WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Friday, June 28, 2013

Kaseja atetewa



Kaseja 

Dar es Salaam.  Baadhi ya wadau wa soka, wamekosoa uamuzi wa klabu ya Simba kutangaza kumtema kipa wake namba moja, Juma Kaseja na kusema hatua hiyo imechangiwa na siasa za chuki dhidi ya kipa huyo.

Kwa wiki nzima sasa, suala la Kaseje kutemwa limekuwa gumzo kwenye vyombo vya habari, huku ikielezwa kuwa uamuzi huo umewagawa viongozi wa klabu, kwani baadhi yao wanataka aendelee kubaki.
Rafiki wa karibu wa Kaseje amelitonya gazeti hili jana kuwa, kipa huyo kwa sasa yuko nje ya jiji na kwamba anatarajia kuzungumza kwa mara ya kwanza kuhusu hatima yake Simba Jumapili wiki hii.

Mwenyekiti wa Simba na hata kocha Abdallah Kibadeni walikaririwa wakisema, kipa huyo aliyesajiliwa mwaka 2003 kutoka Moro United hatakuwamo kwenye kikosi hicho msimu ujao.

Kipa wa zamani wa klabu hiyo, Moses Mkandawile ameshutumu uamuzi wa Simba kumtema Kaseja kwani, yeye binafsi anaamini Kaseja ndiye kipa bora kwa sasa Tanzania.

“Huyu ni nahodha wa timu ya Taifa, ikiwa na maana kwamba kiwango chake bado kiko juu. Sasa iweje Simba wamteme kwa madai ya kushuka kiwango? Kweli uamuzi huu unashangaza sana,” alisema Mkandawile.

“Nadhani kuna chuki binafsi kati yake na baadhi ya viongozi ndiyo maana wengine wanapinga Kaseja kutemwa,” alisema zaidi kipa huyo wa zamani.

Aidha, Katibu Mkuu wa zamani TFF, Fred Mwakalebela naye alishangazwa na uamuzi wa Simba kumtema kipa huyo na kusema haukuzingatia uwezo wake, bali chuki kutoka kwa baadhi ya viongozi wake.

Mwakalebela alisema, anaamini Kaseja bado ni kipa mwenye uwezo wa kucheza timu yoyote kwa vile kiwango chake bado kinadai tofauti na mawazo ya watu wengine.

Kwa upande wake, mchezaji wa zamani Yanga  Kitwana Manara alisema walichokifanya kwa Kaseja siyo sahihi hata kama mpira umekwisha anatakiwa apewe heshima yake kama mchezaji aliyeitumikia klabu muda mrefu.

“Huyu ni alama ya mafanikio Simba, alipaswa kupewa heshima kubwa. Kama hawataki kumsajili, basi wangemweka kwenye benchi la ufundi,” alisema Manara.

Kwa upande wake, nyota wa zamani Taifa Stars, Peter Tino alisema masuala ya usajili waachiwe viongozi na benchi la ufundi na kwamba wasisikilize kelele za mashabiki.

“Kaseja ni kipa mzuri mpaka sasa, ana uwezo wa kucheza zaidi tofauti na wengine wanavyodhani. Apewe nafasi nyingine aonyeshe uwezo wake,” alisema Tino.

Kocha Kennedy Mwaisabula ameishauri Simba kufuta mpango wake wa kumtema kipa huyo, kwani bado ana uwezo mkubwa.

Wakati huohuo, klabu ya Yanga imekana taarifa kuwa ina mpango wa kumsajili Juma Kaseja.

Katibu wa Yanga Laurance Mwalusako alisema, wanatambua kuwa Kaseja bado ana uwezo mkubwa langoni, lakini hayuko kwenye mpango wa kumsajili kwa vile wana makipa wazuri. Kaseja aliwahi kucheza Yanga msimu mmoja, mwaka 2009.

source: mwananchi

No comments:

Post a Comment