WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, March 2, 2013

Neno Fupi La Usiku Huu; Afrika Mama Mkwe Anapokuja Dukani Kwako....!

Ndugu zangu, Inahusu mila na tamaduni. Unafanyaje unapokuwa na duka na mteja aliye mbele yako ni mama mkwe wako?

Mwalimu, Profesa Mbele ameligusia hili la mila na destruri za Kiafrika kwenye kitabu chake kiitwacho African and Americans; Embracing Cultural Differences.

Kijinini unapokuwa na duka usifikiri tu hesabu za faida ya kibiashara, kuna hesabu za faida za kijamii pia.

Kawaida mama au baba wa mke uliyemuoa haji mwenyewe dukani kwako. Atamtuma mtu. Lakini siku ukimwona mkweo amekuja mwenyewe ujue nyumbani mambo hayajakaa sawa.

Atakutajia mahitaji yake. Atajifanya pia yuko tayari kukulipa. Lakini, unachotakiwa kufanya, ni kuchukua mahitaji yote ya mkweo. Kisha utoka kabisa nje ya duka kumkabidhi mwenyewe kwa mikono yako. Naye atajaribu kufungua mkoba wake atoe pesa. Umwombe radhi haraka, kuwa siku hiyo usingependa atoe hata senti tano!

Na usipofanya hivyo, mkwe atakuona kuwa ni mwanamme usie mwelewa wa mila na desturi.

Maana, Afrika mkwe hawezi kuja mwenyewe dukani kwako, na akija, ujue kaishiwa....Usisubiri akwambie! Ni Neno Fupi La Usiku Huu.

Maggid Mjengwa, Iringa

http://mjengwablog.co.tz

No comments:

Post a Comment