WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, November 5, 2012

Mnyika Amuwashia Moto Waziri Muhongo


Mbunge wa Ubungo Mh. John Mnyika bungeni leo akiwasilisha hoja kuhusiana na Uhaba wa Mafuta nchini.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda (aliyesimama) akijibu hoja ya Mh. John Mnyika.
Na. Mwandishi wetu, Dodoma.
Mbunge wa Ubungo (CHADEMA) John Mnyika akihoji kiti cha spika juu ya serikali kushindwa kuleta bungeni kauli ya serikali juu ya mkakati wa serikali kukabiliana na uhaba wa mafuta nchini Tanzania.
Uhaba wa mafuta leo umewakimbiza kwenye kikao cha bunge mjini Dodoma asubuhi, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na naibu mawaziri wake George Simbachawene na Steven Masele.
Waziri huyo na naibu mawaziri wake hawakuwepo bungeni leo wakati Mbunge wa Ubungo (CHADEMA) John Mnyika alitaka serikali itoe sababu ya kutokuja bungeni leo kutoa tamko la serikali ya jinsi inavyoshughulikia swala la uhaba wa mafuta nchini.
Spika wa Bunge Anne Makinda alimlazimisha Waziri kuu Mizengo Pinda kusimama na kujibu hoja ya Mnyika aliyemtaka Spika kulazimisha serikali ijibu hoja  yake pamoja na mkakati wa serikali wa kutatua uhaba wa mafuta nchini.
Waziri Mkuu  Mizengo Pinda alilazimika kunyanyuka nakusema kwa ufupi kuwa serikali ilikuwa ikijiandaa na kuja na hoja nzito ya kueleza umma mikakati kabambe ya kutatua uhaba wa mafuta nchini.
source mjengwa. blog

No comments:

Post a Comment