WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, October 13, 2014

LEO NI SIKU YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE - 1922 - 1999


  • TUTAENDELEA KUENZI DAIMA MAZURI YOTE ALIYOTUACHIA;



"Inawezekana tatizo la paka kwa panya lingekwisha kama paka angefungiwa kengele shingoni: taabu ni kumpata panya wa kuifanya kazi hiyo. Na panya watakuwa wajinga sana wakidhani kuwa paka watajifunga au watafungana kengele shingoni"


"Hakuna umaskini mbaya kama umaskini wa mawazo, ni umaskini mbaya sana"

'Mtu mwenye akili akikuambia neno la kipumbavu -ukalikubali, anakudharau!'

Tutawasha Mwenge na kuuweka juu ya Mlima Kilimanjaro, umulike mpaka nje ya mipaka yetu, ulete matumaini pale pasipo na matumaini, upendo pale palipojawa na chuki na heshima pale palipojaa dharau –


"tunataka kiongozi ambaye anachukia rushwa, na hata tukimwangalia usoni tunaamini anachukia rushwa, Sio ambaye hata ukimuangalia unajiuliza, mnh, huyuu????!" 


“TUNAPOZUNGUMZA habari za uhuru maana yetu nini hasa? Kwanza; kuna uhuru wa nchi,yaani uwezo wa wananchi wa Tanzania kujipangia maisha yao, wakijitawala wenyewe bila ya kuingiliwa kati na mtu yeyote asiyekuwa Mtanzania. Pili; kuna uhuru wa kutosumbuliwa na njaa, maradhi na umasikini. Tatu, kuna uhuru wa mtu binafsi, yaani haki yake ya kuishi, akiheshimika sawa na wengine wote, uhuru wake wa kusema na uhuru wake wa kushiriki katika uamuzi wa mambo yote yanayogusa maisha yake, na uhuru wa kutokamatwa ovyo na kutiwa ndani kwa kuwa tu kamuudhi mkubwa, japo kama hakuvunja sheria yoyote”.



“Lakini ni dhahiri kwamba mambo hayo yanategemea maendeleo ya uchumi, madhali nchi yetu bado masikini; na wananchi hawakupata elimu; na ni wajinga na wanyonge, basi uhuru wetu wa kujitawala unaweza kuhatarishwa na taifa lolote la kigeni lenye maendeleo na nguvu zaidi.”

...."Kiongozi anayetufaa Tanzania , ni yule anayejua kuwa nchi yetu ni masikini na watu wake ni masikini. Na ukimwangalia usoni ...uone anaguswa na umasikini wetu. Vinginevyo hatufai...."

“Kwa sasa uhuru wa taifa letu, mara nyingi ni uhuru wa maandishi tu; maana nchi yetu ni maskini mno, ni nyonge mno kulinganisha na nchi nyingine, hata hatuwezi kutimiza wajibu wetu kwa ukamilifu kwa binadamu wengine”.  

“Watu wenye mawazo tofauti, hata wakiwa wachache, lazima wawe na haki ya kutoa mawazo yao katika majadiliano bila ya hofu ya kusumbuliwa; mawazo yao na yashindwe katika hoja za majadiliano, siyo kwa vitisho au mabavu. Majadiliano yenyewe yatakayoleta uamuzi lazima yawape nafasi watu kusema kwa uhuru kabisa.  Hata baada ya kuamua jambo, watu wawe na uhuru kuendelea kulizungumza jambo hilo”




“Elimu inayotolewa ni lazima ijenge mambo matatu kwa kila mwananchi, akili ya kuuliza, uwezo wa kujifunza kutoka kwa wengine - na kuyakataa au kuyakubali kutokana na mahitaji yake - na uwezo wa kujiamini kama raia huru na sawa katika jamii, anayethamini wengine na kuthaminiwa kwa anayofanya na siyo kwa anachopata” 

No comments:

Post a Comment