WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Thursday, November 29, 2012

KILI STARS YALALA CHALI I - O KWA BURUNDI


Kocha wa Tanzania, Mdenmark, Kim Poulsen akihamaki wakati dakika zikiyoyoma, huku timu yake ikiwa imelala 1-0 katika mchezo wa Kundi B, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge dhidi ya Burundi, Uwanja wa Mandela, Namboole, usiku huu. Burundi ilishinda 1-0
Mbunge wa Kondoa, Juma Nkamia (kushoto) akiwa na Mjumbe wa TFF, Wallace Karia wakifuatilia mchezo wa Kundi B, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge kati ya Tanzania na Burundi Uwanja wa Mandela, Namboole, usiku huu. Burundi ilishinda 1-0
Kikosi cha Stars leo
Mshambuliaji wa Tanzania, Simon Msuva akitafuta mbinu za kumtoka beki wa Burundi katika mchezo wa Kundi B, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge Uwanja wa Mandela, Namboole, usiku huu. Burundi ilishinda 1-0.
Mshambuliaji wa Tanzania, Simon Msuva akijaribu bila mafanikio kumfunga kipa wa Burundi,Arthur Arakaza katika mchezo wa Kundi B, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge Uwanja wa Mandela, Namboole, usiku huu. Burundi ilishinda 1-0.
Mshambuliaji wa Tanzania, Mrisho Ngassa akiwatoka mabeki wa Burundi katika mchezo wa Kundi B, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge Uwanja wa Mandela, Namboole, usiku huu. Burundi ilishinda 1-0
Mshambuliaji wa Tanzania, Mrisho Ngassa akiwatoka mabeki wa Burundi katika mchezo wa Kundi B, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge Uwanja wa Mandela, Namboole, usiku huu. Burundi ilishinda 1-0.
Kiungo wa Tanzania, Frank Domayo akimdhibiti kiungo wa Burundi katika mchezo wa Kundi B, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge Uwanja wa Mandela, Namboole, usiku huu. Burundi ilishinda 1-0.
Kiungo wa Tanzania, Frank Domayo akimdhibiti kiungo wa Burundi katika mchezo wa Kundi B, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge Uwanja wa Mandela, Namboole, usiku huu. Burundi ilishinda 1-0.
Mshambuliaji wa Tanzania, Mrisho Ngassa akimtoka beki wa Burundi katika mchezo wa Kundi B, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge Uwanja wa Mandela, Namboole, usiku huu. Burundi ilishinda 1-0.
Mshambuliaji wa Tanzania, John Bocco akiruka juu lupiga mpira kichwa mbele ya mabeki wa Burundi katika mchezo wa Kundi B, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge Uwanja wa Mandela, Namboole, usiku huu. Burundi ilishinda 1-0.
Mashabiki wa Tanzania wakishangilia bila kukata tamaa

Na Mahmoud Zubeiry, Kampala
BAO pekee la mshambuliaji wa zamani wa Simba SC, Suleiman Ndikumana dakika ya 52, leo limeizamisha Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars katika mchezo wa Kundi B, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge Uwanja wa Mandela, Namboole, usiku huu. 
Nahodha huyo wa Burundi, anayechezea Inter Stars ya nyumbani kwao kwa sasa, alifunga bao hilo kwa penalti, baada ya yeye mwenyewe kuangushwa kwenye eneo la hatari na Shomary Kapombe.
Hadi mapumziko hakuna timu iliyofanikiwa kuona lango la mwenzake na Burundi walifanya mashambulizi mawili ya hatari zaidi, lakini sifa zimuendee ‘TZ One’, Juma Kaseja aliyeokoa hatari hizo.
Stars hawakucheza soka yao ya chini kutokana na hali mbaya ya Uwanja, kujaa matope, kuwa wenye kuteleza kutokana na mvua kubwa iliyonyesha kutwa nzima ya leo.
Kipindi cha pili Stars walijitahidi kutaka kusawazisha mabao hilo, lakini bahati haikuwa yao na zaidi waliishia kukosa mabao mawili ya wazi.
Kwa matokeo hayo, Burundi imeendelea kuongoza Kundi A, kwa pointi zao sita, mabao sita ya kufunga na moja la kufungwa, wakati Bara inabaki nafasi ya pili kwa pointi zake tatu, Sudan ya tatu ikiwa na pointi tatu na Somalia yenye pointi moja inashika mkia.
Kikosi cha Tanzania Bara leo kilikuwa; Juma Kaseja, Erasto Nyoni, Amir Maftah, Shomary Kapombe/Issa Rashid, Kevin Yondan, Frank Domayo, Mrisho Ngassa, Salum Abubakar, John Bocco, Mwinyi Kazimoto/Shaaban Nditi na Simon Msuva/Amri Kiemba.
Burundi; Arthur Arakaza, Gilbert Kaze, Haruna Manirakiza, Hassan Hakizimana, Emery Nimubona, Yussuf Ndikumana, Steve Nzigamasabo, Chris Nduwarugira, Suleiman NdikumanaChris Ndayishimiye na Amisi Tambwe.
source: vijimambo.blog

No comments:

Post a Comment