanayoitaka ni elimu ya kufanyia kazi. Ni elimu ya ufundi na kukomaa kwa mawazo. Mawazo yanayoelekea kwenye kazi na kuendesha mazingira yetu.

Nimejitahidi kueleza. Tumejitahidi huko nyuma kusisitiza shule za ufundi. Hawataki watu wetu. Hasa ninyi wasimamizi wa elimu. Hawataki! Hawazungumzi. Hivi sasa, hivi Tanzania... michango mingi ni michango ya shule za elimu ya ukimbizi. Si elimu ya ufundi ya kuwawezesha vijana, kijana huyu mwenye elimu ambaye akiipata elimu hii, akirudi kwa mama yake, mama yake anamwona mkombozi huyu kwa sababu ana kazi anayoweza kuifanya.

Picture
Julius Kambarage Nyerere
Januari 13, 1985
Akifunga Mkutano wa Chama Che Elimu ya Watu Wazima (CHAWATA)  Dodoma

Source: http://www.wavuti.com