WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Thursday, November 15, 2012

Kaseja na Mashabiki wa Simba


Ndugu zangu wanamichezo wa nchi hii, ni ukweli usiofichika hii filamu ya mashabiki wa simba juu ya tuhuma za kipa wao aliyetumikia timu yao kwa  kipindi kirefu na kuwapa mafanikio mengi ikiwemo ubingwa ligi kuu ni filamu mbovu kuwahi kutokea katika nchi hii, 

Filamu hii niliyoibatiza jina Kaseja & Simba Fans ni filamu ambayo haina mvuto haileweki washiriki inaonekana hawakujiandaa vyema kushiriki filamu hii inaonyesha wazi washiriki wasivyo na talent kama ilivyokuwa kwa kina marehemu steven kanumba, vicent kigosi, Monalisa na wengine wengi wa kwenye tasnia ya Bongo Movie.

Filamu hii imebeba ujumbe wa ya kuwa kaseja sasa hatakiwi kuitumia timu ya simba, haina utofauti na filamu fulani ya nchini Nigeria mtoto ambaye alikataliwa kwao ila wale wanaigeria waliweza kufikisha ujumbe katika jamii kupitia filamu yao ile, maana katika jamii wapo watu wanaofukuza watoto zao hata kwa kisa ambacho kinavumilika leo usishangae mama kamchoma mwanae tena wa kumzaa mikono kwasababu kadokoa nyama jikoni.

Tujiulize ndugu zangu watanzania mashabiki wa soka je kupitia filamu hii ya kaseja & simba fans tumepata ujumbe gani kama jamii ya wapenda michezo je hali hii inafundisha nini kizazi cha kesho katika tasnia ya michezo ya nchi hii, mimi nashauri mashabiki wa simba warudi kwa director wao wa Filamu hii waandike upya script watoe part 2 itakayoonyesha kurudisha imani kwa kipa wao namba moja Juma Kaseja ili mzunguko wa pili wa ligi hali isije kuwa mbaya zaidi.

Pamoja tujenge michezo

Capt Mkami Jr

No comments:

Post a Comment