WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, June 5, 2013

MAREHEMU ALBERT MANGWAIR AAGWA

 Ilikuwa ni simanzi kwawale hasa waliokuwa wakipata Burudani kutoka kwa Albert Mangwair na hakika aliyethibitisha kwa kuona kuwa sasa amelala na hainuki hadi Masiha atakapo rudi walishindwa kujizuia kwa vilio kama Rasta huyu kutoka Ukonga Mazizini maarufu kwajina la Simaga akitokwa na machozi baada ya kutoa heshima za mwisho kwa Mwili wa Marehemu Albert Mangwea katika viwanja vya Lidaz Kinondoni jijini Dar es Salaam. 

Mamia ya Wakazi wa jiji walijitokeza kumuaga Msanii huyo wa muziki wa kizazi kipya aliyefariki Mei 28, mwaka huu Nchini Afrika Kusini alikokuwa kwa shughuli za kimuziki. 

Mangwewa alisafirishwa mchana wa leo kwenda Kihonda mkoani Morogoro kwa mazishi yatakayo fanyika kesho.
 Huyu naye ambaye haikuweza kufahamika jina lake kwa haraka, akipiga picha huku akiangua kilio wakati wa kuaga mwili wa marehemu.....
 Wanafamilia wakipita kuaga mwili wa ndugu yao....
  Mbunge wa kinondoni  Idd Azzan anamuaga Ngwea
  P. Funky akipita kuaga na kutoa heshima za mwisho mbele ya jeneza la Mangwea
 Wasanii wa Bongo Movie wakipita kutoa heshima za mwisho kwa Mwili wa marehemu
Hata wanahabari nao kama Issa Mnali walitoa heshima za mwisho.
 Rais wa Shirikisho la Muziki Tanzania, Addo Novemba kushoto akijadiliana jambo na viongozi wa Kamati ya Mazishi katika shughuli yaa kumuaga marehemu Albert Mangwea, katika viwanja vya Leaders Club leo.
 Ras Simaga akipita na zana zake baada ya kutoa heshima za mwisho.

 Miraji Kikwete akizungumza machache na Ummy Wenselaus 'Dokii' viwanja vya Lidaz
  Sehemu ya wananchi waliojitokeza kuaga mwili wa marehemu Mangwea
   Sehemu ya waombolezaji waliokwenda kumuaga marehemu Ngwea wakionekana katika viwanja vya Leaders Club leo.
  Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Taifa Chadema (BAVICHA), John Heche wa tatu kutoka kushoto akijadiliana na viongozi wenzake waliokwenda kuaga mwili wa marehemu Albert Mangwea leo viwanja vya Leaders Club leo.
Wadau wakubwa wa kazi za Ngwair wakiwa katika pozi la majonzi.
Kamati ya Maandalizi ya Mazishi ya Ngwair ikiwa jukwaani.
 
source: Haki Ngowi

No comments:

Post a Comment