WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, May 5, 2014

‘JK, Shein ndiyo wanaoweza kuirejesha Ukawa bungeni’


Rais wa Tanzania Dk Kikwete akiwa na Rais wa Zanzibar Dk Shein 
Na Raymond Kaminyoge, Mwananchi

Dar es Salaam. Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Juma Duni Haji amesema watu pekee wanaoweza kulinusuru kundi la Umoja wa Katiba ya Watanzania (Ukawa), kurejea bungeni ni Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein.
Duni ambaye pia ni kiongozi wa CUF, alisema hayo jana kwenye mdahalo kuhusu Bunge Maalumu la Katiba tunayoitaka uliofanyika Dar es Salaam.
“Ngoma hiyo imeshakwama, kamwe haturudi bungeni kujadili mambo ya CCM kwani hayatuhusu. Kwa mazingira yaliyopo, ule sasa umegeuka kuwa mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM, wanaweka mambo yenye masilahi kwa chama chao, kamwe haturejei,” alisema.
Alisema kama viongozi hao hawazioni dosari zinazofanywa na wajumbe wa CCM, basi suala la kupata Katiba Mpya ni ndoto kwa sababu Ukawa hawako tayari kurejea katika Bunge hilo.
“Tunawaachia CCM waandae Katiba ya Watanzania, sisi hatutashiriki kwa sababu tumegundua rafu hiyo mapema,” alisema.
Hata hivyo, Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Zanzibar, Vuai Ali Vuai alisema hata kama Ukawa hawatarejea bungeni, vikao vitaendelea kama kawaida kwa sababu kanuni zinawaruhusu kufanya hivyo.
“Katika Bunge Maalumu la Katiba, wapo wabunge wa CCM na wale 201. Walioteuliwa na Rais ambao walitoka nje pamoja na Ukawa ni wajumbe 25 na wamebaki 176, hivyo watu wasiseme waliobaki ni wajumbe wa CCM,” alisema.
Mjumbe wa iliyokuwa Tume ya Marekebisho ya Katiba, Humphrey Polepole alisema Bunge Maalumu la Katiba halina mamlaka ya kubadilisha rasimu hiyo, bali kuiboresha.

source: mwananchi

No comments:

Post a Comment