WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Friday, February 1, 2013

MUUNGANO UKIVUNJIKA NINI KITATOKEA?



seif 43e19
Katika mfumo gandamizi watawala wakitumia system zao za propaganda potofu wameweza kuteka fikra za watu kwa sababu maalumu za kulinda nafasi zao: Ukisema ukweli mweupe usiokuwa na doa hata chembe moja, basi utaambiwa aidha wewe ni Mchochezi au una Jaziba! Haya maneno mawili ni silaha kubwa sana ya tawala gandamizi kote duniani, na maneno haya yamesaidia sana
kuwadhibiti wale wote wanaopenda kudai haki zao au haki za watu wengine. Watawala wanapowagandamiza raia hawaelewi kabisa kwamba wao ndiyo wanaoweka jiwe la msingi wa Uchochezi, lakini wale wanaoonewa na kugandamizwa wanapotaka kujinasua toka mikononi mwa wagandamizaji, tayari wameshaonekana wanataka kutoka, hivyo neno linalotumiwa ili kuwadhibiti ni “Uchochezi” ! Sasa mchochezi hapo ni nani!? Mchochezi ni yule anayeukataa Ugandamizaji, au Mchochezi ni yule Anayemgandamiza mwenzie!? Hapa huhitaji kusomea sheria ili ujibu maswali haya.
Wakati wa utawala wa Idd Amin waandishi wa habari walioandika kwamba Amin anauwa watu; utawala wake uliwaita waandishi hao kwamba ni wachochezi! Viongozi wa kidini waliokemea mauaji ya Idd Amin waliambiwa wana ni Wachochezi na wana Jaziba! Jella anaposema nchi hii kuna mbegu mbaya ya udini ambayo inaharisha amani ya nchi hii; anaambiwa aache Jaziba!  Na wakati mwingine anaweza kutokea mwanasiasa akasema niache Uchochezi!
Mwaka 1990 kuna mcheza sinema mmoja wa Kimarekani Spike Lee alicheza sinema inayoitwa “Do the Right Things”, sinema hii inaonyesha jinsi mfumo gandamizi ulivyokuwa unawagandamiza watu weusi na kujiona kwamba wapo sahihi kufanya hivyo; na watu weusi nao badala ya kufuata taratibu za kisheria, wao wakaamua kupata haki kwa kutumia nguvu; na katika mazingira kama haya wote walipoteza: Wagandamizaji na Wagandamizwaji! Ndiyo maana sinema hii inatufundisha kwamba kila mtu afuate sheria; watu wote wapo chini ya sheria moja bila ya kujali imani za dini zao, rangi zao, elimu zao, kazi zao, makabila yao, uwezo wao kifedha au nyadhifa zao.
Kutumia Maneno ya Jaziba au Uchochezi tukidhani ndiyo tunadumisha Amani na Utulivu kama tulivyozoea kusema; tutakuwa hatupo sahihi asilimia mia moja; bali usahihi ni kutafuta chanzo cha tatizo na kuangalia ni namna gani tunaweza kulitatua bila ya kuidhuru jamii inayotuzunguka.
Wote tumezaliwa hapa hapa, tumesoma hapa hapa, tunaishi hapa hapa, tunafanya kazi hapa hapa, tunazeekea hapa hapa, tutastaafu hapa hapa, tutafia hapa hapa, na tutazikwa hapa hapa, lakini hatujui mambo ya hapa!
A. Ukishabikia Udini, ukajiona kwamba dini yako ni bora kuliko dini zingine, basi jua kwamba Dhehebu lako halikubaliki!
B. Ukishabikia Dhehebu, ukajiona dhehebu lako ni bora kuliko madhehebu mengine, basi jua kwamba Kabila lako halikubaliki!
C. Ukishabikia Ukabila, ukajiona Kabila lako ni bora kuliko Makabila mengine, basi jua kwamba Elimu yako haikubaliki!
D. Ukishabikia Elimu, ukajiona Elimu yako ni bora kuliko Elimu za wengine, basi jua kwamba kazi zako hazikubaliki!
E.  Ukishabikia Kazi, ukajiona Kazi zako ni bora kuliko kazi za wengine, basi jiandae kwa lolote, na kwa wakati wowote kwa vile Wanakitengo wapo kazini watakutafutia tu sababu na watakubana!
Dr. Jella
source: mjengwablog.com

No comments:

Post a Comment