WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Friday, February 22, 2013

NENO LA LEO: KARANGA YA MWISHO...!


Photo: Neno Fupi La Usiku Huu: Karanga Ya Mwisho...!
Ndugu zangu, 
Juzi hapa nilikuwa nafatuna karanga huku nikitafakari sana. Jamaa aliyekaa jirani yangu akaniuliza; " Kaka mbona unafikiri sana ukila  karanga zako kiganjani?"
Nikamjibu, kuwa nafikiri juu ya karanga ya mwisho nitakayoitafuna. Kwamba naziangalia karanga zangu mkononi nikiitafuta ile itakayokuwa ya mwisho kuitafuna. 
Kwa mwanadamu, suala si kutafuna karanga tu, bali, umuhimu wa kujua kitakachotokea kwa karanga ya mwisho. Maana, unaweza kutafuna karanga tamu, lakini, karanga ya mwisho ikiwa imeoza, basi, itaharibu utamu wa karanga zote ulizotangulia kuzitafuna. 
Hivyo, ni heri karanga mbovu iwe ya kwanza kutafunwa, kama utapata bahati mbaya hiyo. 
Swali; Je karanga ya mwisho ikiwa tamu sana itakuwaje?
Jibu; hilo ni jambo la kheri,  maana, hata hapo katikakati ukiwa umetafuna karanga mbovu, karanga ya mwisho itafuta machungu ya karanga mbovu ulizotafuna.
Na kwa mwanadamu karanga ya mwisho ikiwa tamu sana, basi, usiwe na tamaa ya kutafuna karanga nyingine. Utaambulia zenye mang'onying'onyi. Na hutakuwa tena na hamu ya kuonja karanga!
Naam, tafakari karanga yako ya mwisho!
Na hilo ni Neno Fupi La Usiku Huu.
Maggid Mjengwa,
Dar es Salaam
0788 111 765

Ndugu zangu, 
Juzi hapa nilikuwa nafatuna karanga huku nikitafakari sana. Jamaa aliyekaa jirani yangu akaniuliza; " Kaka mbona unafikiri sana ukila karanga zako kiganjani?" Nikamjibu, kuwa nafikiri juu ya karanga ya mwisho nitakayoitafuna. Kwamba naziangalia karanga zangu mkononi nikiitafuta ile itakayokuwa ya mwisho kuitafuna. 


Kwa mwanadamu, suala si kutafuna karanga tu, bali, umuhimu wa kujua kitakachotokea kwa karanga ya mwisho. Maana, unaweza kutafuna karanga tamu, lakini, karanga ya mwisho ikiwa imeoza, basi, itaharibu utamu wa karanga zote ulizotangulia kuzitafuna. 

Hivyo, ni heri karanga mbovu iwe ya kwanza kutafunwa, kama utapata bahati mbaya hiyo. 

Swali; Je karanga ya mwisho ikiwa tamu sana itakuwaje?
Jibu; hilo ni jambo la kheri, maana, hata hapo katikakati ukiwa umetafuna karanga mbovu, karanga ya mwisho itafuta machungu ya karanga mbovu ulizotafuna.

Na kwa mwanadamu karanga ya mwisho ikiwa tamu sana, basi, usiwe na tamaa ya kutafuna karanga nyingine. Utaambulia zenye mang'onying'onyi. Na hutakuwa tena na hamu ya kuonja karanga!

Naam, tafakari karanga yako ya mwisho!

Na hilo ni Neno la Leo.

Maggid Mjengwa,
Dar es Salaam
0788 111 765

No comments:

Post a Comment