WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Sunday, April 13, 2014

MATENGENEZO YA KUREJESHA MAWASILIANO YA BARABARA KATI YA DAR – BAGAMOYO YAENDELEA

daraja_9d19c.jpg 

Sehemu ya barabara iliyoomole katika Daraja la Mpiji kwenye barabara ya Dar es Salaam Bagamoyo
magufuri_4_d837d.jpg
Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (mbele wa kwanza kulia) akiongozana na Viongozi wengine wakati walipotembelea kukagua sehemu ya barabara iliyobomoka katika barabara ya Dar – Bagamoyo. Wengine kutoka kushoto ni; (Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam) Suleiman Kova, (Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam) Mhe. Said Mick saddik na (Mbunge Mteule wa Chalinze) Mhe. Ridhiwan Kikwete.
Mawasiliano ya barabara kati ya Dar es Salaam na Bagamoyo yamejifunga kutokana na barabara hiyo kubomolewa na maji katika Daraja la Mpiji mpakani mwa mikoa wa Dar es Salaam na Pwani.
Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli alifanikiwa kufika katika eneo hilo mara tu baada ya kupokea taarifa za kukatika kwa barabara hiyo. Akiwa ameongozana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Alhaj Mussa Iyombe pamoja na watendaji wengine kutoka TANROADS, Waziri Magufuli amewaagiza watendaji hao kuhakikisha kuwa wanafanyakazi mchana na usiku ili barabara hiyo muhimu na yeye kupitisha magari mengi ifunguliwe mapema iwezekanavyo.
Zaidi ya maelekezo hayo, Mhe. Magufuli pia ameagiza kuahirishwa hadi itakapopangwa baadaye kwa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa TANROADS ambalo lilikuwa limepangwa kufanyika kuanzia siku ya Jumanne ya tarehe 15 Aprili 2014 huko mkoani Tanga. Hatua hiyo imechukuliwa ili watendaji hao wabaki katika vituo vyao vya kazi hadi hali ya mvua zinazoendelea kutulia na taarifa nyingine kutolewa.
Akizungumzia hali katika eneo hilo la Mpiji, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Alhaj Mussa Iyombe kwa upande mwingine alibainisha kuwa kilichozolewa na maji ni sehemu ya barabara na siyo daraja lenyewe la Mpiji.
Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbali mbali hapa nchini zimesababisha madhara kadhaa kwa upande wa miundombinu ya barabara. Waziri Magufuli ameendelea kutahadharisha kuhusu shughuli za uchimbaji wa mchanga zinazofanywa karibu au chini ya madaraja, kwamba kwa maeneo mengi ndicho chanzo cha mito kuhama kutoka katika njia yake ya asili na kubomoa barabara. “Kama manavyoona daraja lenyewe ni zima na linauwezo mkubwa wa kupitisha maji lakini mto umehama kutokana na uharibifu wa mazingira” alisistiza Mhe. Magufuli.
Daraja la Mpiji lilifunguliwa rasmi mwezi Julai 2005 na Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete wakati huo akiwa ni Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
TANROADS kwa kushirikiana na kampuni za ujenzi za SKOL na Estim Construction Company Limited zote za Dar es Salaam tayari wameanza kazi za kurekebisha sehemu hiyo.(MARTIN NTEMO) (FS)

source: mjengwa blog

No comments:

Post a Comment