WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, October 6, 2012

NAFASI YA ZANZIBAR KATIKA MJADALA WA KATIBA MPYA

TamKongamano - Nafasi ya Zanzibar katika mjadala wa kba mpya

TAMKO LA PAMOJA LA KONGAMANO LA KITAIFA LA KUZUNGUMZIA NAFASI YA ZANZIBAR KATIKA MJADALA WA KATIBA MPYA, UKUMBI WA SALAMA, HOTELI YA BWAWANI, TAREHE 06 OKTOBA, 2012

Sisi washiriki wa Kongamano la Kitaifa la Wazanzibari tuliloliitisha kuzungumzia Nafasi ya Zanzibar katika Mjadala wa Katiba Mpya leo hii Jumamosi, tarehe 06 Oktoba, 2012 katika Ukumbi wa Salama, Hoteli ya Bwawani, mjini Zanzibar tunatambua kwamba fursa iliyopo mbele yetu katika Mjadala huu wa Kitaifa ni fursa adhimu ambayo inapaswa kukumbatiwa na kila Mzanzibari Mzalendo katika kuamua Mustakbali wa Zanzibar na watu wake.

Katika kuikumbatia fursa hii, tunatambua, kuheshimu na kuthamini hatua iliyofikiwa ambapo Wazanzibari kutoka makundi na taasisi tofauti wameungana na kuja pamoja katika kusimamia na kuendesha harakati zenye lengo la kuirejesha Zanzibar yenye mamlaka kamili kitaifa na kimataifa itakayofuatiwa na mashirikiano ya Muungano wa Mkataba kati yake na Tanganyika.
 
Hata hivyo, tunaelewa pia kuwa zimekuwepo jitihada za makusudi za kujaribu kuuvunja umoja huu wa Wazanzibari kwa kutumia hoja dhaifu zenye lengo la kutuondoa katika mstari ili kuzima vuguvugu la Wazanzibari.

Mhsoor alipochangia kwenye Kongamano la nafasi ya Zanzibar



Mh Mansoor Yussuf Himid amewataka baadhi ya watu kutokuwa wepesi kwa kuwanyooshea vidole wenzao kwa sasa ni wakati wa kuzungumza kweli tena bila ya uwoga hasa katika mustakbali wa wazanzibar na nchi yao.
 
Amesema wanaosimama na kusema hadharani kuwa mkiutaka msiutake muungano ndio huu huu kuwa wanakosea kwani hakuna mwenye haki ya kumlazimisha mtu juu ya anachokitaka mwenyewe.
Iweje leo baadhi ya viongozi wawatishe wananchi juu ya mustakbali wa nchi yao
 
Amewataka Wazanzibari kutokukubali kurudishwa walipotoka kwa sasa ni kwenda mbele na sio kurudi tena nyuma na amewaomba viongozi wenzake kuwa ni mabalozi juu ya hili kufikisha ujumbe kwa wengine wasiojua nini cha kufanya kwa sasa juu ya nchi yao ili waweze kuungana na wazanzibari wanaotaka kupumua na muungano huu.
 
Pia amesema yeye haoni tatizo kwa mwananchi kutoa maoni yake anayoyataka juu ya muungano anaoutaka mwenyewe.
 
Amewataka wananchi kutokuvunjika moyo na wajitokeze kwa wingi sana kutoa maoni yao wakati wa tume ya kukusanya maoni itakapopita waende kwa wingi sana kwenye mchakato wa kutoa maoni muda utakapofika ili waweze kuikomboa Zanzibar yao.

Stori kwa hisani ya Hamed Mazrui via Face book

Jssa aipongeza kamati ya maridhiano


 Mh Ismail Jussa amewapongeza wanachi kwa kujitokeza kwao kwa wingi sana katika kongamano lilofanyika leo Bwawani. Pia ameipongeza kamati ya maridhiano kwa kitendo cha kuwakatisha tamaa wale wote wasioitakia mema Zanzibar.
 
 Pia amemuomba MwenyeziMungu kumpa umri mrefu Mzee wetu  Hassan Nassor Moyo mpaka siku Zanzibar itakapokuwa huru na kwenda kupachika bendera yake Umoja wa Mataifa na kuweza kutambulika kuwa ni nchi huru.
 
Amesema kuwa yeye binafsi hatachukua maamuzi yoyote yatakayokwenda kinyume na chama chake hapa amekusudia kuwavunja moyo wale wasiojua kwa nini amejiuzulu unaibu Katibu Mkuu jana ila lengo lake nikupata wasaa nzuri wa kuongeza nguvu katika wimbi la kuitetea Zanzibar ndani ya Baraza la Wawakilishi

No comments:

Post a Comment