WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, October 24, 2012

JE UVUMILIVU NI KARAMA AU MAZOEA


UVUMILIVU HUJENGWA NA MISINGI GANI?

Taifa letu katika siku hizi za karibuni limeendelea kugubikwa na wimbi la matendo ambayo yanaashiria uvunjaji wa amani ambayo Viongozi wetu waanzilishi wa Taifa hili wazee wetu hayati Abeid Aman Karume na Mwalimu Julius Nyerere, walifanya kazi kubwa kuasisi Amani na Umoja wa kitaifa ambao umekuwa ni kioo cha Taifa letu katika macho ya kimataifa.


Tumeendelea kuona matukio ya kutisha yakiendelea kutokea sehemu mbalimbali kama vile Zanzibar, Dar es salaam, Arusha na kwingineko wakati kundi moja likijiona kuwa lina haki zaidi kuliko kundi nyingine na kusababisha hata wananchi kadhaa kupoteza maisha na mali zao.

Naanza kwa kujiuliza kuwa je fujo za aina hii zinapotokea ambazo zinasababisha uvunjaji wa makusudi wa amani pengine dhidi ya jamii au kundi nyingine, na kundi ambalo linatendewa vibaya kwa kudhalilishwa au hata kuharibiwa mali zao na halichukui hatua ya kulipa kisasi mara moja na kusababisha maafa makubwa kwa amani ya Taifa swali hapa ni je kundi hilo linakuwa katika hali ya subira au uvumulivu? Je kama wako kwenye subira, subira yao itaisha lini na nini kitatokea?


Je na viongozi wetu nao wanakuwa na subira au uvumilivu? Wa kuto chukua hatua inayostahili ili kukomesha fujo ana matendo hayo ya uvunjaji wa amani? 

Kwa haraka haraka tu Uvumilivu ni uwezo wa, au ni mazoezi ya, kutambua na kuheshimu imani au matendo ya wengine; uvumilivu uko katika kila nyanya ya maisha yetu, kuanzia maisha yetu ya kila siku;

TATIZO katika maisha ya kawaida sana, swala la uvumilivu halizungumzwi sana, tunachokiona sana ni mazungumzo ya kulipa kisasi;

Nafikiri itakuwa jambo njema kama tutaendelea kufundisha na kuhubiri uvumilivu katika nyanya zote. Pengine fujo hizi ambazo taifa linaendelea kujionea zikizidi kujitokeza zingeweza kukoma au kupungua.

Uvumilivu huongelewa sana kwa mapana hasa katika maswala ya uongozi, uongozi ni hali ya kuongoza nchi katika mwelekeo wa kuleta maendeleo na ni ukweli kama mwandishi mmoja alipowahi sema kuwa “KUONGOZA watu na hasa wa watu wazima ni kazi nzito inayohitaji mtu anayepewa jukumu hilo kuwa makini, vinginevyo mambo yanaweza kuwa magumu na hatimaye kuangukia katika mtego wa udikteta. 

Hii inatokana na kukosekana mambo makubwa matatu ambayo ni ufahamu au maarifa, hekima na  hasa uvumilivu. Kiongozi asiye mvumilivu anaweza kujikuta anatumia mabavu kutawala ili watu wajue kuwa yupo, ana nguvu na ana mamlaka”. Na hii falfasa ambayo huangukia kwa wananchi vile vile pale ambapo wanakuwa hawana uvumilivu;

Ni ukweli ulio wazi kuwa  kiongozi anatakiwa kuwa, mtulivu, mvumilivu na anayetumia zaidi hekima kuliko mabavu”, kiongozi anatakiwa Kuwa na  msimamo wa uvumilivu ni moja ya kazi ngumu zaidi miongoni mwa viongozi dhidi ya wananchi katika jamii. Ni ukweli ambao haufichiki kuwa  viongozi hawakuzaliwa wakiwa wavumilivu, lakini lazima tujifunze kuwa wavumilivu. Na hii ni kweli hata kwa jamii inatupasa kuvumiliana na kumaliza tofauti zetu kwa busara ya majadiliano.


Katika siasa uvumilivu wa kisiasa unakuza  utamaduni wa utawala bora na ukomavu wa demokrasia; na Kwa demokrasia kufanya kazi vizuri, wananchi lazima kuwa tayari kuvumilia na kuvumiliana.

Dhana ya uvumilivu ni ya msingi sana kwa maendeleo kwani inaruhusu mawazo mapya ndani ya jamii; kupitia dhana hii ya uvumilivu, kiongozi anakuwa  tayari kukubali  na kuheshimu  maoni na mawazo ya watu wengine na haki zao kwa uwazi na uhuru. Katika hali hii,uvumilivu huruhusu kuwepo kwa vyombo  huru vya habari kutumika kama chombo muhimu kuwahabarisha wananchi na kuwasilisha madai yao kwa viongozi wao.


Demokrasia inahitaji vyombo vya habari ambavyo hugeuka kuwa daraja la mawazo kati ya viongozi na waongozwa. Vyombo huru vya habari husaidia   wananchi kuelewa taratibu ambazo zinaimarisha demokrasia.uvumilivu wa viongozi huru utasaidia kueneza demokrasia  na uwajibikaji kwani wananchi wataweza kukosoa serikali na ujumbe kufikishwa serikalini bila kuogopa.


Ni ukweli kuwa Falsafa ya Uvumilivu hufunza na kuwakumbusha viongozi na wananchi wake kuwa wanatakiwa kuishi kulingana na fikira njema. Mwenye kuifuata falsafa ya uvumilivu hayuko tayari kuamsha fikra mbaya za uvunjajiwa amani bali daima atajitaidi kuziepusha kwa kuendeleza uamuzi  wa uwazi na kwa kutumia njia  ya utulivu wa hekima kupitia uzoefu makini wa kimantiki: Kiongozi mwenye uvumilivu daima hutafakari, na kuziweka fikira mahali pamoja kabla ya kufanya uamauzi.Msingi wa kimaadili wa falsafa ya uvumilivu  kama mtaalam mmoja alivyo wahi kusema kuwa kwa ufupi tunaweza kusema kuwa uvumilivu umesheheni nini?

Kwa wananchi wa Tanzania bado tuna kila sababu ya kuendelea kuenzi na kuthamini uvumilivu miongoni mwetu; uvumilivu kati ya wananchi wa dini tofauti, kusikilizana na kushauriana kwa faida ya taifa letu; tukiweza kuutumia uvumilivu katika kiwango cha juu tutafanikiwa kuondoa chuki ambayo inaanza kueneakatika taifa letu;

Kwa ufupi Uvumilivu  tunaweza kuueleza kuwa:

  • Tendo lililojaa subira kubwa,
  • Tendo lililojaa utu,
  • Tendo ambalo linaashiria Ukuaji wa demokrasia


Ni ukweli ambao haufichiki kuwa sisi kama  wananchi tukiweza kuvumiliana katika maisha yetu ya kawaida, na kuweza kukosoana bila kugombana mara moja  hurudisha imani ya wananchi, upendo na matumaini kati wananchi wao kwa wao au dhidi ya serikali yao; Tukumbukwe kuwa Ingawa watu wengi kufikiria uvumilivu ni upole  na kuto wajibika la hasha uvumilivu ni uwajibikaji ulio jaa busara na subira; 

  • Kwa nini uvumilivu wetu unatoweka katika kipindi hiki cha sasa?
  • Ni kweli kuwa hakuna nafasi ya wananchi kuvumiliana katika kuchangia hoja katika mambo mbali mbali yanayohusu maendeleo ya Taifa letu au pale kunapotokea kutofautiana?
  • Kuna maswali mengi sana ya kujiuliza hasa katika kipindi hiki ambapo kuna mwendelezo wa fujo.


MUNGU IBARIKI TANZANIA TUJALIWE TUWEZE KUDUMISHA UVUMILIVU 

No comments:

Post a Comment