WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, February 13, 2013

Nigeria mabingwa Afcon 2013



Wachezaji wa Timu ya Taifa ya Nigeria,wakishangilia baada ya kutwaa Taji ya Mataifa ya Afrika kufuatia kuifunga Burkina Faso bao 1-0. 
NIGERIA ilitawala mchezo wa fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika na kuifunga Burkina Faso bao 1-0 na kutwaa taji mjini, Johannesburg, Afrika Kusini.
Sunday Mba alikuwa shujaa wa ushindi wa Nigeria (Super Eagles) baada ya kufunga bao pekee dakika tano kabla ya filimbi ya kutenganisha nusu ya mchezo huo mkali ulioshuhudiwa na watazamaji 85,000.
Wilfried Sanou angeweza kusawazisha bao hilo kwa Burkina Faso (Stallions) katikati ya kipindi cha pili, shukrani kwa kipa wa Nigeria Vincent Enyeama aliyecheza vizuri kuokoa hatari hiyo.
Ilikuwa mechi ya kwanza kwa Nigeria hatua ya fainali tangu mwaka 2000, na walikuwa wakipewa nafasi kubwa ya kutwaa taji mbele ya Burkina Faso, taifa dogo Afrika Magharibi.
Burkina Faso haijawahi kuifunga Nigeria katika mechi 12 walizokutana katika mashindano mbalimbali, na hiyo ilitosha kuipa Nigeria nafasi ya kushinda mchezo. Efe Ambrose alikuwa na nafasi tano za kufunga kipindi cha kwanza, lakini ya kukumbukwa zaidi ni pale alipopiga juu mpira akimalizia kiki ya adhabu ndogo kutoka kwa Victor Moses ndani ya dakika saba tangu kuanza mchezo.
Nigeria waliotawala mchezo kwa kiasi kikubwa, walikaribia kufungwa kama siyo, Aristide Bance kupoteza nafasi nzuri ya kufunga baada ya shuti lake la mita 25 kukosea shabaha na kwenda nje ya lango huku.
Nigeria wangeweza kufunga bao la pili kama Ideye angetumia vizuri pasi aliyopewa kuusindikiza kirahisi mpira wavuni, lakini akaishia kupiga nje.
Huo ni ubingwa wa tatu kwa Nigeria, lakini wa kwanza kwa tangu mwaka 1994 walipotwaa mara ya mwisho baada ya kuifunga Zambia mabao 2-1 katika mchezo wa fainali.
REKODI
Nigeria:
Kocha wa Nigeria, Stephen Keshi anakuwa kocha wa pili kama mchezaji kutwaa taji na pia kama kocha katika historia ya michuano hiyo, akiungana na Mahmoud Al Gohari wa Misri.
Nigeria ina rekodi ya pekee ya kiwango cha ubora wa soka duniani (Fifa), kwani ndiyo timu pekee Afrika iliyowahi kushika nafasi ya tano duniani mwaka 1994. Kwa sasa inashika nafasi ya 52.Kwa mara ya kwanza Nigeria ilicheza fainali za Kombe la Dunia mwaka 1994, ikiwa kundi moja na Bulgaria, Ugiriki na Argentina na kufanikiwa kuongoza kundi lake.
Iliifunga Bulgaria 3ñ0, ikapoteza kwa kufungwa mabao 2-1 na Argentina na kufanikiwa kusonga mbele raundi ya pili baada ya kuifunga Ugiriki mabao 2ñ0.
Katika raundi ya pili, Nigeria ilicheza na Italia, ambapo mpaka dakika 25 za kwanza tayari walikuwa wakiongoza kwa bao 1-0 lililofungwa na Emmanuel Amunike.
Source: Mwananchi

No comments:

Post a Comment