WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Friday, March 7, 2014

YANGA, AL AHLY KUCHEZA ALEXANDRIA

MMG25849_803f3.jpg

Wachezaji wa Young Africans mara walipowasili katika hoteli ya Nile Paradise Inn jijini Cairo

Baada ya utata juu ya ni sehemu gani utakaofanyika mchezo wa marudiano kati ya wenyeji Al Ahly dhidi ya wawakilishi pekee wa Tanzania kwenye mashindano ya Kimataifa Young Africans huku ikiwa iebakia siku tatu kabla ya mchezo, maamuzi ya shirikisho la soka nchini Misri yameamulu mchezo huo utafanyika mjini Alexandria katika Uwanja wa Border Guard stadium (Haras el Hadod)

Taarifa ya Chama cha Soka nchini Misri imesema mchezo huo ambao awali ulikua ufanyike katika jiji la Cairo sasa utafanyika katika mji wa Alexandria takribani kilometa zaidi ya 200 kutoka Cairo ambapo kikosi cha Young Africans kimeweka kambi kujiandaa na mchezo huo.

Mara baada ya kupata taarifa hizo kupitia Ubalozi wa Tanzania nchini Misri, uongozi wa Young Africans uliopo jijini Cairo ukiongozwa na makamu mwenyekiti Clement Sanga ambaye pia ndio mkuu wa msafara, tayari umeanza maandalizi ya kuhakikisha timu inakwenda mjini Alexandria kucheza mchezo huo wa jumapili na kufanya vizuri.

Ni jambo la kushangaza taarifa za Uwanja zinatolewa siku tatu kabla ya mchezo huku fika wahusika wakitambua kuwa Young Africans ilifahamu mchezo huo utafanyika Cairo takribani wiki mbili zilizopita viongozi wa Al Ahly waliopokuwa nchini Tanzania walidhibitisha hilo.

Pamoja na mabadiliko hayo ya ghafla ya sehemu utakapofanyika mchezo siku ya jumapili, benchi la ufundi pamoja na wachezaji na viongozi waliopo jijini Cairo bado wana imani ya kufanya vizuri na kusonga mbele katika hatua ya 16 bora.

Wakati huo huo washambuliaji wawili wa timu ya Taifa ya Uganda Hamisi Kizza na Emmanuel Okwi tayari wameshawasili jijini Cairo majira ya saa 7 usiku kwa shirika la ndege la Egypt Air wakitokea nchini Zambia walipokuwa wakiiwakilisha timu yao ya Taifa kwenye mchezo wa kirafiki jana siku ya jumatano.

Wachezaji hao mara baada ya kuwasili Uwanja wa ndege moja kwa moja wameungana kambini na wachezaji wengine katika Hoteli ya Nile Paradise Inn kuendelea na maandalizi ya mchezo huo wa jumamosi.

Mchezo huo wa siku ya jumapili ambao unafanyika mjini Alexandria katika Uwanja wa Border Guard Stadium (Haras El Hadod) hautakua na watazamaji kutokana na mamalaka ya ulinzi na usalama kuzuia mashabiki kuingia katika mchezo wowote wa mpira wa miguu nchini Misri.

source: mjengwa blog

No comments:

Post a Comment