WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Friday, May 3, 2013

HII IMEKAAJE

  • Mitihani kidato iv kusahihishwa upya

pinda ce5dc
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Tume ilioundwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuchunguza matokeo ya mtihani wa kidato cha nne uliofanyika mwaka jana, LEO imeitaka serikali ifute matokeo yote na mitihani isahihishwe upya.


Akisoma ripoti ya Tume hiyo hivi punde bungeni Mjini Dodoma, Waziri wa Nchi Katika Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia sera na uratibu, William Lukuvi amesema kwamba mitihani hiyo inapaswa kusahihishiwa kwa kuzingatia vigezo vilivyotumika katika kusahihisha mitihani ya kidato cha nne mwaka 2011.

Mwaka jana matokeo ya wanafunzi wa kidato cha nne yalikuwa mabaya kuliko matokeo mengine yaliowahi kutolewa na Baraza la Mitihani la Taifa. Wanafunzi walifeli kwa asililimia 60.

Kutokana na matokeo ya tume hiyo, Lukuvi ameipongeza tume hiyo kwa kutoa matokeo hayo.

Wataalamu wa elimu wanasema kwamba endapo serikali itatekeleza pendekezo hilo itaingia kwenye gharama kubwa ambazo pengine zitaigharimu serikali. 

Chanzo: Habarimasai.com

No comments:

Post a Comment