WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, October 31, 2012

Dkt Shein Afanya Uteuzi




NA MAELEZO ZANZIBAR 31/10/2012 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein amemteua Amina Juma Zidikheir kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Utumishi wa Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Zanzibar. Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar Dkt Abdulhamid Yahya Mzee imesema kuwa uteuzi huo ameufanya kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya kifungu 8(1) (a) cha sheria ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Zanzibar namba 11 ya mwaka 2003. Amina Juma Zidikheri aliwahi kuwa Mhasibu mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kabala ya kustaafu kwake. Uteuzi huo umeanza tarehe 27 Oktoba,2012 

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR 31/10/2012

No comments:

Post a Comment