WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, June 29, 2013

Kiwango changu bado juu

 

Juma Kaseja Juma  

Kigoma. Kipa aliyefunguliwa mlango kuondoka Mtaa wa Msimbazi, Juma Kaseja amesema taarifa za kutemwa kwake anazisikia kwenye vyombo vya habari tu, na kwamba hata kama ni kweli hazijamshtua kwa vile anaamini kiwango chake bado kimesimama kwenye mstari.
Kwa zaidi ya wiki sasa, vyombo vya habari vimekuwa vikiandika taarifa zilizokosa maelezo ya kina kuhusu kutemwa kipa huyo namba moja wa Simba na nahodha wa timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars.
Kaseja ambaye kwa sasa yuko Kigoma kwa ajili ya mapumziko, alisema anafahamu kuwa mkataba wake na Simba ulishakwisha tangu baada ya kumalizika kwa msimu uliopita, hivyo yeye ni mchezaji huru.
“Nasikia tu nimetemwa Simba, lakini kweli sijapata barua na hata kama ningejulisha, nisingeshangaa kwa sababu mkataba wangu na Simba ulishamalizika,” alisema Kaseja.
Mlinda mlango hiyo mwenye rekodi ya pekee nchini, alisema hana ugomvi na uongozi wa Simba pamoja na kutomjulisha kama hawatamwongezea mkataba.
“Sijawahi hata siku moja kujulishwa kuwa sitaongezewa mkataba mpya baada ya kumalizika uliotangulia. Hakuna kiongozi aliyeniambia lolote zaidi ya kusikia kwenye vyombo vya habari kwamba sitakiwi,” alisema Kaseja.
“Kwa sasa siwezi kuzungumza mengi kwa vile sina haki hiyo kwa sasa, muda utafika nitaongea. Napumzika huku pia nikiendelea kufanya mazoezi kwa sababu soka ndiyo ajira yangu,” aliongeza Kaseja.
Kaseja aliyeidakia Simba kwa miaka tisa mfulilizo tangu mwaka 2003, hakuwa tayari kuweka bayana mwelekeo wake kama uamuzi wa kutemwa Simba utabaki palepale.
Alisema: “Siwezi kusema lolote kwa sasa, ila muda ukifika nitaweka wazi mambo yangu. Naamini bado nina uwezo na kamwe sitakata tamaa hata kama nitaondoka Simba.”
Tangu kutangaza kutemwa kwa Kaseja zaidi ya wiki moja iliyopita, taarifa za ndani kutoka Simba zinadai kuwa uamuzi huo umezaa mgogoro chinichini baina ya viongozi.
Ingawa Mwenyekiti wa Simba Aden Rage, aliwahi kukaririwa akisema kipa huyo hatavaa jezi za Msimbazi msimu ujao, viongozi wenzake wanapinga uamuzi huo.
Kaseja aliwahi kulalamikiwa na mashabiki wa Simba mwishoni mwa msimu uliopita wakimtuhumu kucheza chini ya kiwango hali iliyosababisha kufungwa mabao ya kizembe.
Mbali na kudaiwa kushuka kiwango, kuna taarifa pia kuwa Simba imeamua kuachana na kipa huyo kutokana na kudai dau kubwa ili kusaini mkataba mpya baada ya ule wa awali kumalizika

source: mwananchi

No comments:

Post a Comment