WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, October 22, 2012

Jalada la Elizabeth Michael ‘Lulu’ larejeshwa Kisutu


 
Picture

Msanii maarufu wa filamu nchini, Elizabeth Michael a.k.a LULU, (Katikati), akielekea kupanfa basi la magereza kwenye viwanja vya mahakama ya hakimu mkazi Kisutu, baada ya kesi inayomkabili ya kutuhumiwa kumuua msanii mwenzake, Hayati Steven Kanumba, kuahirishwa tena na hivyo mwanadada huyo ambaye umri wake unaleta utata ataendelea kusota rumande hadi hapo kesi yake itakapotajwa tena. (picha via K-VIS)
MSANII  wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, anayekabiliwa na kesi ya mauaji, amehoji Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuhusu lilikofikia jalada la kesi.

Lulu aliuliza swali hilo jana mbele ya Hakimu Mkazi Stuarti Sanga baada ya Wakili wa Serikali, Keneth Sekwao kudai kuwa kesi ilikuja kwa ajili ya kutajwa na kwamba, upelelezi wake haujakamilika.

Baada ya Sekwao kueleza hiyo, Lulu alinyoosha mkono na kuhoji jalada la kesi inayomkabili lilikofikia. Hakimu Sanga alimuuliza Wakili Sekwao iwapo anauliza jalada halisi au la kudurufu.

Wakili Sekwao alimwambia Hakimu Sanga kuwa, anaulizia jalada halisi.Hakimu Sanga alimwambia Lulu kuwa jalada halisi limekwisharudi  na kuahirisha kesi hiyo hadi Novemba 5, mwaka huu itakapotajwa tena.

Lulu anatuhumiwa kumuua msanii mwenzake, Steven Kanumba. Anadaiwa kutenda kosa hilo Aprili 7, mwaka huu nyumbani kwa Kanumba, Sinza, Dar es Salaam.

Habari imeandikwa na Tausi Ally via MWANANCHI
Picture
Lulu akielekea kupanda gari tayari kwa safari ya Segerea kunako mahabusu. (picha via K-VIS)
Source: http://www.wavuti.com

No comments:

Post a Comment