WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Tuesday, November 13, 2012

MATOKEO YA WAJUMBE WA NAFASI 10 ZA NEC ZANZIBAR



 Mohamed Seif Khatib
 Dr Hussein Mwinyi
 Shamsi Vuai Nahodha.
  Omar Yussuf Mze
   Samia Suluhu Hassan

 Profesa Makame Mbarawa 
---
MATOKEO  ya uchaguzi wa wajumbe wa NEC katika kura zilizopigwa juzi mjini Dodoma katika mkutano wa  nane wa Chama cha Mapinduzi (CCM) yamevuja.

Huku Mwenyekiti wa chama hicho kinachoiongoza Serikali, Rais Jakaya Kikwete akitangaza jana kuwa matokeo hayo yatatangazwa leo pamoja na matokeo ya nafasi za Makamu Mwenyekiti lakini tayari hadi jana mchana zaidi ya asiliamia 90 ya wajumbe walisha jua matokeo hayo na kuanza kupongezana huku yale ya wagombea wa bara yakiwekwa na idadi ya kura zao. 

Ingawa baadhi ya wajumbe wameoneshwa kushangazwa na idadi ya kura alizopata Katibu Mkuu wa Chama hicho Wilson Mukama kwa kushika nafasi ya 9 huku Steven Wasira akiwaongoza.

Wanaodaiwa kushinda nafasi 10 Zanzibar:
Mbunge wa Uzini, Mohamed Seif Khatib; Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Ali Mwinyi, Waziri wa Fedha Zanzibar, Omar Yussuf Mzee, Abdulhakim Chasama na  Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Shamsi Vuai Nahodha.

Wengine  ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, Khadija Hassan Aboud, Bhaguanji Mansuria, Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa na Khamis Mbeto

No comments:

Post a Comment