WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Tuesday, October 21, 2014

BREAKING NEWZ: MSANII WA BONGO FLEVA Y-P AFARIKI DUNIA

http://photos-a.ak.instagram.com/hphotos-ak-xaf1/10727233_709860805766368_1533290281_n.jpg
Tasnia ya Bongo Flava imepata pigo baada ya msanii wa kundi la Wanaume Family anaefahamika kwa jina la YP kufariki jana usiku baada ya kuugua muda mrefu ugonjwa wa kifua.

Meneja wa kundi la Wanaume Family amethibisha kifo cha msanii huyo na kueleza kuwa alikuwa akisumbuliwa na maradhi hayo kwa muda mrefu.



“Tatizo alikuwa anaumwa kifua muda tu, lakini alishaanza kunywa dozi lakini majuzi akazidiwa na tukampeleka hospitali. Jana ndo mwenyezi Mungu kampenda zaidi akamchukua. Wazazi wa marehemu wapo Keko pale, lakini wazazi wake baba na mama walifariki ila ndugu zake wapo, na kuna kibanda waliachiwa na wazazi wake, kwahiyo msiba utakuwa Keko.” Fella ameiambia Bongo5.
Kuhusu ratiba ya msiba huo, Fella amesema itafahamika leo majira ya saa saba mchana.
Mungu ailaze pema roho ya marehemu YP. Amen!

source: matukiotz.com

No comments:

Post a Comment