WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, May 31, 2014

PETER MUTHARIKA NDIE RAIS MTEULE MALAWI


Peter Muthirika anayeongoza chama cha DPP ndiye rais mteule nchini Malawi
Hatimaye Malawi imepata Rais mpya baada ya mivutano ya kisheria kwa wiki nzima.

Mwandishi wa BBC Baruan Muhuza amesema kutoka mjini Blantyre kuwa Profesa Peter Mutharika 
ameshinda uchaguzi huo kwa kupata asilimia 36.4 ya kura zote akifuatiwa na Dr Lazarus Chakwera mwenye asilimia 27.8 huku Rais anayemaliza muda wake Dr Joyce Banda akishika nafasi ya tatu kwa asilimia 20.2 na Atupele Muluzi amekuwa wa nne na asilimia 13.7

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Jaji Mackson Mbendera amesema uchaguzi huo ulikumbwa na changamoto nyingi lakini mwishowe nchi ni lazima ipate kiongozi wake na kuwaomba wananchi kuwa na utulivu .

Kesi Mahakamani
Awali Jaji Kenyata Nyirenda wa mahakama kuu mjini humo jana usiku alitoa uamuzi kuwa hawezi kuvunja sheria kwa kuruhusu tume iongeze muda wa 
kuhesabu upya kura kwenye maeneo yenye utata.
Na kwamba sheria inaitaka tume kutangaza matokeo ndani ya siku nane na si vinginevyo.

Uchaguzi wa Malawi ulifanyika Mei 20 nchini kote lakini siku moja tu baada ya kupiga kura, malalamiko yakiambatana na mapingamizi ya kisheria yakatawala kwenye mahakama kuu za Lilongwe na Blantyre.

(P.T) Chanzo:BBC

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOANI DODOMA KUHUSU CHANZO CHA AJALI ILIYOPELEKEA KIFO CHA DIRECTOR GEORGE TYSON



Na. Sylvester Onesmo wa Jeshi la Polisi.
Watu wawili wamepoteza maisha kutokana na ajali mbili zilizotokea  katika maeneo mawili tofauti na nyakati tofauti Mkoani Dodoma.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME – SACP ameeleza kuwa, ajali ya kwanza ilitokea tarehe 30/05/2014 majira ya saa 18:30hrs katika kijiji cha Ipala Wilaya ya Dodoma ambapo gari lenye namba za usajili DFP 614 Toyota Land Cruiser mali ya chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo likitokea chuoni kuelekea Dodoma mjini likiendeshwa na ALFRED S/O MLIGO, MIAKA 35, MHEHE, liliacha njia na kupinduka na kusababisha kifo chake.  Pia watu watano walipata maumivu mbalimbali na walitibiwa na kuruhusiwa. 

Mwili wa marehemu upo katika Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Dodoma kusubiri taratibu nyingine.
Kamanda MISIME AMESEMA ajali ya pili imetokea majira ya saa 18:45hrs huko katika kijiji cha SILWA barabara ya Dodoma – Morogoro ambapo gari lenye namba za usajili T.150 CWA Toyota Granvia Station Wagon likiendeshwa na MGENI S/O SHEMAKAME, MBONDEI, MIAKA 29 MKAZI WA MBURAHATI DSM liliacha njia na kusababisha kifo cha GEORGE S/O TYSON, MIAKA 39, MWONGOZAJI WA FILAMU, Mkazi wa mbezi DSM. 


Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Gairo ukisubiri taratibu za Polisi na wanandugu.  

Pia katika ajali hiyo wanahabari wanne (4) wa Mboni show walipata majeraha mbalimbali na kutibiwa na kuruhusiwa, ambao ni:-

1.   NIXON S/O KABUMBILE, MHAYA, MIAKA 31
2.   GRACE D/O MEENA, MCHAGA, MIAKA 28
3.   NTWA S/O KABOLE, MNYAKYUSA, MIAKA 33
4.   JUSTINE S/O BAYO, MIAKA 27, MMASAI

Uchunguzi wa awali unaonyesha ajali zote mbili zimesababishwa na mwendokasi. 

Kamanda MISIME ametoa wito kwa madereva kuepuka mwendokasi na kuwa na udereva wa kujihami ambao unasaidia dereva kusimama bila kusababisha madhara linapotokea jambo lolote na hata kama ajali ikitokea madhara hayawezi kuwa makubwa kama yanavyokuwa anapokuwa kwenye mwendo wa kasi


CHANZO: MATUKIOTZ.COM

PIGO NYINGINE BONGO MOVIE:GEORGE TYSON AFARIKI DUNIA


George Tyson enzi za uhai wake.
George Tyson akimlisha keki Yvonney Chery ‘Monalisa’ wakati mtoto wao Sonia alipopata kipaimara.
NI pigo tena kwa tasnia ya Bongo Muvi, mwongozi filamu Bongo na aliyekuwa mume wa staa wa filamu za Kibongo, Yvonny Cherry 'Monalisa', George Tyson amefariki dunia baada ya kupata ajali mbaya ya gari maeneo ya Gairo, Morogoro akitokea mkoani Dodoma. Tyson alikuwa ameambatana na watu kadhaa katika safari hiyo ambao wanadaiwa kuumia vibaya. Mwili wa marehemu Tyson pamoja na majeruhi wa ajali hiyo wamepelekwa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro. Tyson enzi za penzi lake na Monalisa walifanikiwa kupata mtoto aitwaye Sonia.
Marehemu Tyson akiwa na Monalisa (kushoto), kulia ni Tyson na mwanae Sonia.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Monalisa amemlilia Tyson kwa kuweka picha hiyo juu na kuandika maneno yafuatayo:
Monalisa akimnywesha kinywaji Tyson wakati wa kipaimara cha Sonia.
MUNGU AIPUMZISHE ROHO YA MPENDWA WETU MAHALI PEMA PEPONI. AMEN!


GARI ALILOPATA NALO AJALI DIRECTOR GEORGE TYSON

Muonekano wa Gari alilopata nalo ajali Director George Tyson.
Kwenye hii safari, George Tyson (kulia) aliambatana na mtangazaji Mboni Masimba wa The Mboni show.
DJ Choka (kushoto), akiwa na marehemu George Tyson (kulia) wakiwa Dodoma enzi za uhai wake.
Marehemu George Tyson enzi za uhai wake.
Dj Choka ambae alikua kwenye safari moja ya Dodoma na Marehemu George Tyson, ameandika kwamba Marehemu alikuwa yupo kijiji cha Chilonwa Chamwino kwenye utoaji wa madawati katika shule ya msingi Chaula iliyopo Dodoma.
Baada ya kumaliza shughuli hii huku akiwa kama producer wa The Mboni Show mauti yalimkuta majira ya saa 12 jioni ikiwa ni saa 4 tu toka tuanze safari ya kurudi Dar es Salaam maeneo fulani hivi kama unataka kukaribia GAIRO mjini.
Kwenye gari walikuwa watu 8 ila yeye pekee ndio aliyepoteza maisha ila wengine wamepata majeraha mwilini akiwemo dereva wa gari hilo ambapo kwa sasa mwili wa marehemu umehifadhiwa hapa Morogoro katika hospital ya mkoa Morogoro baadae asubuhi safari ya kurudi Dar es Salaam itaanza.
PICHA/HABARI KWA HISANI YA DJ CHOKA

SOURCE: GLOBAL PUBLISHER

Thursday, May 29, 2014

RACHEL HAULE AMETANGULIA MBELE YA HAKI ALILIWA NA WENGI


Msanii wa Bongo Movie, Rachel Haule 'Recho' (pichani), amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es slaaam. Habari zilizotua Global na kuthibitishwa na Mwenyekiti wa Bongo Movie, Steve Nyerere, zimesema kuwa Recho alikwenda Muhimbili jana kujifungua ambapo mara baada ya kujifungua mtoto alifariki na yeye hali yake kuwa mbaya, ilibidi ahamishiwe ICU ambako hali ilizidi kuwa mbaya na baadae kufariki dunia.
Kifo cha Recho kimekuja ndani ya wiki moja baada ya kufariki kwa msanii mwingine wa Bongo Movi Adam Kuambiana Jumamosi iliyopita, kifo hiki kimeleta mstuko mkubwa kwenye tasnia ya ya filamu za kibongo. Habari na picha zaidi zitawajia baadae.
 PICHA: Makatab za GPL

MWILI WA RACHEL HAULE WAAGWA , IRENE UWOYA AZIMIA. PICHA HIZI HAPA

Mwili wa muigizaji wa filamu nchini Rachel Haule umeagwa leo hii katika viwanja vya Leaders na baada ya hapo atazikwa katika makaburi ya Kinondoni. Wasanii wengi ndugu, jamaa na marafiki wamejawa katika simanzi kubwa huku Irene Uwoya akizimia pengine kwa mshituko wa kuondokewa na msanii mwenzao. Angalia picha zikionyesha matukio ya mwili wa Rachel tangu akitolewa Muhimbili, kupelekwa Sinza na Leaders..........

Irene Uwoya akiwa amezimia 

RACHEL HAULE AZIKWA LEO KATIKA MAKABURI YA KINONDONI

 Aunt Ezekiel na Wema Sepetu wakiwa makaburini.
 Mchumba wa Marehemu Rachel, Saguda (katikati) akiwa na majonzi tele wakati wa mazishi ya mchumba wake
 Majeneza yenye mwili wa marehemu Rachel na Mwanae yakiletwa Katika makaburi ya Kinondoni leo
 Mchungaji akiendesha sala ya kusalia Miili ya Marehemu Rachel na Mwanae katika Makaburi ya Kinondoni
 Majeneza Yakiweka katika kaburi 
 Waombolezaji wakiweka mchanga katika kaburi la Marehemu Rachel
 Bibi Wa Marehemu akiweka mchanga katika kaburi ya Mtoto wa Marehemu Rachel aliyefariki wakati akijifungua
 Mchumba wa Marehemu akiweka mchanga katika kaburi la Mchumba wake, Marehemu Rachel
 
Mwakilishi wa Kampuni ya Proin Promotions akiweka Shada la Maua wakati wa mazishi ya Marehemu Rachel Haule na mwanae yaliyofanyika katika Makaburi ya Kinondoni.
 Mwenyekiti wa Bongo Movie akiweka Shada la Maua katika kaburi la Rachel
Mchungaji akiweka Shada la Maua katika kaburi la Marehemu Rachel Haule

Tuesday, May 20, 2014

ANGALIA PICHA MAELFU WAMZIKA ADAM KUAMBIANA KINONDONI DAR


Mashada yakiwa tayari juu ya kaburi la marehemu Adam Philip Kuambiana, muda mfupi baada ya shughuli za maziko kukamilika.
Jacob Steven 'JB', akiweka shada kwenye kaburi. 
Msanii wa fialmu Bongo, Mariam akiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu Kuambiana.
Mwili wa marehemu Kuambiana ukiwasili makuburini tayari kwa shughuli za kuusitiri.
Jeneza lenye mwili wa marehemu Kuambiana likishushwa kaburini.
Jeneza likishushwa kaburini.
Msanii wa filamu, Richie Richie akiweka udongo kwenye kaburi la marehemu Kuambiana.
Baadhi ya mafundi wakichanganya zege kujengea kaburi.
Mafundi hao wakikamilisha shughuli za kujengea kaburi hilo.
Mchungaji akiweka msalaba kwenye kaburi.
Mke wa marehemu Janeth Rithe ambaye ni Diwani Kata ya Kunduchi (Chadema), akiweka shada la maua kwenye kaburi la mumewe.
Mkurugenzi Mkuu wa Global Publishers Ltd, Eric James Shigongo akitoa salamu za mwisho kwenye mwili wa marehemu Adamu Kuambiana.
Baadhi ya waombolezaji wakiaga mwili wa marehemu.
Msanii wa Filamu Bongo, Flora Mvungi akiaga mwili wa marehemu Kuambiana.
Mtangazaji wa Kipindi cha Jahazi kinachorushwa na Clouds FM, Ephraim Kibonde akipita kuaga mwili wa marehemu Kuambiana.
JB, akiwa chini baada ya kuzidiwa na kudondoka wakati akitoa wasaha wa marehemu Adam Kuambiana.
Baadhi ya mabaunsa na wasanii wenzake wakimnyanyua JB, baada ya kuzidiwa na kudondoka chini.
Msanii wa Filamu Bongo, Jini Kabula akiaga mwili kwa machungu.
Davina akibebwa baada ya kuzidiwa wakati wa kuuaga mwili wa marehemu Adam Kuambiana kwenye Viwanja vya Leaders, Kinondoni jijini Dar es Salaam leo.
Jack Wolper akipita kutoa heshima za mwisho.
CHANZO GPL