WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, November 26, 2012

NINI KIFANYIKE ILI WASANII WA KITANZANIA WASIUZE HAKIMILIKI ZA KAZI ZAO?




Ray Kigosi aliwahi sema kuwa , “Ukweli si kama tunapenda kuuza haki zetu kwa wasambazaji au wanaonunua filamu, sababu kubwa ni ukosefu wa soko la uhakika pamoja na wawekezaji kushindwa kujitokeza”. Hii ni sababu ambayo inaonyesha ukosefu wa sera nzuri za kulinda hakimiliki za wasanii wetu ni jukumu la serikali yetu.

Ray Kigosi “lakini tuwe wakweli na kukumbuka tulikotoka tulikuwa tunaigiza katika Televisheni kwa kulipwa 40,000/ tu kundi la wasanii kibao, lakini leo hii tunamiliki kampuni na kumudu maisha yetu kwa kununua magari na vitu vingine,” tatizo hapa ni wasanii wetu wanaangalia na kufikiria zaidi faida ya muda mfupi elimu inahitajika hapa.

Swali la msingi hapa Je ni jukumu la serikali kuandaa mazingira yatayoweza kumsaidia mmiliki kuweza kuzimiliki  na kumpa mwenye hakimiliki haki zote katika matumizi ya kazi yake au ni jukumu na mhusika mwenyewe kwanza kujiandalia mazingira ya umiliki yeye mweyewe.


Je sheria ya Tanzania inampa nani nguvu ya  hakimiliki? Je hakuna utaratibu ambao katika mazingira yeyote yale yakamsaidia mtunzi kuwa na hisa nyingi katika kazi yake na sio kuishia kuwa  mwajiriwa, na kuishia tu kupewa kiasi Fulani cha pesa mara moja?

Je hakimiliki ni mnyama gani huyu?
katika kifungu na 9(1) cha Sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki ya 1999.
Kifungu hiki cha sheria kinaonyesha haki ambazo wasanii wakizielewa zitawasaidia katika kulinda haki zao kwa faida yao na familia zao nazo ni:

  (i) Kurudufu kazi, (ii) Kusambaza kazi, (iii) Kukodisha, (iv) Kuonesha hadharani, (v) Kutafsiri, (vi) Kubadili matumizi ya kazi, (vii) Kufanya maonesho ya hadhara, (viii) Kutangaza kazi katika vyombo vya utangazaji, (ix) Kutangaza kwa njia nyingine zozote, na (x) Kuingiza kazi nchini.

Haki hizi ndio msaafu wa kazi za wasanii, wanatakiwa kuuelewa ni ili waweze kuuelewa vizuri ni ukweli ambao haupingiki kuwa wasanii wetu wanahitaji ufahamu na uelewa amba ni rahisi kupatikana kupitia elimu.


Kama Pastor Emmanuel Myamba katika moja ya Kongamano; alivyoshauri kuwa, wao kama wasanii  wanahitaji elimu ili iweze kuwasaidia katika kufaya kazi bora na elimu hiyo itawasaidia wao kujua haki za kazi zao.

Je wasanii wetu wakiangalia hiyo sheria ya hakimili wanahaki ngapi? msambazaji anahaki ngapi?

Elimu itawasidia wasanii wetu kuwapa uwezo wa kupapmabua na kujiamini katika maamuzi na umiliki wa kazi zao. Lakini inapotokea msanii anauza  haki zote ategemee nini katika maisha yake kama sio umasikini? Ukifanya kosa hili kubwa la kuuza haki zote basi ujue wewe kuwa umempa nguvu  msambazaji


KWA NINI WASANII WANASHAUSHIKA KUZA HAKI ZAO?
Je ni kwa sababu ya umasikini?
Je ni kwa sababu ya Tamaa ya maendeleo ya haraka haraka?
Je kwa sababu ya kushindwa kuzielewa haki zao?
Je ni kwa sababu ya ushindani miongoni mwao?
Je au ni kwa sababu ya uduni wa kazi zao?

Pengine kwa wakati huu sikubaliani sana na Msanii Vincent Kigosi ‘Ray the greatest’ ambaye aliwahi sema kuwa ni kweli wasanii wanauza haki zao za filamu wanazotengeneza kwa wasambazaji kutokana na hali halisi ya soko lenyewe kuwa finyu likimilikiwa na kampuni moja tu, ambayo angalau imewatoa hapo walipo tofauti na siku za nyuma walivyoanza kuigiza katika televisheni.

Nafikiri tatizo kubwa la wasanii wetu ni Elimu ya uelewa, kujua sheria za kuwalinda kazi zao, na mbaya zaidi wasanii wanatakiwa wapunguze kuridhika haraka na kuona kuwa soluhisho la tatizo la soko na umasikini ambao unawazunguka ni kuuza haki zao zote kwa kipande cha muhogo kumbe na baadae wanakumbuka kuwa kumbe walifanya kosa wakati wanakuwa wameshachelewa kabisa.


Ikumbukwe kuwa watafiti wengi wa habari za wasanii kama Bishop Hiluka  wanasema kuwa sekta ya filamu ni sekta iliyosheheni utajiri mkubwa lakini cha kushangaza ni pale ambapo wadau wake wanaongoza kwa kuwa, na hasa pale ambapo kwa bahati mbaya wanatangulia mbele ya haki warithi wao wanakuwa hawana chochote cha kiuchumi. 

Swali hapa ni nini chanzo cha hali hii? Hapa tunapata mitazamo tofauti pengine kutokupewa kipaumbele amabcho kinalenga sheria nzuri za kuwalinda wasanii wetu hasa katika kumiliki kazi zao kwa faida yao wenyewe.


Nje ya sababu zote za kisheria na sera mbovu za serikali kuhusu kazi za wasanii; mimi naona vile vile kunatatizo kubwa sana linalotokana na dhana ya kutojiamini na kuridhika upesi kwa wasanii wenyewe na kukosa sauti ya kushikilia kazi zao na hivyo kumpa sauti na nguvu zaidi msambazaji ambaye kwa upande wake yeye anakuwa na pesa za kununua kazi hiyo na kushikilia hakimiliki na kuwaacha wasanii wetu wakiendelea kushikilia kuti kavu la maisha yao. 




Katika kuhakikisha kuwa kilio cha wasanii kinafikia mwisho na kuwawezesha kufaidi zaidi kazi zao na faida itokanayo na kazi zao. Serikali imeazimia kuifanyia marekebisho  sheria ya Ushuru wa Bidhaa, Sura 147, huku akitambua kuwepo kwa kilio cha muda mrefu cha wasanii kurudufiwa kazi zao za sanaa na kukosa maslahi kwa kazi wanazofanya., Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato itaanza kurasimisha biashara ya bidhaa za muziki na filamu kwa nia ya kuhakikisha kwamba uasili wake unatambulika na hivyo kuzuia vitendo vya kurudufu kazi za sanaa hali ambayo inadumaza ukuaji wa sanaa na vipaji hapa nchini.Tumebakiwa na kipindi kifupi tu  kwa Mamlaka ya Mapato kuanza kuweka stampu kwenye bidhaa hizo ili uuzaji wa kazi hizo uwe rasmi na kuwawezesha wasanii kupata kipato stahili kutokana na kazi zao, uwekaji huo wa stampu utaanza kuanzaia  tarehe 1 Januari, 2013.


Pamoja na nia nzuri ya serika bado tunaendelea kuwahimiza wasanii kuwa, marekebisho ya sheria pekee hayatoshi lakini wasanii wanahitaji zaidi vilevile elimu itakayo wasaidia kujiamini na kuthubutu katika kazi zao, pamoja na nchi yetu kukosa kabisa mfumo mzuri ambao ungesaidia kumuendeleza msanii wa Tanzania na hatuna vyuo vinavyotoa mafunzo yanayojikita kwenye filamu tu kama ilivyo kwa jirani zetu.

KIFO CHA KANUMBA KIMETUFUNDISHA NINI KUHUSIANA NA HAKIMILIKI?

Kama kweli kama waandishi na wadadisi wa mambo walivyowahi kuongea kuwa pamoja na sekta ya filamu kuwa na nguvu na mvuto ndani ya jamii, lakini wahusika wake wamendelea kutofaidika sana na kazi zao; mfano ambao wengi wanautoa ni ule wa Marehemu Steven Kanumba hasa pale wanapouliza

Kanumba baada ya kufa amefaidika vipi? Taathimini ya uchambuzi wa namna kanumba pengine alivyokuwa maarufu lakini wakati wa kifo chake mengi yalijitokeza hata kamati ya mazishi ambayo ilikuwa na wajumbe wake wengi wasanii wenzake waliwahi sema kuwa, imedai kanumba amefariki dunia akiwa maskini, kinyume kabisa cha umaarufu mkubwa aliokuwa nao wakati wa uhai wake. Kanumba alishiriki kwenye filamu zaidi ya 40 lakini amekufa maskini.

Tatizo ni nini hasa? Jibu ni  haki za wasanii na watayarishaji wa filamu zitaendelea kuporwa, kwa kutumia unyonge wao na umasikini wao wataendelea kutumika kwa maslahi ya wachache, na mwishowe watakufa wakiwa masikini lakini wenye majina makubwa, tena bila hata kuwaachia wategemezi wao urithi unaoeleweka. Mwandishi mmoja aliwahi sema “kuwa Kama mwandishi mmoja alivyowahi sema kuwa;”Kwa wenzetu pesa inatengenezwa hata pale mtu anapokuwa amefariki dunia, hii ni kutokana na nchi hizo kuwa na sheria nzuri za hakimiliki, serikali kuwasimamia watu wake na viongozi kutimiza wajibu wao ipasavyo. msanii anaeendelea kutengeneza fedha nyingi japo amefariki miaka mingi sana iliyopita”.


Nakubaliana na falfasa hii kuwa “Kwa mtu aliyefanya kazi nzuri, kufariki siyo mwisho. Anaweza kuendelea kuishi hata baada ya kifo, kwani kazi zake, pamoja na nembo zake zinaweza kuendelea kuvuna mashabiki ambao wanamkumbuka, na wale waliozaliwa muda mrefu baada ya kufa, na kuingiza mapesa kibao kama inavyotokea kwa mastaa niliowataja hapo juu”

Tatizo la ukosemu wa elimu na umakini ndio umemfanya Marehemu Kanumba na wengine waliotangulia mbele ya haki kuwa jasho lao kuendelea kufaidisha watu wachache kosa liko wapi?

Hebu tumtathimini maisha msanii maarufu, Kanumba alikuwa mmoja wa wale ambao walikuwa wanaojiona washindi kwa kuingia mikataba inayowafanya kuuza haki zao kwa msambazaji na kuishia kupewa gari na pesa zinazowasaidia kwa miezi michache, masikini hakujua kabisa kuwa atakapoaga dunia haki yake itakuwa imeishia hapohapo, na hawa waliobaki wanapaswa kujifunza kupitia yeye kwani siku 'wakichuja' na thamani yao kupungua watarudi kwenye msoto kwani haki zao tayari zitakuwa zimeshapotea.

Baraza la sanaa Tanzania Basata liendelee kuwaelimisha wasanii kuhusu nini maana ya haki miliki; kama ilivyojadiliwa na waandisha kadhaa wa habari za sanaa na sheria za haki miliki kuwa, Sheria ya Hakimiliki ya nchi yetu inasema wazi kuwa hakimiliki hudumu kwa mwenye haki kwa maisha yake yote na miaka hamsini baada ya kifo chake. Kwa nchi kama Marekani wameongeza hadi miaka sabini. Ndiyo maana utaona kuwa kuna kazi nyingi ambazo zinaendelea kuwa maarufu miaka mingi baada ya wenye kazi kufariki, huku zikiwanufaisha warithi wao.


Hebu tumsikilize Issa Mussa Claude anahoja nzito kama wasanii wameisikia itawasaidia sana  kuamka mara moja, wakumbuke kuwa  wakati ni ukuta wasanii wanatakiwa kubadilika ili waweze kufurahia vipaji vyao na faida inayotokana na kazi zao na sio kuendelea kumtajirisha mtu mwingine kwa jasho lao linalopatikana kwa kazi ngumu ya kufikiri na kutenda


wasanii wakifanikiwa kuyasimamia haya sanaa itakuwa ndio gurudumu nzuri kwa maendeleo yao na familia zao na fani ya sanaa haitaendelea kuwa ni fani ya kuganga njaa tena.

No comments:

Post a Comment