WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Tuesday, November 13, 2012

Mkutano Mkuu wa CCM ukiendelea kwa Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti leo Dodoma


Mwenyekiti wa CCM Taifa Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akiondoka katika kiti cha Mwenyekiti baada ya kujiuzu na Makamu wake wa Zanzibar Dk. Amani Abeid Karume na Pius Msekwa wa Tanzania Bara ,wakiondoka katika sehemu hiyo na kukaa sehemu maalumu kwaajili ya kupiga kura.

Mwenyekiti wa Muda wa Uchaguzi wa kumchangua Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaaf wa Tanzania Benjamin Mkapa akiongoza kikao hicho katika muda wa kupiga kura.
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa  Tanzania Dk. Kikwete Mrisho Kikwete na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, wakiwa katika nafasi maalum baada ya Mwenyekiti kujiuzulu akiwa na viongozi wengine  wakati wa kupiga kura ya kumchagua Mwenyekiti na Makamu wa Zanzibar na Bara. 
Mama Maria Nyerere, Mama Fatma Karume, na wake wa Viongozi wengine wakiwa katika ukumbi wa Mkutano wakati wa uchaguzi ukiendelea jioni hii mjini Dodoma.
Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania Dk. Mohammed Gharib Bilal, na Waziri Mkuu Mstaafu Msuya.wakibadilishana mawazo wakati wa mkutano mkuu wa CCM ukiendelea kwa hatua ya kumchagua Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Zanzibar na Bara, kulia Rais Mstaafu wa Zanzibar Dk. Salimin Amour Juma akiwa katika ukumbi wa mkutano Kizota mjini Dodoma
source: mapara blog

No comments:

Post a Comment