WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Friday, March 28, 2014

Kikwete: Tuwaache wabunge waamue serikali mbili au tatu


Rais Jakaya Kikwete
Rais Jakaya Kikwete amesema amemaliza  kazi ya kulihutubia Bunge Maalum la Katiba na sasa anawaachia wabunge wa bunge hilo kujadili na kuamua muundo wa Muungano unaofaa kama serikali mbili au tatu kwenye mapendekezo ya  Rasimu ya Katiba Mpya.
Rais Kikwete alielezea msimamo huo juzi wakati akizungumza na wazee  katika Ikulu ndogo ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga.

Rais Kikwete ambaye alikuwa katika ziara yake ya siku moja wilayani hapa, alitoa msimamo wake baada ya wazee hao kumweleza kwenye risala yao kuwa wao wanataka serikali mbili. Risala hiyo ilisomwa na   Mwenyekiti wa Wazee wa Wilaya ya Muheza, Hamisi Mzee.

Rais Kikwete alisema kwa sasa amewaachia wabunge kuamua muundo wa Muungano unaotakiwa na baadaye wananchi wataamua kama wanataka serikali tatu ama mbili wakati wa kupitisha Katiba.

Alisema kama watapendekeza serikali tatu ruksa kwani ndiyo mapendekezo yao, hivyo hayawezi kupingika kwa namna yoyote.

Hata hivyo, Rais Kikwetee alisisitiza kuwa lakini waelewe kuwa serikali tatu zina changamoto zake.
 
CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment