WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Tuesday, April 22, 2014

Sitta aifuata Ukawa Z’bar


Dodoma/ Z'bar. Wakati viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakiweka kambi Zanzibar, Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta jana naye alitumia siku nzima visiwani humo akikutana na baadhi ya viongozi wa Serikali, katika kile kinachotafsiriwa kuwa kulinusuru Bunge hilo.
Habari zilizolifikia gazeti hili kutoka Zanzibar zinasema Sitta alikutana na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein, Makamu wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharif Hamad, Rais Mstaafu, Aman Karume na mwanasiasa wa siku nyingi wa CCM, Mzee Hassan Nassor Moyo.
Zanzibar kwa sasa ndiyo moyo wa upatikanaji wa Katiba Mpya kutokana na wajumbe wake katika Bunge kutegemewa ama kuipitisha au kuikwamisha kwa kuwa kila upande kati ya mbili zinazovutana, hauna uhakika wa kupata theluthi mbili za kura.
Baada ya kuondoka bungeni na kutangaza kususia vikao vya Bunge hilo Aprili 16, mwaka huu, siku mbili baadaye viongozi wa Ukawa waliingia Zanzibar wakitaka kufanya mikutano ya hadhara kuwaeleza wananchi sababu za kufanya hivyo, lakini wakazuiwa na polisi na hadi jana walikuwa wanasubiri kibali. (J M)
Safari ya Sitta
Katibu wa Bunge Maalumu, Yahya Khamis Hamad pamoja na kuthibitisha ziara ya Sitta Zanzibar kuwa alikuwa akutane na Dk Shein, alisema hafahamu lolote kuhusu mkutano wake na Maalim Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CUF.
"Sifahamu malengo ya safari wala walichokwenda kuzungumza, ila ni kweli kwamba alifika Zanzibar leo (jana) na alitarajiwa kuondoka jioni kurejea Dodoma," alisema Hamad na kuongeza:
"Hilo la kuonana na Maalim Seif silifahamu ila ninachojua aliniambia nimfanyie miadi ya kuonana na Dk Shein na nikaifanya kama alivyoelekeza."
Mapema habari zilizolifikia gazeti hili kutoka Zanzibar zilisema, Sitta baada ya kukutana na Karume, Shein na Mzee Moyo alitarajiwa kukutana na Maalim Seif saa 9:00 alasiri.
Katibu wa Maalim Seif, Issa Kheri Hussein alithibitisha kwamba Sitta alikutana na kiongozi huyo nyumbani kwake, Mbweni saa 9:30 alasiri jana, lakini alidai kutokuwa na taarifa za mazungumzo hayo.
"Hilo naweza kulithibitisha kwamba mkutano huo umefanyika lakini mazungumzo yenyewe yalikuwa ya faragha na mimi baada ya Sitta kufika niliondoka, hivyo sikuweza kufahamu kilichozungumzwa kwa undani, pengine mpaka nizungumze na Maalim mwenyewe," alisema Hussein.
Ziara ya Sitta kwenda Zanzibar imekuja wakati ambao kumekuwa na wasiwasi mkubwa wa kukwama kwa vikao vya Bunge hilo kutokana na msimamo wa Ukawa.
chanzo mwananchi

No comments:

Post a Comment