WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Thursday, June 27, 2013

Neno La Leo: Julius Nyerere Na Ushirikina Wetu....!


9 8fa48

Ndugu zangu,

 Asubuhi ya leo hapa Iringa nilishangaa kuona makundi ya watu yakitokea maeneo ya Kihesa kuelekea katikati ya mji.

Nilipouliza nikaambiwa wanakwenda kwenye maombi. Ndio, Alhamisi asubuhi, watu wanafunga safari kwenda kwenye maombi. Nimeambiwa maombi hayo ni ya siku kadhaa. Ni siku kadhaa za watu kutokufanya kazi.

 Na wengi ni watu wazima, na zaidi wanawake. Kwa kuwaangalia,

kuna wenye kwenda kuombewa kwa hofu ya kuwa wamerogwa, au wanahofia wasije wakarogwa.  Ni hofu ya ushirikina. Na wengi wanaumwa kisaikolojia. Kuna wenye kujihisi wamerogwa, ama , wanaishi na wachawi kama majirani. Hawa wako gizani kwenye wengine tunachokiona ni nuru.

 Inanikumbusha kisa cha Julius Nyerere na mwandishi wa Kimagharibi. Miezi ya mwanzo kabisa ya Tanganyika huru, mwaka 1961,  Julius Nyerere alitembelewa na mwandishi wa habari kijana wa Kimagharibi. Mwandishi yule alimwuliza Julius Nyerere, Rais kijana kwenye nchi changa  swali lifuatalo;

 “ Mheshimiwa Rais, unadhani kwa sasa ni kitu gani kimetawala fikra za watu unaowaongoza kwa maana ya Watanganyika ?”

 Julius Nyerere alitulia kidogo, kisha akajibu;
 “ Kwa kweli kilicho mbele kabisa kwenye fikra za watu wangu ni ushirikina. WaTanganyika wengi wanafikiri sana juu ya mambo ya kishirikina, hasa zaidi watu wa vijijini”.

 Miaka mingi ikapita, na kabla ya Julius Nyerere hajang’atuka uongozi, mwandishi yule alirudi tena Tanzania. Akakutana na Julius Nyerere. Akamwuliza swali lile lile la mwaka 1961, akitaka kujua Watanzania wa sasa ni kitu gani kilicho mbele kwenye fikra zao.

 Julius Nyerere hakuchukua muda mrefu kutoa jibu. Alisema;“ Ooh! Kwa sasa hali ni mbaya zaidi. Watanzania wa sasa  wanafikiri zaidi mambo ya ushirikina, na sasa si vijijini tu, hata watu wa mijini nao wanatanguliza sana mambo ya ushirikina kwenye fikra zao!”

 Ndio, msafara ule niliowaona leo asubuhi wakitokea Kihesa na kwingineko ni WaTanzania wa mijini!

Ni Neno La Leo.
 Maggid Mjengwa

No comments:

Post a Comment