WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Sunday, June 2, 2013

Maalim Seif, Karume waungana kupinga mfumo wa Muungano


Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad ametangaza kushirikiana na Rais mstaafu wa Awamu ya Sita Zanzibar, Dk Amani Abeid Karume kuhakikisha Zanzibar inapata mamlaka yake kamili.

Tamko hilo amelitoa wakati akihutubia mkutano wa hadhara uliokuwa umebeba agenda ya kujadili mabadiliko ya Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uliofanyika kwenye uwanja wa Kibandamaiti na kuhudhuriwa na wanachama wa CUF toka mikoa mitatu ya Unguja.

Maalim Seif alisema mbali na Dk Karume kazi hiyo pia itaendelea kufanywa na kamati ya maridhiano inayoongozwa na Mwenyekiti wake Waziri wa zamani wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hassan Nassor Moyo na Makamu wake Abubakari Khamis Bakari wakiwemo wajumbe wanne.

Wajumbe hao ni pamoja na mjasiriamali Eddy Riyami, mwakilishi wa Jimbo la Mji Mkongwe (CUF) Ismail Jussa Ladhu, Aliyekuwa Waziri wa SMZ Mansour YusuF Himid, Mkurugenzi wa Uenezi na Mawasiliano ya Umma wa CUF Salum Bimani.

Maalim Seif aliwaeleza wanachi kuwa Dk Karume na Kamati hiyo hawatarudi nyuma hadi pale Taifa la Zanzibar litakapopata uwakiklishi katika Umoja wa Mataifa na kuwa dola yenye mamlaka kamili kama lilivyokuwa kabla ya Aprili 26,1964.

“Madai haya si ya Seif, Karume, Jussa, Moyo au Eddy, ni sauti ya Wazanzibari wote bila kujali itikadi zao za kisiasa, kwanini tusiwe na mamlaka yetu kamili, kudai haki ni wajibu uliohimizwa na Mungu hivyo hatutakatishwa tamaa,”alisema Maalim Seif.

Alisema kwa upande wake yuko imara katika kuitetea nchi yake na kwamba dola ya Zanzibar ni kongwe kuliko Tanganyika, Malawi, Kongo, Rwanda, Uganda, Kenya na Burundi iliokuwa na mabalozi wake katika mataifa mbalimbali ulimwenguni.

Alisema kabla ya kukatwa kwa mipaka na wakoloni mwaka 1884/1885 huko Berlin, Zanzibar ilikuwa ni Taifa kamili lakini baada ya kukatwa kwa mipaka hiyo ikabakishiwa visiwa vya Pemba na Unguja pamoja na maili kumi katika masafa ya usawa wa mwambao wa Pwani.

“Nitaendelea kushirikiana na Dk Karume, Wazanzibari na kamati ya maridhiano hadi pale mamlaka kamili yatakapopatikana, mimi ndiye Maalim Seif, nishazoea kufungwa, kutukanwa, kunyanyaswa hivyo hakuna ninalolihofia katika kuipigania Zanzibar,”alisema huku akishangiliwa na wananchi.

Akiizungumzia Tume ya Katiba ya Jaji Joseph Warioba alisema ni muhimu kwa rasimu ijayo ya katiba mpya mambo kadhaa aliyoyataja yakazingatiwa ili kuipa haki Zanzibar ya kuwa na madaraka yake kamili ambayo yataisaidia kujijenga kiuchumi na kimataifa.

Akionekana kutia shaka ya wananchi wengi kutopewa vitambulisho vya ukaazi na kuandikishwa kwenye daftari la kudumu la wapiga kura, alimtaka Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein kuwa mkweli na kutimiza ahadi yake ya kumpa kila Mzanzibari kupata haki yake.
 
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

No comments:

Post a Comment