WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, June 3, 2013

WanaCCM Zanzibar wamshukia Maalim



Makamu wa kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharrif Hamad 


Msuguano huo unatokea katika kipindi ambacho nchi iko katika mchakato wa kupata Katiba na rasimu yake.
Zanzibar. Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa upande wa Zanzibar imemshutumu Makamu wa kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharrif Hamad kwa kumchonganisha Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein na viongozi wastaafu.
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui, Zanzibar jana, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Vuai Ali Vuai alisema kauli za Seif zinaweza kusababisha mitafaruku isiyokuwa ya lazima.
Maalim Seif, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), alikaririwa jana Jumapili akieleza kuwa marais wa zamani, Dk Aman Karume na Dk Salmin Amour walikuwa wanaunga mkono haja ya Zanzibar kuwa na mamlaka ya doka kamili ndani ya Muungano.
Akihutubia mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Kamati ya Maridhiano huko Zanzibar juzi, Maalim Seif alikwenda mbali zaidi na kumsifia Dk Karume kuwa alikuwa Rais bora wa Zanzibar.
Hata hivyo, kitendo cha Maalim Seif kumsifia Karume ni cha kushangaza kwani aliwahi kutomtambua baada ya kushindwa na Rais huyo wa zamani kwenye chaguzi za urais za miaka ya 2000 na 2005.
Vuai alisema jambo hilo linakwenda kinyume na matakwa ya Katiba ya Zanzibar na linaonyesha dharau kwa Serikali iliyokuwa madarakani.
“CCM kinalaani kwa nguvu zote kauli za uchochezi, kejeli, fitna na dharau zilizotolewa na Katibu Mkuu huyo wa CUF dhidi ya Dk Shein.
“Maalim Seif ametoa kauli zinazoweza kuleta mtafaruku wa maelewano kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa,” alionya Vuai.
Vuai pia ameipinga Kamati ya Maridhiano, ambayo ilihusika kuandaa maandamano huko Zanzibar juzi. Alistaajabu kuwepo kwa kamati hiyo yenye wajumbe sawa kutoka vyama vya CCM na CUF.
“Chama cha CCM hakijawahi kufanya kikao cha pamoja kwa kukubaliana kuunda kamati kama hiyo ya maridhiano wala hakuna kikao chochote cha CCM cha kikatiba kilichowahi kujadili na kuwateua baadhi ya wanachama wake kuwa wajumbe wa Kamati ya Maridhiano,” alisema Vuai.
Vuai alishauri wananchi wa Zanzibar kutumia fursa ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba ili kutoa ushauri kuhusu Katiba Mpya.
“Kama kuna mtu ana mawazo yake kuhusu katiba basi aheshimu mchakato wa kutoa maoni kuhusu Katiba Mpya,” aliongeza Vuai.
Malumbano haya ya CCM na CUF yanaashiria mpasuko wa ndoa ya vyama hivyo vinavyounda Serikali ya Umoja wa Taifa huko Zanzibar.

source: mwananchi

No comments:

Post a Comment