WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, November 14, 2012

IKULU:Rais Jakaya Kikwete Akutana na Sekretarieti Mpya ya CCM Ikulu Mjini Dodoma




 Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Katibu Mkuu wa CCM aliyemaliza muda wake Dk.Wilson Mukama ikulu ndogo mjini Dodoma leo asubuhi. Dk.Mukama ameteuliwa kuwa Mkuu wa Chuo cha Uongozi  cha CCM.
Mwenyekiti wa CCM Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Katibu mpya wa oganaizesheni  ya CCM Bwana Mohamed Seif Khatib mjini Dodoma
 Mwenyekiti wa CCM Dk. Jakaya Mrisho  Kikwete akiwa na Naibu Katibu Mkuu mpya wa CCM, Mwigulu Nchemba ikulu ndogo mjini Dodoma leo asubuhi.
 Mwenyekiti wa CCM Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akifurahia jambo pamoja na Makamu mweyekiti mpya wa CCM Bara, Philip Mangula (Katikati) pamoja na Makamu Mwenyekiti Bara aliyemaliza muda wake Bwana Pius Msekwa ikulu ndogo mjini Dodoma
Mwenyekiti wa CCM Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete (wapili kushoto) akizungumza na Makamu wa pili wa Rais Zanzibar Balozi Sefu Iddi,Makamu mpya wa CCM Bara Bwana Philip Mangula(watatu kushoto) pamoja na makamu wa CCM Bara aliyemaliza muda wake Bwana Pius Msekwa.
Mwenyekiti wa CCM Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa pamoja na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein (kushoto) pamoja na Makamu Mwenyekiti  mpya wa CCM Bara, Philip Japhet Mangula (kulia) ikulu ndogo mjini Dodoma. Picha zote na Freddy Maro-IKULU

No comments:

Post a Comment