WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Sunday, April 13, 2014

PICHA ZAKWANZA ZA MAKAMU WA RAIS, MKUU WA MKOA NA KAMANDA KOVA BAADA YA AJALI YA HELIKOPTA


Screen Shot 2014-04-13 at 4.01.50 PM
Asubuhi April 13 2014 makamu wa Rais Dr. Mohammed Gharib Bilal, mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Said Mecky Sadick na Kamanda wa polisi kanda maalum ya Dsm Suleiman Kova walipata ajali ya Helikopta iliyoanguka uwanja wa ndege Dar wakitaka kutembelea sehemu zilizo athirika na mafuriko.
Mwandishi mmoja aliekuepo kwenye ndege hiyo aliongea kwa
ufupi anasema wakati wanaanza kupaa, ni kama upepo mkali ulikua unaivuta Helikopta kurudi nyuma ikiwa imepaa urefu wa kama futi tano ambapo ilizidiwa nguvu na kugonga paa kisha ikaanguka.
Baada ya ajali walijitazama wakaona ni wazima isipokua michubuko midogomidogo kisha wakarudi kwenye magari yao na kuyatumia kuelekea moja kwa moja kwenye maeneo waliyokua wamepanga kwenda kwa Helikopta.
Screen Shot 2014-04-13 at 3.58.45 PM 
Makamu wa Rais akionyeshwa na katibu mkuu wa wizara ya ujenzi Injinia Mussa Iombe, sehemu ya daraja la Mpiji linalounganisha Bagamoyo na Dar es Salaam lililokatika kutokana na mvua kubwa.
Screen Shot 2014-04-13 at 4.01.43 PM 
Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal akitoa maelekezo kwa katibu mkuu wa wizara ya Ujenzi Injinia Mussa Ibrahim Iombe wakati alipotembelea kukagua maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Mpiji lililokatika kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha, katikati ni mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Said Mecky Sadick.
Screen Shot 2014-04-13 at 4.01.33 PM 
Malori yakiendelea kumwaga vifusi vya mawe kwenye daraja hilo
Screen Shot 2014-04-13 at 4.01.26 PM 


Screen Shot 2014-04-13 at 4.01.19 PM 
Nguzo za umeme baada ya kuzidiwa nguvu na maji yaliyobomoa daraja.

Screen Shot 2014-04-13 at 3.59.11 PM
Screen Shot 2014-04-13 at 3.59.03 PM
Screen Shot 2014-04-13 at 3.58.54 PM
Screen Shot 2014-04-13 at 4.01.59 PM
Screen Shot 2014-04-13 at 4.02.06 PM 
Picha zote zimepigwa na OMR
 
source: blog ya mwananchi

No comments:

Post a Comment