WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, October 29, 2014

Rais wa kwanza mzungu ndani ya Afrika

Guy Scott
Guy Scott ambaye alikuwa makamu wa rais Zambia wakati wa utawala wa Michael Sata ametajwa kushika nafasi ya urais wa nchi hiyo kwa sasa mpaka pale ambapo ataapishwa mara baada ya kufanyika uchaguzi mkuu wa nchi hiyo.Waziri wa ulinzi Zambia Edgar Lungu amesema maandalizi ya uchaguzi huo yataanza muda wowote ambapo katiba ya nchi hiyo inaagiza kufanyika uchaguzi wa Rais ndani ya siku 90 baada ya kufariki kwa aliyekuwa rais wa nchi hiyo.

Scott ameteuliwa kushika wadhifa huo ambapo hii itakuwa mara ya kwanza kwa rais mzungu kuongoza nchi ya Afrika tangu kuisha kwa kipindi cha ubaguzi wa rangi Afrika Kusini chini ya utawala wa FW de Klerk.
Kulikuwa na utata uliotokana na katiba ya Zambia kumruhusu Scott kushika wadhifa huo kwa sababu wazazi wake wanatokea Scottland, huku katiba hiyo ikitaja rais wa nchi hiyo ni lazima awe Mzambia kamili kwa maana ya kwamba wazazi wake wote wawili wanapaswa kuwa wamezaliwa nchini humo.
source: matukiotz.com

BREAKING NEWS: RAIS WA ZAMBIA MICHAEL SATA AMEFARIKI DUNIA


Sata, 77, had been in office since September, 2011 [AP]
Zambian President Michael Sata has died in London, where he had been receiving treatment for an undisclosed illness, three private Zambian media outlets said.
The reports on the private Muzi television station, and the Zambia Reports and Zambian Watchdog websites, said the southern African nation's cabinet was about to meet.
 Government officials gave no immediate comment.
The reports said Sata had died on Tuesday evening at London's King Edward VII hospital. The hospital declined to comment.

Sata, 77, left Zambia for medical treatment on October 19 accompanied by his wife and family members, according to a brief government statement that gave no further details.

There has been no official update on his condition and acting president Edgar Lungu had to lead celebrations last week to mark the landlocked nation's 50th anniversary of independence from Britain.
Concern over Sata's health has been mounting in the country since June, when he disappeared from the public eye without explanation and was then reported to be getting medical treatment in Israel.
He missed a scheduled speech at the UN General Assembly in September amid reports that he had fallen ill in his New York hotel.
A few days before that, he had attended the opening of parliament in Lusaka, joking: "I am not dead." Sata has not been seen in public since he returned to Zambia from New York in late September.
Sata, who once worked as a railway porter in London, had been the country's president since September, 2011 after winning a tight presidential race against the then incumbent, Rupiah Banda.

SOURCE ALJAZEERA ENGLISH

Wednesday, October 22, 2014

ANGALIA PICHA MSANII WA TMK WANAUME FAMILY, YP AZIKWA MAKABURI YA CHANG'OMBE DAR

Wasanii wa Bongo Fleva wakiuaga mwili wa marehemu Yesaya Ambikile 'YP' katika Viwanja vya TCC Chang'ombe, Dar es Salaam.


Waombolezaji wakiwa katika msiba wa msanii wa Bongo Fleva, Yesaya Ambikile 'YP' kwenye Viwanj vya TCC, Chang'ombe, Dar.…



Wasanii wa Bongo Fleva wakiuaga mwili wa marehemu Yesaya Ambikile 'YP' katika Viwanja vya TCC Chang'ombe, Dar es Salaam.

Waombolezaji wakiwa katika msiba wa msanii wa Bongo Fleva, Yesaya Ambikile 'YP' kwenye Viwanj vya TCC, Chang'ombe, Dar.
Mke wa marehemu YP, Sakina Robert (mwenye kiremba cheupe) akiwa katika hali ya majonzi.

Msanii wa Bongo Fleva, Juma Nature akizungumza jambo kwa niaba ya wasanii wenzake waliofanya kazi na marehemu enzi za uhai wake.

Baadhi ya wasanii na waombolezaji wakiwa mbele ya jeneza muda mfupi kabla ya kuuaga mwili wa marehemu.

Juma Nature akifunua jeneza tayari kwa shughuli ya kuuaga mwili huo.

Mtoto wa marehemu, Ambikile Yesaya akisogezwa mbele ye jeneza kuuaga mwili wa baba yake.

Msanii wa filamu, William Mtitu akipita kuaga mwili wa marehemu.

Msanii wa vichekesho, Mussa Kitale 'Mkude Simba' akiaga mwili.

Maombolezaji wakiwa wamebeba jeneza kwenda makaburini.

Sehemu ya mamia ya waombolezaji wakiwa makaburini.

Waombolezaji wakiwa wamebeba bango lenye picha ya marehemu.

Jeneza likishushwa kaburini.

MSANII WA TMK WANAUME FAMILY, Yesaya Ambikile 'YP' aliyefariki usiku wa kuamkia janai, amezikwa leo katika makaburi ya Chang’ombe maduka mawili jijini Dar jioni hii. Baadhi ya wasanii wa Bongo Movie waliokuwepo kuungana na wasanii wenzao wa Bongo Fleva ni pamoja na JB, Steve Nyerere, Jacqueline Wolper, Kajala Masanja, Shilole, William Mtitu, Mkude Simba na wengineo.

(PICHA: HANS MLOLI NA NASSOR GALLU/GPL)

source: matukiotz.com

Tuesday, October 21, 2014

BREAKING NEWZ: MSANII WA BONGO FLEVA Y-P AFARIKI DUNIA

http://photos-a.ak.instagram.com/hphotos-ak-xaf1/10727233_709860805766368_1533290281_n.jpg
Tasnia ya Bongo Flava imepata pigo baada ya msanii wa kundi la Wanaume Family anaefahamika kwa jina la YP kufariki jana usiku baada ya kuugua muda mrefu ugonjwa wa kifua.

Meneja wa kundi la Wanaume Family amethibisha kifo cha msanii huyo na kueleza kuwa alikuwa akisumbuliwa na maradhi hayo kwa muda mrefu.



“Tatizo alikuwa anaumwa kifua muda tu, lakini alishaanza kunywa dozi lakini majuzi akazidiwa na tukampeleka hospitali. Jana ndo mwenyezi Mungu kampenda zaidi akamchukua. Wazazi wa marehemu wapo Keko pale, lakini wazazi wake baba na mama walifariki ila ndugu zake wapo, na kuna kibanda waliachiwa na wazazi wake, kwahiyo msiba utakuwa Keko.” Fella ameiambia Bongo5.
Kuhusu ratiba ya msiba huo, Fella amesema itafahamika leo majira ya saa saba mchana.
Mungu ailaze pema roho ya marehemu YP. Amen!

source: matukiotz.com

Monday, October 20, 2014

Yanga yabadilika mara tatu


Beki wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ (aliyelala chini) akimzuia mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi wakati wa mechi ya Ligi Kuu Bara iliyochezwa juzi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Timu hizo zilitoka 0-0. Picha na Emmanuel Herman 
Dar es Salaam. Licha ya kocha mkuu wa Yanga, Marcio Maximo kubadilisha fomesheni mara tatu katika mechi dhidi ya Simba, bado malengo yake hayakutosha kuisaidia timu hiyo kuondoka na pointi tatu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam juzi.
Mechi hiyo ya Ligi Kuu ya Bara ilimalizika kwa suluhu.
Katika mechi hiyo, Maximo alianza na fomesheni ya 4-2-3-1, akimtumia Jaja kama mshambuliaji pekee akisaidiwa na Haruna Niyonzima, Mrisho Ngassa na Andrey Coutinho, kabla ya kubadilisha na kutumia 4-4-2 iliyomuhusisha Ngassa na Jaja kama washambuliaji wawili na kisha kutumia 4-3-3 baada ya kuwaingiza Simon Msuva na Hamisi Kiiza kusaidiana na Ngassa katika mashambulizi.
Maximo alisema alilazimika kubadilisha fomesheni aliyoanza nayo kutokana na aina ya uchezaji wa wapinzani wao.
“Simba walitumia mabeki wanne na kiungo mkabaji mmoja juu ya mabeki hao, ikawa ngumu kwa wachezaji wangu kushambulia. Nikabadili fomesheni na kutumia 4-4-2 ambayo pia haikunisaidia kupata bao,” alisema Maximo.
Anasema fomesheni ya mwisho aliyotumia ni ile ya 4-3-3 ili kuongeza nguvu ya mashambulizi na kukaba katikati ya uwanja.
“Vijana wangu walitaka kufunga ila fomesheni waliyoitumia Simba, walikuwa na wachezaji wengi katikati na katika safu ya ulinzi, halafu walikuwa wakipiga pasi fupi na ndefu,” alisema Maximo.
Alisema: “Mabeki wa Simba walikaba wawili wawili, hawakumuacha mshambuliaji wa Yanga na beki mmoja, ila ni mara tatu tu ndiyo beki ya Simba ilitoa nafasi kwa washambuliaji wa Yanga, lakini nafasi hizo tulishindwa kuzitumia, Coutinho alipata nafasi mbili, Jaja alipata nafasi moja.”
Kocha wa Simba, Patrick Phiri alisema alitumia fomesheni ya 3-5-2 japo nafasi ya kiungo ilipwaya baada ya Jonas Mkude kuumia na kuingia Pierre Kwizera.
“Mkude alipotoka timu ilibadilika, ilipwaya katikati. Mkude ana uwezo wa kuchukua mipira na kuchezesha timu, pia anakaba, kuumia kwake ilikuwa pengo hata hivyo, timu ilicheza vizuri, lakini bado sijafurahia kiwango chake kwa kuwa hii ni sare ya nne,”alisema Phiri.
Wakati huo huo, JKT Ruvu imeichapa Tanzania Prisons 2-1 katika mechi ya Ligi Kuu iliyochezwa jana kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya. Pia katika Ligi daraja la kwanza JKT Oljoro imetoka sare 1-1 na Mwadui kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha. Hata hivyo zilitokea vurugu mashabiki wakipinga mpira wa faulo ulioipatia Mwadui bao la kusawazisha.
(Imeandaliwa na Imani Makongoro, Bertha Ismail na Godfrey Kahango).
source: mwananchi

TAZAMA PICHA ZA MTANANGE WA WATANI WA JADI YANGA NA SIMBA ULIYOCHEZWA KWENYE UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR ES SALAAM


 Jaja hakuweza fua dafu...

Mtanange ukiendelea...
 
Kiungo wa timu ya Simba,Amri Kiemba akuchuana vikali na Mshambuliaji wa timu ya Yanga,Andrey Coutinho wakati wa mtanange wa watani wa Jadi Yanga na Simba uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana  ikiwa ni sehemu ya muendelezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.Timu hizo zimetoka sare ya bila kufungana.


 Dogo akiwachambua wana Yanga...

 
Shabiki wa Simba akionyesha bango linaloonyesha michezo iliyopita waliowahi kucheza na Yanga na kushinda



 Mashabiki wa Simba

 Mashabiki wa  Yanga Wakifanya Yao

kipa wa timu ya Simba, Manyika Peter (kushoto) akipongezwa na kipa wa Yanga, Deogratius Munishi baada ya kumalizika kwa  mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania  uliochezwa katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jana. timu zote zimetoka sare ya bila kufungana. katika michezo mingine iliyochezwa katika viwanja tofauti, Azam FC wameweza kuwafunga, Mbeya City bao 1-0 lililofungwa katika daki ya 18 ya mchezo na Agrrey Moris, mchezo huo ulichezwa katika Uwanja wa Sokonne jijini Mbeya na huko Mtwara katika Uwanja wa Nangwanda, JKT RUVU wameweza kwafunga wenyeji timu ya Ndanda FC bao 3-1 na katika mchezo mwingine uliochezwa katika Uwanja wa Jamhuri mjini Kasoro Bahari mkoani Morogoro kati ya Mtibwa Sugar na Polisi Morogoro, timu hizo zimetoka suru bin suru, Coast Union nayo imeibuka na ushindi wa bao 2-0 dhidi ya Mgambo

 
Kipa wa Siba, Manyika Peter akipongezwa na mashabiki wa timu hiyo baada ya mchezo kumalizika.

 Kocha Mkuu wa Yanga, Marcio Maximo, akiwasalimia mashabiki wa timu hiyo

Makocha wa yanga na Simba, Maximo (kushoto)akisalimiana na Patrick Phili kabla ya mchezo.

PICHA NA OTHMAN MICHUZI NA ANTHONY SIAME

source: haki Ngowi

Monday, October 13, 2014

LEO NI SIKU YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE - 1922 - 1999


  • TUTAENDELEA KUENZI DAIMA MAZURI YOTE ALIYOTUACHIA;



"Inawezekana tatizo la paka kwa panya lingekwisha kama paka angefungiwa kengele shingoni: taabu ni kumpata panya wa kuifanya kazi hiyo. Na panya watakuwa wajinga sana wakidhani kuwa paka watajifunga au watafungana kengele shingoni"


"Hakuna umaskini mbaya kama umaskini wa mawazo, ni umaskini mbaya sana"

'Mtu mwenye akili akikuambia neno la kipumbavu -ukalikubali, anakudharau!'

Tutawasha Mwenge na kuuweka juu ya Mlima Kilimanjaro, umulike mpaka nje ya mipaka yetu, ulete matumaini pale pasipo na matumaini, upendo pale palipojawa na chuki na heshima pale palipojaa dharau –


"tunataka kiongozi ambaye anachukia rushwa, na hata tukimwangalia usoni tunaamini anachukia rushwa, Sio ambaye hata ukimuangalia unajiuliza, mnh, huyuu????!" 


“TUNAPOZUNGUMZA habari za uhuru maana yetu nini hasa? Kwanza; kuna uhuru wa nchi,yaani uwezo wa wananchi wa Tanzania kujipangia maisha yao, wakijitawala wenyewe bila ya kuingiliwa kati na mtu yeyote asiyekuwa Mtanzania. Pili; kuna uhuru wa kutosumbuliwa na njaa, maradhi na umasikini. Tatu, kuna uhuru wa mtu binafsi, yaani haki yake ya kuishi, akiheshimika sawa na wengine wote, uhuru wake wa kusema na uhuru wake wa kushiriki katika uamuzi wa mambo yote yanayogusa maisha yake, na uhuru wa kutokamatwa ovyo na kutiwa ndani kwa kuwa tu kamuudhi mkubwa, japo kama hakuvunja sheria yoyote”.



“Lakini ni dhahiri kwamba mambo hayo yanategemea maendeleo ya uchumi, madhali nchi yetu bado masikini; na wananchi hawakupata elimu; na ni wajinga na wanyonge, basi uhuru wetu wa kujitawala unaweza kuhatarishwa na taifa lolote la kigeni lenye maendeleo na nguvu zaidi.”

...."Kiongozi anayetufaa Tanzania , ni yule anayejua kuwa nchi yetu ni masikini na watu wake ni masikini. Na ukimwangalia usoni ...uone anaguswa na umasikini wetu. Vinginevyo hatufai...."

“Kwa sasa uhuru wa taifa letu, mara nyingi ni uhuru wa maandishi tu; maana nchi yetu ni maskini mno, ni nyonge mno kulinganisha na nchi nyingine, hata hatuwezi kutimiza wajibu wetu kwa ukamilifu kwa binadamu wengine”.  

“Watu wenye mawazo tofauti, hata wakiwa wachache, lazima wawe na haki ya kutoa mawazo yao katika majadiliano bila ya hofu ya kusumbuliwa; mawazo yao na yashindwe katika hoja za majadiliano, siyo kwa vitisho au mabavu. Majadiliano yenyewe yatakayoleta uamuzi lazima yawape nafasi watu kusema kwa uhuru kabisa.  Hata baada ya kuamua jambo, watu wawe na uhuru kuendelea kulizungumza jambo hilo”




“Elimu inayotolewa ni lazima ijenge mambo matatu kwa kila mwananchi, akili ya kuuliza, uwezo wa kujifunza kutoka kwa wengine - na kuyakataa au kuyakubali kutokana na mahitaji yake - na uwezo wa kujiamini kama raia huru na sawa katika jamii, anayethamini wengine na kuthaminiwa kwa anayofanya na siyo kwa anachopata” 

Thursday, October 9, 2014

NINI HASARA YA DEMOKRASIA MATAYARISHO YA KATIBA MPYA JAMUHURI YA MUUNGANO TANZANIA?


Demokrasia imefafanuliwa katika namna mbalimbali; wengi wa wanazuoni wameeleza  kuwa “Demokrasia ni mfumo wa utawala ambao watu huwachagua  viongozi wa serikali yao wenyewe na kuainisha jinsi inavyopaswa kufanya kazi”. Wakaendelea kukufafanua kuwa “ Demokrasia hukuza ustawi wa watu wote kwani Kila raia ana haki ya kushiriki katika uendeshaji wa shughuli za umma na katika mambo yote yanayoathiri maisha yake”.wengi wa wanazuoni wanakubalia kuwa Demokrasia inauwezo mkubwa wa kushugulikia  uwajibishaji serikali kupitia kura za maoni  na maamuzi yanayofanywa na wawakilishi wao katika vyombo mbalimbali vya maamuzi”.



Kwa maneno mengine Demokrasia ni  mkataba wa kijamii kati ya wananchi na watawala(serikali); mkataba huu ni wa pande mbili raia wana wajibu wa kutekeleza sehemu yao na serikali pia inawajibu wa kuwatendea raia matakwa yao. Kwa maneno mengine ni mkataba wa kijamii unadhihirisha uaminifu na matumaini ambayo raia  wanakuwa nayo kwa wawakilishi wao ili watende kwa niaba yao.na pale wanaposhindwa kufanya majukumu ambayo jamii iliyowachagua imewapa wananchi wanayo nafasi ya kuwachagua wawakilishi wengine.


Swali la msingi chimbuko la demokrasia ni nini?

Tunafahamu kuwa lengo kubwa la demokrasia ni kuleta mabadiliko kwa wananchi wake, ili kuwaletea maisha mazuri, kuwatoa  kwenye dimwi la umasikini na kuwaletea maisha bora kwa jamii nzima na sio kikundi kidogo cha watu; kwa msingi huu ukifuatwa vizuri na kutekeleza kwa ufanisi ni ukweli usiopingika kwamba mfumo wa utawala wa kidemokrasia una umuhimu wake katika  maendeleo ya jamii nzima.

Je demokrasia inatumika wakati wote?

Hili ni swali lenye changamoto kubwa; lakini ni lazima ieleweke na tujiulize kuwa  ni wakati gani demokrasia inapaswa kutumika na wakati gani siyo muhimu kuitumia; Nasema hivyo kwa sababu siyo wakati wote ni muhimu ama lazima kutumia mfumo wa demokrasia umaohusisha maamuzi ya wengi, ndani ya  uendeshaji wa serikali na maamuzi yake; mfano mzuri ni uamuzi ambao uliwahi tolewa Mheshimiwa Raisi Kikwete baada ya kukutana na wawakilishi wa vyama vya siasa na kukubaliana kuwa mchakato wa kupata katiba mpya utakao husisha maoni ya wananchi utaendelea baada ya uchaguzi ujao.  Uamuzi huu umekuwa tofauti na uamuzi wa awali kuwa Katiba mpya itapatikana kabla ya uchaguzi 2015.

Je msingi wa demokrasia ni nini?

Msingi wa demokrasia inawapendelea sana walio wengi kwa kukubali mawazo ya wengi. Usahihi wa hoja mara nyingi sio jambo muhimu kuliko wingi wa ufuasi. Walio wengi katika kufikia muafaka wa jambo kulingana na demokrasia ndio washindi wa demokrasia hata kama hawana hoja

Je hasara ya demokrasia ni nini?
Demokrasia inaangalia uwingi wa wawakilishi na sio lazima hoja zinazotolewa, hata kama hoja hazina mantiki lakini zina ungwa mkono na wengi zinafanyiwa maamuzi na hatimaye yanaonekana kuwa sahihi.

Hasara hii ya demokrasia tunaweza kulinganisha na mwenendo wa upatikanaji wa katiba mpya ambao umekamilika huko Dodoma hivi karibuni.
kinachoangaliwa katika kufikia upatikaji wa katiba mpya umekuwa ni wa wawakilishi ndani ya bunge la Katiba, kwa mfano katika nchi yetu ya Tanzania “Chama cha Mapinduzi (CCM) kina wajumbe wengi katika Bunge la Katiba kwa hiyo  Msingi wa wingi wao ni ushindi walioupata katika uchaguzi halali wa kisheria na kidemokrasia”

 
Kutokana na mazingira haya, mjadala wa upande mmoja uliokuwa unaendelea bungeni ulikuwa halali, hata kama UKAWA waliamua vikao vya bunge hilo. Walichofanya UKAWA ni mbembwe za siasa za kususia ili pengine kupata huruma ya wananchi lakini kimsingi walitakiwa kuendelee kujenga hoja ili kuwafanya walio wengi wabadilishe mawazo yao na wananchi weelewe msingi wao wa hapana ni nini.

Naamini kuwa UKAWA walikuwa na hoja walitakiwa kufa kiume katika ushindani wa hoja Bungeni;  kwa maneno menginehii ndio demokrasia ya ushindani iliyoletwa kwetu na warumi na tukaikubali na kuona ni chombo sahihi cha maamuzi. Ndio hasara ya demokrasia lakini kwa kuwaachia wenzao uwanja wamewanyima wananchi ushindani wa hoja za pande mbili.

Hata kama UKAWA watafanya mikutano ya kupinga katiba nje ya vikao halali vya Bunge inakuwa ni hadithi, ni simulizi ya upande mmoja ambao hauna usindani.

Ushindani wa hoja kati ya wanasiasa na kati ya vyama vya siasa inatakiwa ieleweke kama ustawi wa jamii husika. Kwa kuwa tofauti ya hoja haitakiwi ilete  utengano na hatimaye migongano, bali iwe ni sehemu ya kuleta maendeleo ndani ya jamii husika; kwani demokrasia ya ushindani itakayo ishia katika kuleta vurugu na ugomvi ndani ya jamii itaathiri maendeleo ya jamii na kuongeza maisha magumu kwa jamii husika hivyo kubadilisha mfumo huu na kuingia katika mfumo wa kikatili

 

Utawala wa demokrasia unatakiwa utufundishe namna ya kupanua fikra za wawakilishi wetu. Demokrasia inatakiwa iwe mkombozi wa fikra na kuwapa wananchi uhuru wa kufikiri, uhuru wa kutenda na hata wa kwenda kinyume na fikra za kikale. Ili jamii iweze kuendelea na iwe na demokrasia iliyopevuka ni muhimu wananchi wawe na uhuru wa kuweza kuasi kisiasa na kuwa na fikra zisizofuata mkondo wa fikra za kawaida za wanajamii.

 

Tofauti za hoja baina ya wafuasi wa vyama tofauti  ndani ya mfumo wa demokrasia huzaa chuki ambayo inajengwa kati ya watawala na wapinzani dhidi ya wananchi kila upende ukijaribu kushinda  hisia za wananchi ambao ndio wenye nchi. Ni wajibu wa wananchi kuamka  na kuwa  imara na kukataa mbwebwe za wanasiasa.

 Tunatakiwa kuanza kuhoji mambo ambayo tunaona kuwa sio ya kweli. Inafurahisha kwa sasa ndani ya Tanzania  kuwa mwamko wa wananchi wetu kwa sasa umebadilika na wananchi wameanza kuonyesha dalili ya kuelewa Zaidi nini wanataka hasa kuhusiana na maendeleo yao.
 

Tukiweza kuepukana na itikadi za matukio  na polojo za matukio na udaku: Lazima tukubali kuwa kila chama cha siasa Tanzania tupende au tusipende kina uzuri wake na ubaya wake, lakini la msingi katika mantiki ya demokrasi lazima tukubali kuwa chama ambacho kimefanikiwa kuingia mkataba wa hiari na wananchi wa kuongoza nchi ndicho kimefanikiwa kupata ridhaa ya kuongoza ndipo tunapona hasara ya demokraisa pengine matendo yao hayakubaliki na wachache ambao wanafikiri kuwa nao wana mwelekeo tofauti na wenye tija kwa jamii. Kwa msingi huo ni kuwa  tofauti za siasa na wanasiasa katika jamii haziwezi kuepukika na wakati mwingine unyama wao unaotokana na tofauti zao za kutamani kuhodhi madaraka unapelekea kuiangamiza  jamii ambayo haina kosa kutokana tu na uelewa wao mdogo;


Napenda katika hitimisho la Makala yangu nimshukuru sana Mheshimiwa Raisi Kikwete na Mheshimiwa Ally Mohamed Shein wamekuwa wasikivu, wavumilivu  na walezi wa demokrasia ya kweli kwa  kuendelea kuvishirikisha vyama na asisi zote ambazo zimefika mahala na kukinzana na serikali zetu zote mbili ili kufikia muafaka kwa kusikiliza mawazo ya wachache bila  kinyongo na hata wakati mwingine kubadilisha  msimamo wa wengi na kufuata mawazo ya wachache.
 

Hapa tunaona  Sifa mojawapo ya demokrasia ya kweli ni kwamba: inawapatia wachache VILEVILE nafasi ya kisheria ya kuwashawishi wengi waone ubora wa maoni yao hata kama hawakubaliani nayo. Demokrasia ya namna hii ndiyo njia pekee ya kuleta mawazo mapya katika jamii kwa njia ya amani na utulivu. Hii ndio sifu kubwa ya viongozi wa serikali zetu Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete na Dr. Mohamed Ally Shein

Lazima tukubali kuwa demokrasia in faida na hasara yake na kamwe sio kila mtu ataridhika na maamuzi ambayo yataendelea kutolewa katika uwajibikaji wa pamoja.

 

Mungu Ibariki Tanzania