WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, June 3, 2013

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZINDUA RASIMU YA KATIBA MPYA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, KARIMJEE DAR LEO

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiinua juu na kunyesha Kitabu cha Rasimu ya Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ikiwa ni ishara ya uzinduzi rasmi wa rasimu hiyo uliofanyika leo katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, (kushoto) ni Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya, Joseph Sinde Warioba.
Meza kuu ikiwa na baadhi ya Viongozi wakuu wa Serikali na Jukwaa la Tume ya Katiba mpya.

 Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe (kulia) akiwa na baadhi ya Viongozi wenzake katika hafla ya uzinduzi wa rasimu ya Katiba hiyo.

 Baadhi ya wazee waasisi waliohudhuria hafla ya uzinduzi huo leo.

  Sehemu ya waandishi wa habari wakiwa bize kunakili kila kinachozungumza mahala hapo.


 Sehemu ya wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari, waliohudhuria hafla hiyo, wakiwajibika.Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais
 
source:haki ngowi

No comments:

Post a Comment