WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Sunday, October 21, 2012

SIMBA KUNANI? YATOKA SARE TENA NA MGAMBO JKT





MABINGWA watetezi wa ligi kuu ya Tanzania Bara, Simba leo wameendelea kuchemsha baada ya kulazimishwa kutoka suluhu na Mgambo JKT katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.

Licha ya kulazimishwa sare, Simba bado inaendelea kuongoza ligi hiyo kwa kuwa na pointi 19 baada ya kucheza mechi tisa, lakini inaweza kuenguliwa kileleni na Azam, iwapo itashinda mechi yake dhidi ya Ruvu Shooting Jumatano ijayo kwenye uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.

Katika mechi nyingine ya ligi hiyo iliyochezwa leo, JKT Ruvu ilitoka sare ya bao 1-1 na ndugu zao wa JKT Oljoro katika mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Chamazi wakati Prisons iliichapa Toto African bao 1-0 kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.

Habari na Liwazo Zito blog

No comments:

Post a Comment