WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Friday, November 30, 2012

“YANI MTU KAFA KWASABABU DAKTARI HAKUWEPO WAT A SHAME”



 Msomaji wangu alitoa maoni haya ambayo kwa kweli yalinigusa sana kufuatia kifo cha msanii John Maganga ambaye alikuwa anafanya vizuri katika kuelimisha umma wa Tanzania.


YANI MTU KAFA KWASABABU DAKTARI HAKUWEPO,WAT A SHAME JAMANI SISI WATANZANIA WAT A SHAME.

 

“Stephano aliingizwa chumba cha upasuaji, wakati sisi kwa maana ya mimi na baba yake tukiwa tumekaa, dokta alitoka na kutuambia mashine za kupumulia zina matatizo kwa hiyo tunafanya transfer ya kwenda Muhimbili kwa matibabu zaidi, hivyo zilifanyika taratibu na Stephano aliingizwa kwenye gari la wagojwa na kupelekwa hospitali ya  Muhimbili.

 
Baada ya kufika Muhimbili, Stephano aliingizwa chumba cha dharura (emergence room), na baada ya dakika kama 10 hivi, alitoka Doctor ambaye tunafaamiana naye na kusema kuwa, kwa tatizo alilonalo John, hatakiwi kufanyiwa upasuaji kama walivyofikiria madaktari wa Mwananyamala ambapo walidhani kuna utumbo umekatika.

 

Daktari huyo wa Muhimbili aliendelea kutuambia sehemu ambayo inaonekana kuleta matatizo ni sehemu ya kongosho ambapo vipimo vinaonesha ina matatizo, ime fell kwa hiyo ina mwaga maji kwenye tumbo ndiyo maana anapata maumivu kwenye tumbo na tumbo kujaa.

Baada ya maelezo hayo Dokta tunayejuana naye alitueleza kwamba mtaalamu wa tatizo hili hayupo na kwamba anategemewa kuja kesho yake asubuhi na kutuasa tuende nyumbani na kwamba watammwekea mashine ya kupumua na sisi turudi kesho.”

 

Kwa kweli kma  msomaji ambaye ameeleza hisia zake hapo jua, ukisoma maelezo haya kweli yanachefua na kuona kuwa hospitali yetu bingwa ambayo tunaitegemea haina emergency protocol , kwa kweli ni aibu ambayo kama taifa lazima tuitafutie mfumbuzi mara moja;

Je huyo daktari bingwa haruhusiwi kiitwa ili aje kuokoa maisha ya mtanzania mwenzetu?

Je daktari huyo bingwa kwa wakati wa tukio alikuwa Nje ya Mkoa wa Dar es salaam au alikuwa Nje ya Nchi?

Je madakatari wetu bingwa hawaruhusiwi kuitwa kazini kama kuna issue ya dharua?

Au wanaitwa katika shughuli za dharua kwa viongozi wa juu tu na familia zao tu?

Je matababu yetu ya dharua yanakwenda kwa madaraja ili dakatari mhusika aweze kurudi kazini na kuokoa maisha ya mgonjwa?

Maelezo haya kweli yamesikikisha na kuhudhunisha sana na tunajiuliza sisi watu wa hali ya chini tukimbilie wapi sasa wakati wa dharura kama madaktari wetu ambao wanafanya kazi zao kwa viapo ya kuokoa maisha ya watu, hawawezi kurudi kazini kutoa huduma mpaka siku inayofuata;

Serikali yetu inamelionaje jambo hili, inakubaliana nautaratibu huu wa utendaji ambao hauonyeshi kujali maisha ya raia wake kupitia madakatari wetu bingwa na sekta nzima ya afya:

 

MWENYEZI MUNGU AILAZE ROHO YAKO MAHALI PEMA PEPONI SISI TULIKUPENDA LAKINI MWENYEZI MUNGU AMEKUPENDA ZAIDI NDUGU YETU JOHN MAGANGA.

No comments:

Post a Comment