WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Tuesday, June 18, 2013

ICC yaamua kuhusu Ruto


ruto 14444
Mahakama ya kimataifa imeamua kuwa Naibu wa rais wa Kenya ambaye pia ni mshukiwa wa ghasia za baada ya uchaguzi Kenya, William Ruto, awepo mahakamani Hague wakati kesi yake ikisikilizwa.

Hasa mahakama inamtaka Ruto kushiriki baadhi ya vikao muhimu katika mahakama hiyo wakati kesi yake itakapokuwa ikisikilizwa kuanzia mwezi Septemba mwaka huu.
Bwana Ruto alikuwa ameiomba mahakama imruhusu ashiriki vikao hivyo kwa njia ya video kwenye mtandao wa Internet.
Mahakama imesema kuwa imemruhsu kutohudhuria vikao vingine kutokana na majukumu ya wadhifa wake.
Aidha Ruto alikanusha madai kuwa alihusika katika ghasia za baada ya uchaguzi nchini Kenya mwaka 2007 ambapo mamia waliuawa na maelfu kuachwa bila makao baada ya kufukuzwa makwao kufuatia vita vya kikabila.
Alishtakiwa na Rais Uhuru Kenyatta . Wawili hao walikuwa mahasimu wa kisiasa wakati wa uchaguzi miaka sita iliyopita.
Watu 1,200 walifariki na wengine laki tano kuachwa bila makao katika vita ambavyo nusura vitumbukize nchi kwa mapigano ya wenyewe kwa wenyewe.
Mahakama ya ICC ilisema kuwa Ruto atastahili kuhudhuria ufunguzi wa kesi yake pamoja na kikao cha mwisho ambapo wahusika wa kesi watatoa kauli yao ya mwisho kabla ya uamuzi kutolewa.
Pia atatakiwa kuhudhuria kikao ambapo jaji watatoa uamuzi katika kesi hiyo na siku ya kutolewa kwa hukumu ikiwa.
Mapema mwezi huu majaji katika mahakama ya ICC, walikubali ombi la mawakili wa Ruto, kuakhirisha tarehe ya kuanza kwa kesi dhidi yake ili wapate muda zaidi kujiandaa.
Mahakama pia imependekeza baadhi ya vikao vya kesi kusikilizwa nchini Kenya au Tanzania.
Tangazo lilijitokeza wiki chache baada ya shinikizo kutoka kwa mataifa mengine ya kiafrika kuitaka mahakama kufutilia mbali kesi dhidi ya Kenyatta na naibu wake Ruto.
Muungano wa Afrika ulisema kuwa mahakama hiyo ina ubaguzi , tuhuma ambazo mwendesha mkuu wa mashtaka katika mahakama hiyo alikanusha vikali.
Kesi dhidi ya rais Kenyatta inatarajiwa kuanza mwezi Julai. 

Chanzo: bbcswahili

No comments:

Post a Comment