WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Thursday, October 9, 2014

NENO LA LEO: NI LAZIMA TUPANDE MBEGU...!

Ndugu zangu,

Kwenye moja ya mashairi yake, Marcelino Dos Santos wa Msumbiji anasema; " We Must Plant". Kwa maana ya tuna lazima ya kupanda.
Dos Santos hazungumzii kupanda mbegu za mahindi au mtama, bali kupanda fikra za kimapinduzi kwa wanajamii.

Ni fikra zitakazowasaidia kutoka katika hali iliyopo na kwenda kwenye hali nyingine iliyo bora zaidi.
Na mwanadamu unafanyaje unapoamka na kukuta dunia unayoishi ardhi yake imeanza kumegeka na kuchotwa na bahari? Kuna niliyemwuliza swali hilo. Naye akanijibu;(P.T)

" Huo ndio utakuwa mwisho wa dunia!" Aliyenijibu alikuwa amechoka kufikiri. Nilidhani amgetamka, kuwa angeanza kujifunza kuogelea. Maana, kwa kuogelea majini angeweza kukutana na kisiwa, au nchi kavu.

Wanadamu tumejaliwa akili ili tuweze kufikiri. Na kufikiri ndiko njia mojawapo ya kuiteka kweli. Kufikiri kunahamisha milima na hata kuiweka kando kuruhusu mwanga upite.

Inakuwaje basi mwanadamu anapoacha kufikiri?
Jibu: Anaanza kuamini kwa yasiyo na maana. Ni kama haya ya kuendekeza abrakadabra za Freemasons. Ni kielelezo cha udhaifu wetu Watanzania, Si tunakumbuka ilivyokuwa kwa Babu wa Loliondo, Tuliamua kuacha kufikiri. Ndiyo, kuna waliojifunika vilemba vya ujinga. Wako gizani. Wanahitaji mwanga.
Ni Neno La Leo.
.
Maggid Mjengwa,
Nairobi.

No comments:

Post a Comment