WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Thursday, October 25, 2012

UGOMVI WA SHY-ROSE BANJI VS SOPHIA SIMBA TUNAJIFUNZA NINI?


 


WAPAMBE wakiwasha moto



SWALI LILILOLETA MTAFARUKU:

"Wewe ukiwa mwenyekiti wa UWT kwa kipindi cha miaka minne iliyopita hatujawahi kukuona ukisimama jukwaani kutetea Chama."

Jibu 
 la swali 
Sofia Simba alijibu "Inaonekana aliyeuliza swali hajakomaa katika siasa za nchi, ndio maana ameambulia kuzomewa na wajumbe wa mkutano huu. Habwatuki bungeni au majukwaani kwa vile yeye ni serikali, na hata mbunge wa CCM hapaswi kukikosoa chama chake. Mimi si mithili ya upinzania kukaa na kukiosoa chama napaswa kukitetea. Anayesema Sofia Simba hajafanya kitu anajidanganya kwani wapiga kura wako kwenye matawi, kata, wilaya na mikoa, hao ndio wapiga kura wa chama na mimi kama mwenyekiti wa UWT nilijiimarisha katika ngazi za chini."

Je Baada ya jibu hili tunafikiri kulikuwa na sababu yeyote ya wawili hawa ambao wamekabidhiwa dhamana ya uongozi katika nafasi mbalimbali ndani ya serikali  kuzozona?

Je mzozano wao ndio ukuaji wa demokrasia au ilikuwa tu ni sehemu ya kuonyeshana ubabe na nani ni nani mbele ya wapambe wao?

Nafikiri kama taifa tunahitaji zaidi viongozi ambao wanaweza kuvumiliana nakukabili challenges katika njia ambayo itadumisha amani na kuepusha ugomvi na uhasama.

Tulijenge Taifa pamoja kwa upendo na kuvumiliana.

No comments:

Post a Comment