WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, May 13, 2013

Azam kucheza shirikisho afrika mwakani, yaifunga Mgambo 3-0

  • azam 5e58a
Azam FC
Jana katika uwanja wao wa nyumbani Chamazi, Azam fc wameshuka dimbani kuvaana na maafande wa Mgambo Shooting kutoka mkoani Tanga “Waja leo waondoka leo” huku wakihitaji sare ama suluhu ili kupata pointi moja na kujihakikishia nafasi ya pili msimu huu.

Hatimaye dakika tisini zilimalizika kwa wachezaji John Bocco “Adebayor” aliyejuta na kuwaomba radhi watanzania kwa kukosa penati muhimu nchini Morroco, Kipre Herman Tchetche pamoja na Attudo kufunga bao moja moja na kurudisha furaha kubwa kwa mashabiki, viongozi na benchi la ufundi la klabu hiyo chini ya kocha Muingereza Sterwat John Hall.
Sasa Azam wametetea nafasi yao ya umakamu bingwa baada ya kufikisha pointi 51 na kuwachinjilia mbali wekundu wa Msimbazi Simba waliokuwa wanawania nafasi hiyo.

Afisa habari wa klabu ya Azam fc Jafar Idd Maganga amesema ushindi wa leo umetokana na mipango waliyojiwekea tangu wapoteze mchezo nchini Morroco.

Jafar alisema baada ya kutolewa na FAR Rabat walisikitika sana na wakajipanga kurejea tena katika mashindano hayo mwakani na mipango yao ilikuwa kushidna mchezo wa leo ili kuitwaa nafasi ya pili na kuiwakilisha nchi kwa mara nyingine michuano ya kimataifa na hatimaye wameweza leo hii.

“Azam imedhihirisha kuwa ni timu nzuri na inacheza soka safi, tutaendelea kuwapa burudani mashabiki wetu na sasa tunajipanga zaidi kufanya vizuri michuano ya kimataifa zaidi ya mwaka huu”. Alisema Jafar.

Jafar aliongeza kuwa baada ya ushindi wa leo wataendelea kukaa kambini kujiandaa na mchezo wa mwisho dhidi ya maafande wa JKT Oljoro katika dimba la Shekh Amri Kaluta Abeid jijini Arusha.

Azam fc msimu wa mwaka jana walikuwa katika kinyang`anyiro cha kuwania ubingwa na Simba, mwaka huu Simba kajitoa na kuwaacha wana lambalamba hao kubaki na wanajangwani katika mbio za kuwania ubingwa, lakini mbio hizo zimeishia ukingoni kwa Yanga kutwaa taji msimu huu na kupata nafasi ya kucheza ligi ya mabingwa barani Afrika mwakani. 

Chanzo: www.fullshangweblog.com

No comments:

Post a Comment