WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Tuesday, October 30, 2012

Maalim Seif ashauri kupatiwa taaluma kwa vikosi vya serikali ya mapinduzi kukabiliana na vurugu


Tuesday, October 30, 2012
 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo yake na ujumbe wa Umoja wa Mataifa huko Ofisini Kwake Migombani Zanzibar. Kushoto ni kiongozi wa ujumbe huo Bw. Akinyemi Adegbola.


Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akiagana na kiongozi wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa Bw. Akinyemi Adegbola baada ya mazungumzo yao huko Ofisini Kwake Migombani Zanzibar. Kushoto ni Mjumbe wa Umoja huo ofisi ya Zanzibar bibi Njeri Kamau.(Picha, Salmin Said, OMKR).
 Na Hassan Hamad OMKR

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad amesema vikosi vya ulinzi vya Tanzania na vile vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar vinahitaji kupatiwa mafunzo ya ziada juu ya kukabiliana na vitendo vya vurugu na kulinda amani ya nchi.

Amesema vikosi hivyo vimekuwa vikitumia nguvu za ziada katika kukabiliana na vitendo hivyo, hali inayopelekea kuleta madhara kwa raia wasiokuwa na hatia pamoja na mali zao.

Maalim Seif ametoa kauli hiyo ofisini kwake Migombani Mjini Zanzibar alipokuwa na mazungumzo na ujumbe wa Umoja wa Mataifa uliofika kwa ajili ya kubadilishana mawazo.

No comments:

Post a Comment