WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, March 17, 2014

MBUNGE MTEULE WA KALENGA ASHUKURU WAPIGA KURA , CHADEMA WAPINGA USHINDI WAKE ....


Godfrey Mgimwa na Robby Mgimwa wakionesha hati yao ya ubunge baada ya kukabidhiwa leo
 
 
Mbunge mteule  wa  jimbo la Kalenga  Bw Mgimwa akionyesha  dole


Sehemu ya msafara wake


Boda boda nao walikuwepo


AKIWA ameambatana na mkewe, Robby Mgimwa, Godfrey Mgimwa wa Chama cha Mapinduzi (CCM) jana alitangazwa mshindi wa ubunge katika uchaguzi mdogo jimbo la Kalenga baada ya kuvibwaga kwa kura za kishindo vyama vingine viwili vilivyoshiriki uchaguzi huo.
 
Katika uchaguzi huo uliofanyika Jumapili ya Machi 16, mwaka huu, Mgimwa alizoa kura 22, 962 ambazo ni sawa na asilimia 79.32 dhidi ya kura 5,853 sawa na asilimia 20 alizopata Grace Tendega wa Chadema na kura 150 sawa na asilimia 0.52 alizopata Richard Minja wa Chausta.
 
Msimamizi wa uchaguzi huo Pudenciana Kisaka ambaye pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa jana alimkabidhi Mgimwa hati yake ya kuchaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo.
 
Godfrey Mgimwa
Akizungumza na wanahabari baadaye Mgimwa alisema anazikumbuka ahadi zote alizotoa kwa wananchi wa jimbo hilo wakati wa kampeni zake na anajipanga kutekeleza moja baada ya nyingine.
 
“Kama mnavyojua nyingi ya ahadi hizo zitatekelezwa kupitia Ilani yetu ya CCM; nachowahakikishia wananchi wangu wawe na imani kwani mambo yatatekelezwa,” alisema huku akiwashukuru wapiga kura wa jimbo hilo kwa kumpa ushindi wa kishindo dhidi ya wapinzani wake.
 
Pamoja na Chadema kuleta wabunge wake wote siku tatu kabla ya uchaguzi huo na kutumia chopa kwenye kampeni zake kabla ya kuitumia kulinda kura siku ya uchaguzi, Mgimwa alimgaragaza mgombea wa Chadema hata katika kata zilizokuwa zikielezwa kuwa ni ngome ya chama hicho.
 
Kata hizo ni pamoja na Ifunda ambayo Mgimwa alipata jumla ya kura 1,627 dhidi ya 601 alizopata mgombea wa CCM na 13 za mgombea wa Chausta.
 
Nyingine ni Nzihi ambayo CCM ilipataa kura 1,793 dhidi ya 606 za Chadema na saba za Chausta.
 
Katika kata ya Magulilwa ambako mgombea wa Chadema ndiko anakotokea, Mgimwa alifanya vizuri zaidi kwa kupata kura 2,065 dhidi ya kura 549 za Chadema.
 
Matokeo ynayofana na hayo yalitokea pia katika kata zingine zote za jimbo hilo; wakati Mgimwa akipata kati ya kura 1,500 na 3,000, mgombea wa Chadema alipata kati ya kura 200 na 700 tu.
 
Grace Tendega
Tendega akizungumza na wanahabari
Akizungumza na wanahabari nje ya iliyokuwa kambi ya Chadema mjini Iringa ya CK Lodge, Tendega alianza kwa kumshukuru Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe na viongozi wengine wote walioshiriki kampeni za chama hicho.
 
Huku baadhi ya wafuasi wa chama hicho wakiangua kilio alisema; “Ninawashukuru makamanda wenzangu na wanaharakati waliokuwa wanapigania haki Kalenga, wafuasi na wanachama wa Chadema wote, nawapa pole na hongera kwa kuanza na kumaliza uchaguzi huu uliokuwa na dosari nyingi,” alisema.
 
Alisema maapambano ya ukombozi yana changamoto nyingi na kwamba huo ni mwanzo wa safari ya mabadiliko makubwa nchini, pale walipokesea mbele ya safari watajipanga upya.
 
Benson Kigaila
Kigaila akisisitiza kuyakataa matokeo
 
Katika mkutano huo na wanahabaari, Mkurugenzi wa Oparesheni wa Chadema, Benson Kigaila alisema Chadema haiyakubali matokeo hayo japokuwa haitakakata rufaa mahakamani kuyapinga.
 
Alisema daftari la wapiga kura lililotumika katika uchaguzi huo sio la mwaka 2010 bali ni lile walilolilalamikia awali kufanyiwa marekebisho mwaka huu.
 
“Kuna wapiga kura wengi waliondolewa katika daftari hilo lakini wengine wengi wapya waliingizwa, tunao ushahidi tuliouwasilisha kwenye kikao tulichofanya na Tume ya Taifa ya Uchaguzi,” alisema.
 
Alisema “ni mwendawazimu pekee ndiye anayeweza kusema kwamba uchaguzi huu wa Kalenga ulikuwa huru na wa haki, vinginevyo haki ya watanzania inaendelea kuporwa kwa njia ya masunduku ya kura.”
 
Alisema yako mambo ya kisheria yaliyojitokeza wakati wa zoezi la upigaji kura ambayo watataka ufafanuzi wake kutoka kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa.
 
“Kuna gari na watu wetu hawajulikani walipo mpaka sasa, kuna wafuasi wetu walikamatwa wakapigwa na kuteswa baada ya kukamatwa na watu wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa CCM, tunataka kujua wahusika wamechukuliwa hatua gani kwasababu wanafahamika,” alisema.
 
Alisema yeye na baadhi yaa viongozi wa chama hicho hawataondoka mjini Iringa mpaka watakapopata majibu ya mambo wanayolalamikia.
 
Jimbo la Chalinze
Kigaila alisema wakimaliza kushughulikia changamoto zote zilizojitokeza wakati wa uchaguzi huo, mapambano yao watayaelekeza katika uchaguzi mdogo jimbo la Chalinze.
 
“Kule Chalinze kampeni zimekwishaanza; tukitoka Iringa breki yetu ni Chalinze; tutapita kijiji kwa kijiji kuwaeleza watanzania umuhimu wa kuichagua Chadema,” alisema.
 
Alisema katika kampeni hiyo wimbo wao mkubwa utakuwa ni fursa sawa kwa watanzania wote ili kuondokana na tabia inayojengekea ya watoto kurithi nafasi za uongozi za wazazi wao.
 
“Wote tuna haki sawa, Chadema tunataka kuona wakulima, walimu na watu wengine wa kawaida wanapata fursa katika nchi hii badala ya kuendelea kutoa madaraka kwa watoto wa wakubwa,” alisema.
 
CHANZO:FRANCI GODWIN

No comments:

Post a Comment