WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Tuesday, November 20, 2012

Dk. Slaa amtaka Kikwete kutoshambulia upinzani


Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa, amemtaka Rais Jakaya Kikwete kutotumia muda mwingi kuvishambulia vyama vya siasa.
Badala yake Dk. Slaa amemtaka Rais Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutumia muda huo kuzungumza jinsi ya kutatua kero za wananchi ili kupunguza ukali na ugumu wa maisha unaowakabili sasa.

Aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika Mahakama Kuu ya Kanda ya Arusha kuhusiana hoja mbalimbali zilizozungumzwa katika mkutano wa CCM uliofanyika jijini Dar es Salaam juzi.
Akijibu shutuma mbalimbali zilizotolewa katika mkutano wa kuwapokea viongozi mbalimbali wa CCM waliochaguliwa mjini Dodoma, Dk. Slaa alisema katika mkutano huo viongozi wengi wa chama hicho akiwamo Rais Kikwete, walitumia muda mwingi kuelekeza nguvu zao jinsi ya kukabiliana na vyama pinzani katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
Alisema CCM imeelekeza nguvu zake kujifua ili kukikabili Chadema katika uchaguzi ujao na siyo kuwaeleza wananchi nini watawafanyia ili kuwaondoa katika janga la umaskini.
Aidha, aliwatuhumu viongozi wa CCM kuchukua sera mbalimbali zilizoanzishwa na Chadema ikiwamo ya kusomesha wanafunzi bure kutoka shule ya msingi hadi sekondari.
Aidha, alisema anashangaa uteuzi wa Katibu Mkuu wa ccm, Abdulrahman Kinana kwa madai kwamba siyo msafi.
CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment