WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Thursday, October 9, 2014

RAIS KENYATTA APOKEWA KWA SHANGWE NAIROBI



Makundi ya watu wanaoshangilia, yamempokea Rais Uhuru Kenyatta ambaye amerejea Kenya baada ya kuhudhuria Mahakama ya Kimataifa ICC, iliyopo The Hague.


Bwana Kenyatta alihudhuria shauri mahakamani siku ya Jumatano, na kuwa rais wa kwanza aliyepo madarakani kufika katika mahakama ya ICC.


Anakanusha mashtaka dhidi yake ya uhalifu dhidi ya ubinaadam kuhusiana na ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka 2007, zilizosababisha vifo vya watu 1,200 na wengine 600,000 kupoteza makazi.

Rais Kenyatta alipokelewa Nairobi kwa gwaride la heshima na ngoma.


Picha: Bw Kenyatta akiwa na mmoja wa mawakili wake wa utetezi ICC
source: matukiotz.com

No comments:

Post a Comment